Habari wapendwa.
Mimi ni Mtanzania ambaye nimebahatika kumaliza elimu ya Sayansi ya Kompyuta (BS CS) katika chuo kikuu kimoja hapa Tanzania.
Mimi siyo mwalimu kwa taaluma (professional) ila nimekuwa katika tasnia ya elimu kwa zaidi ya miaka mitano nikifundisha masomo ya Physics na Mathematics. Pia nimekuwa mwalimu wa Vyuo vya Ualimu kwa takribani miaka mitatu sasa nikifundisha masomo ya MATHEMATICS, PHYSICS, ICT na EMT kwa ngazi ya DIPLOMA na TEHAMA na HISABATI kwa ngazi ya CHETI.
Nimejaribu kutafuta nafasi serikalini ila nimegonga mwamba kwani sina vyeti vya ualimu. Wanajamii wenzangu naomba kama kuna chuo/shule chochote kina nafasi ya kazi na kinatafuta mwalimu naomba mnijulishe. Pia nina uwezo wa kufundisha masomo ya progamming language mbalimbali. Natanguliza shukrani za dhati.
Ahsanteni!
Mimi ni Mtanzania ambaye nimebahatika kumaliza elimu ya Sayansi ya Kompyuta (BS CS) katika chuo kikuu kimoja hapa Tanzania.
Mimi siyo mwalimu kwa taaluma (professional) ila nimekuwa katika tasnia ya elimu kwa zaidi ya miaka mitano nikifundisha masomo ya Physics na Mathematics. Pia nimekuwa mwalimu wa Vyuo vya Ualimu kwa takribani miaka mitatu sasa nikifundisha masomo ya MATHEMATICS, PHYSICS, ICT na EMT kwa ngazi ya DIPLOMA na TEHAMA na HISABATI kwa ngazi ya CHETI.
Nimejaribu kutafuta nafasi serikalini ila nimegonga mwamba kwani sina vyeti vya ualimu. Wanajamii wenzangu naomba kama kuna chuo/shule chochote kina nafasi ya kazi na kinatafuta mwalimu naomba mnijulishe. Pia nina uwezo wa kufundisha masomo ya progamming language mbalimbali. Natanguliza shukrani za dhati.
Ahsanteni!