Mwanadada kuhamia kwa fiance: Hii imekaaje?



Mhh hapo kazi.
Binti anaishi kwake mwenyewe.
 
Muulize huyo jemba mkiwa wawili nia yake ni ipi haswa? Na kama anania nzuri, aende kwa wazazi wenu, huku huyo dada yako akiwa karudi home mapema.

Seriously???

Unaweza kwenda kumuuliza shemeji yako mambo kama hayo kweli??

Babu DC
 
Mbona rahisi jibu,aoe ndio achukue mke, huyo mwanamme angekua dada yake angekubali kufanyiwa hivyo? mwambie dada yako asijirahisishe na aiheshimu familia, huyo ni mwanamme vyovyote itakavyo kua,kama anataka wakumfulia nakumpikia
atafute mfanya kazi.

Thanks you could not say better words than these!
 
Mwambie amshauri mchumba wake akajitambulishe nyumbani na kufuata taratibu za kikwenu. Akikataa ujue hana nia naye na anataka kumtumia tu kwa manufaa yake binafsi.
Tafakari ....

Yaah nadhani huu ni ushauri mzuri sana wa kuufanyia kazi.
 
Huyo ataishia kuwa hivyo, the day alipokubali kuwa mchumba bila idhini ya wazee. Mwache tu aendelee kumegwa kwa tamaa ya kuwa wachumba.

Anaweza kuoana but normal after 2 kids in a row, the future is unpredictable.

There you are. This is my worry too...
 
Seriously???

Unaweza kwenda kumuuliza shemeji yako mambo kama hayo kweli??

Babu DC

Unaweza kuibua tifu la ajabu na shemeji yako na hata baadaye dada yako atakugeueka na kukuona kigeugeu.
 
Unaweza kuibua tifu la ajabu na shemeji yako na hata baadaye dada yako atakugeueka na kukuona kigeugeu.


Ni jambo gumu na hadi sasa nakuonea huruma...Ongea tu na dada yako. Kama siyo sikio la kufa atakusikia tu!!

Hata hivyo uwe mwangalifu sana, kwani mwisho wa siku wewe mwenye unaweza kuwa victim mkubwa kuliko hata huyo dada yako unayejaribu kumuonea huruma!!

Hakuna mtu angependa kuona ndugu zake wanafanywa toys za kujifunzia ila kama wamekubali wenyewe...inabidi uwe mpole!!

Babu DC!!
 

Ni kweli kabisa. Inawezekana kabisa nia yangu ya kuona ndugu yangu hageuzwi toy inaweza kunitokea puani!:cool2:
Hata hivyo, nitatimiza jukumu langu kama dada
 
A big NO! mtoto ulielelewa ukaleleka huamii kwa mwanaume billa kufwata utaratibu! wanaofanya hivi either wana uhuru kupita kiasi hata wazazi hawana kauli au wamefukuzwa makwao na mimba! sasa ukioa mwanamke aliyefall kwenye category ya wazazi kutokuwa na kauli juu yake hofu ya kuvunjiaka ndoa huwa hakuna! siku mkitibuana wewe utaumia zaidi mana utataka suluhu kwa kuheshimu ndoa wakati mwenzio haogopi mtu maamuzi ni mikononi mwake! mana tunapovumilia kwenye ndoa kigezo kimojawapo ni kuogopa kuvunja heshima kwa watu wako wa karibu! sasa background matters! hata ampose basi kama hataki mambo makubwa kuchukuana kama kuku no my parents and myself was against that!
 
inaonesha dada yako hajitambui,hajui wajibu wake kwa familia,mpenziwe na taifa,inaonesha mwenzi wake ana nia njema ila anataka kutumia njia ya kujitoa muhanga kuishi na dada ako ili badae wazaz wampige fyn ya kimila ili kuweka mambo sawa,ushauri wangu ni kwa dada ako kuonesha ukomavu ktk kuweza kuishi na mwenzi wake kwa kuwa na uwezo wa kumshauri na kutetea hoja yake pasipo hisia kuwa yeye kutoka kwenu kwnd kwa hyo kijana si tatizo ila vema washirikiane kutoa taarifa kwa wazazi,yaani dada yako na mwenzi wake waende kwa wazaz wenu ili nao wajuzwe dada aendako ni kwa manufaa ya wote coz huwez jua kesho kitatokea nini kama binadam.so wazungumze kwa nia njema kwa mustakbali wa maisha yao.
 
Hebu dada yako akwambie maamuzi yake kwanza maana mambo ya mapenzi haya; unaweza ukamshauri au kumkataza mwisho wa siku wewe ndio unakuwa mbaya.
 


Twande, You have made my day.
Dada yangu asiposikia, basi atakuwa ni sikio la kufa
 

Point taken
 
asiende mana nina shost wangu alihamia toka 2007 hadi leo hajaolewa na wana mtoto..............bwana full vituko

Mara nyingi wanaume wanakuwa hivyo, maana mwanamke amejipeleka mwenyewe, na mbaya zaidi, hata kashfa hazikosekani.
 
Hebu dada yako akwambie maamuzi yake kwanza maana mambo ya mapenzi haya; unaweza ukamshauri au kumkataza mwisho wa siku wewe ndio unakuwa mbaya.

Yeye anataka kurudisha nyumba aliyopanga na kwenda kwa mwanaume, ndugu ndio tunamshauri asifanye hivyo, bali amkazanie mwanaume aende kwa wazazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…