mwanafunzi aliyemaliza udsm

aka2030

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
2,657
Reaction score
3,679
Kuna mwanafunzi alimaliza udsm mwaka jana amepata kazi hapa ofisini kwetu aithee kichwani empty brain kabisa hajui hata ethics za kazi muda wote yeye ni kushinda internet kwenye social networks huyu mwanafunzi hiyo pspa sijui aliisomaje kiukweli ni mzigo kwenye ofisi
 
So what is your point? Kwamba waliomaliza UDSM vilaza au? We uliyepost hapa hukukaa kwenye internet?
 
Wewe nawe mbona hushinda hapa JF? Umesoma chuo gani na wewe? acha ulimbukeni,vyuo havimfanyi mtu kuwa makini.Umakini wa mtu ni yeye binafsi. Nyinyi ndio mnaoamini hata kabila fualani ni nzuri kuoa na nyingine mbaya...u.j.inga kabisa!
 

Hueleweki kabisa;
  • Jamaa kakosa ethics za kazi?
  • Kushinda kwenye mtandao au
  • Empty brain?
Lipi kati ya hayo ndiyo shutma yako, vinginevyo utakuwa umeleta majungu tu hapa jukwaani.
 
Wewe umesowa chuo gani vile?
 

Kama ni kweli unachokisema, tafadhali mfundishe kazi, mkumbushe kuhusu ethics za kazi, na uache majungu juu yake. Eventually ni taifa kwa ujumla litakaloumia kwa kukosa input yake, siyo yeye!
 
muelekeze namna ya kufanya kazi na taratibu zake chuoni na kazini tofauti kabisa.
 
watu wakipindi chetu mkakosa nafasi za udsm mna chuki sana na hiki chuo!
 
kumlalamikia mtu kwa background yake ya kimasomo si tija...wewe umechukua hatua gani ili kumrekebisha?...hayo ni maneno tu,mfundishe kazi na maadili...ninaamini hata wewe ulipoanza kazi ulikuwa haufahamu kile ukijuacho leo...na vipo vingine vingi utakavyohitaji msaada...be a helping hand,itakusaidia kuliko kulalama.MSAIDIE
 
Wewe uliepost mada ndio empty brain mkumbushe mwenzako kumaliza ud ndio hoja? .Au wee unajua kila anaemaliza ud ni mungu acha woga.
 

Wewe ni Kilaza kuliko Ridhiwani, kwanini usiongee naye na kumshauri badala yake na wewe unakuja kubwabwaja JF na kujaza server.
 
Mbona kama umeleta uzi kimajungu sana, kama mzoefu kazini ulipaswa kumfuata na kumueleza kosa lake na sio kumlamba kisogo.

Inavyooneka bwana mkubwa una-allergy na wasomi wa vyuo vikuu.
 
So what is your point? Kwamba waliomaliza UDSM vilaza au? We uliyepost hapa hukukaa kwenye internet?

huyu jamaa naona ana matatizo mm nilifikiri hawezi kazi, angeleta evidence kuwa hawezi kazi tungejadili lkn maneno yake yana lengo la kujaribu kuichafua UDSM baada ya ile post ya jana iliyoonesha udsm ni chuo cha 6 Afrika kwa ubora, roho ilimuuma, mwache apoze maumivu yake, wengine tunazidi kusonga mbele
 

naona una matatizo mm nilifikiri hawezi kazi, ungeleta evidence kuwa hawezi kazi tungejadili
maneno yako yana lengo la kujaribu kuichafua UDSM baada ya ile post ya jana iliyoonesha udsm ni chuo cha 6 Afrika kwa ubora, roho ilikuuma eeh, haya poza maumivu yako kwa jinsi hiyo, wengine tunazidi kusonga mbele
 
Labda ofisi yenu ipo ipo tu haina kazi za kufanya ndio maana anaona bora ashinde kwenye internet.
 
Tatizo siyo UDSM bali yeye mwenyewe.. Hao ndiyo generation Y kama hujui-'social networks,tech-savvy, casual dress-kata K,tattoo on the neck '..
 

Una machungu na UDSM wewe,kila leo mada za kuponda flan UDSM.nafikiri unafanya michezo ya sizitaki mbichi hizi... Ha ha haaa...pole sana!
 
kuna viofisiki vingine ukifika saa 2, saa 3 kazi zimeisha halafu sheria kutoka saa 9:30 kwa hiyo mtu unakuwa na muda mwingi sana wa kutumia majamiiforums, mafacebook n.k kwa hiyo usimlaumu mtu moja kwa moja!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…