Ukiwa msomaji wa kiutafiti katika kuyachunguza maandiko utagundua pia hakuna aliewahi kufunga 40 pasipo uwepo wa Mungu, Lazima Mungu awepo ndo unaweza kufanya hicho kitu na istoshe sio hiari ukiangalia Musa alifunga 40 Mara tatu mfululizo lakini ni kwamba katika hizo tatu, mbili haikuwa choice yake ila ilikuja by the way au naweza sema by circumstances au tuseme hakupenda au hakupanga. kwani alipokwenda mlimani kuchukua amri hakuambiwa afunge 40 ila kinachoonekana ni kwamba Mungu alikaa kimya mpaka akajikuta amekaa hizo siku 40 au alifundishwa hizo amri kwa siku 40. Aliposhuka chini akakuta watu wake wamejiharibu nafsi na kwa vile alishuka na nguvu ya upako na uwepo wa Mungu kutoka mlimani aliweza kustahimili 40 nyingine ili kuwaombea toba. na hata aliporudi mlimani hakusema nakaa 40 tena ila ni mazingira yaleyale ya awari ndo yaliyojiri. kadhalika Nabii Elia alikua anamkimbia mwanamke kwenda kule mlima wa Mungu sinai. pia tunaona Mungu alimtokea kule na ni wazi kwamba hakupanga kufunga siku 40 ila ilijikuja by the way na pia kumbuka aliletewa chakula kabla ya huko kufunga kwake aliletewa na malaika chakula kutoka juu. pia hata Bwana wetu Yesu Kristo hakusema anaenda kufunga siku 40 au biblia haikusema Yesu aliongozwa kwenda kufunga, hapana ila inasema ilongozwa kwenda jangawani HATA baada ya siku 40 aliona njaa. kwa hiyo alipoongozwa na Roho kwenda jangwani very likely pia hata yeye hakuambiwa afunge ila kwa vile Roho alimuongoza kwenda jangwani (kiufunuo jangwani ni mahali ambapo mahitaji ya mwili wa nyama hayapatikani) na pia nionavyo Roho baada ya kumfikisha huko jangwani alimtelekeza huko jangwani pasipo chakula wala maji. na hii ilikua kwa sababu aweze kujustifiy kutukomboa kutoka katika nguvu ya majaribu ili kwamba pasiwe na jaribu ambalo linaloweza kuvuka hapo kwa maana kwamba kila pigo tutakalopitishwa maana yake hiyo dhiki haitafikia kipimo cha funga ya 40 na kwa maana hayo majaribu yote pia yatakua yameshindwa juu yetu kwa kuwa Bwana Yesu kwa kwenda kwenye kipimo cha juu cha majaribu kwa njia hiyo tumeshindiwa mapigo yetu wala sio dhambi peke yake pia na nguvu ya kushinda majaribu magumu.