Mwambie huyo rafiki yako anikome………………..!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
"Mwambie yule rafiki yako asipende kunizoea, mwambie mimi siyo Malaya. Yaani mtu anajidai wewe ni rafiki yake, halafu anakuja kunitongoza…………!"

Hebu tuchukulie kwamba kauli hiyo anaitoa mkeo au mpenzi wako………………Je wewe utachukuwa hatua gani………….?
 
Bila shaka hii ni kwa wanaume tu,nimepita kukujulia hali..
 
Bila shaka hii ni kwa wanaume tu,nimepita kukujulia hali..
Mie mzima tu hofu ni wako wewe ulioko mbali na upeo wa macho yangu...............!
 
kwanza nitamuuliza umeshagongwa nini maana huwezi kuwa mkali kiasi hicho pili ntamuuliza kaanza kukutongoza lini? hayo maswali machache nitajua nini cha kumfanya either kumuonya mshikaji au kumkimbia mpenzi wangu kimyakimya..
 
Mi naona mtu ukiwa kwenye ndoa ukitongozwa unatakiwa uhandle issue mwenyewe..
Kwa sababu women wakitongozwa kama hajamtamani huyo mtu hata kidogo ndo anakuja kukwambia...kama na yeye kadevelop hata some feelings hakuambii ng'o
 
Mie mzima tu hofu ni wako wewe ulioko mbali na upeo wa macho yangu...............!

aah mie swalama..
Back to topic:ningemwambia anithibitishie akisemacho with evidence..from there ningepata pa kuanzia
 
Ningemwambie kuwa amweleze kuwa...."yeye si malaya na ni mke/GF wa rafiki yake".......Na iakizidi kusumbua basi awe mbayuwayu!!

Mie nitakwendaje kusema hayo maneno wakati siwezi kuthibitisha pasipo shaka yoyote kwamba yeye si malaya na hatambei na marafiki zangu wengine ambao amewazimia? Bora abebe mzigo wake!

Babu DC!!!
 
Kizur kula..... Mwenyewe... Hata akikwambia ksha ukamuonya yeye au rafiki yako kama akiamua kwenda kumegwa atamegwa tu. Cha muhmu ni kusisitiza uaminifu katika mahusiano... Hawalindiki hao kama wenyewe hawajaamua kujilinda.
 

Unajickiaje na hali Babu DC?
 
Mkeo akikwambia haya maneno jua ni mtu mbaya sana na hakufai,actually akishayasema muulize...'na siku ukitiwa utakuja uniambie?'
 
Mkeo akikwambia haya maneno jua ni mtu mbaya sana na hakufai,actually akishayasema muulize...'na siku ukitiwa utakuja uniambie?'
Bishanga .....Ni kweli kabisa mkuu, maana hata mimi hawa mabinti wanaojipitisha humu JF na vimini na vipedo vyao huku wakijichekesha na kunirembulia mbona sijawa kumwambia.................awaambie wanikome?
 
Last edited by a moderator:
Bishanga .....Ni kweli kabisa mkuu, maana hata mimi hawa mabinti wanaojipitisha humu JF na vimini na vipedo vyao huku wakijichekesha na kunirembulia mbona sijawa kumwambia.................awaambie wanikome?


That will be gross irresponsibility kumweleza mwenzio mambo madogo madogo kama hayo.....!!

Babu DC!!
 
ni hatari sana kukaribisha marafiki nyumbani mara kwa mara na kuwa na mazoea ya ndani kabisa na mkeo au Gf wako, au kupenda kuwakaribisha marafiki kwenye mitoko na gf wako au mkeo, mazoea makubwa hujenga matamanio baada ya hapo...ukisafiri amakutoka watu wanaanza kudonoana..
 

maandiko matakatifu yanasema ya kuwa ushahidi wa mtu mmoja hauna nguvu mashahidi lazima wawe wawili au zaidi ya hapo......................kwa hiyo ushahidi wa mwandani wangu kamwe sitaufanyia kazi hadi pale atakapolewta shahidi wa pili.......au zaidi..................na isitoshe ni wangapi wanamtongoza na iwaje huyu tu amtaje kama siyo uchonganishi tu?
 
Nitamiomba aniambie na aliowakubalia na ku Do nao

Akiwa mke kuna issue anatakiwa kuzi handle yeye mwenyewe

Hiyo ni kwa mke wangu

Lakini kwa rafiki yangu nitafanya ajue kwamba nimetambua nini anakifanya , lakini ni Baada ya kuhakikisha
 
That will be gross irresponsibility kumweleza mwenzio mambo madogo madogo kama hayo.....!!

Babu DC!!
hapo mkuu tutabishana mpaka asubuhi,mwanamke wa kukutamkia haya maneno ni mchonganishi kizabinazabina,ukimuendekeza atakuchonganisha na ndugu.
Never entertain hii tabia mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…