1.Fungua akauti NMB,mshahara wako utapitia benki hii.2.Ripoti mapema(tarehe za mwanzo).Jaza fomu utakazopewa na mwajiri kwa usahihi.3.Ukishajaza fomu, zikabidhi kwa wahusika(wengine wanaondoka nazo).4.Nenda karipoti shule uliopangiwa na hakikisha mkuu wa shule anaandika barua kumtaarifu mwajiri wako kwamba umesharipoti.Usipofanya hivyo mshahara wako utachelewa.5.Kama mambo yako hayajakaa vizuri,na unataka ukayaweke sawa usitoroke,omba ruhusa.6.Mheshimu mkuu wa shule utakaemkuta maana yeye ndio kila kitu.Ukipuuza hili yatakukuta yakukukuta.Utaichukia hii kazi.7.Ukikuta shule inampasuko(kuna makundi baina ya walimu) uwe makini,usijiunge upande wowote,uwe neutral itakusaidia.8.Epuka uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi.Utaozea jela.9.Piga kazi sio majungu.10.Wakumbuke waliokufikisha hapo(waliokulea na kukusomesha).MUNGU akusaidie kutekeleza hayo,Amen.