Mwanafunzi uandishi wa habari ajiua

Mwanafunzi uandishi wa habari ajiua

Michael Amon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
8,768
Reaction score
3,622
MWANAFUNZI wa Chuo cha Uandishi wa Habari Morogoro, Hemed Athuman (21), amejinyonga kw akutumia shuka baada ya kufeli mitihani.

Kamanda wa polisi mkoani hapo, Adolphina Chialo, alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:30 usiku nyumbani kwao, eneo la Mafiga.

Chialo alisema mwanafunzi huyo alikuwa anasoma Chuo cha Uandishi wa Habari Morogoro ngazi ya cheti, baada ya majibu kutoka ya kuingia semista ya pili, ilionekana hakufanya vizuri.

Kwa mujibu wa ndugu, Athuman aliacha barua ujumbe kuwa hakutendewa haki katika mitihani yake na asihusishwe mtu yeyote na kifo chake, kwani ameamua mwenyewe.

Alisema ameamua kujiua kutokana na kutotendewa haki kwenye mitihani yake huku akisema alijitahidi kusoma kwa bidii kutokana na kwamba, ndugu ndiyo waliokuwa wakimsaidia kwa sababu wazazi wake walishafariki, lakini ameona ndoto yake haiwezi kutimia.

Hata hivyo, Chialo alisema uchunguzi zaidi wa kifo hicho unaendelea. Katika lingine, mtu asiyefahamika amefariki dunia baada ya kugongwa na gari.

Chialo alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:00 usiku eneo la Makunganya barabara ya Morogoro – Dodoma, gari isiyofahamika ilimgonga mtu huyo na kusababisha kifo chake papo hapo.

Wakati huohuo, Martine Emilly (38), mkazi wa Kihonda, Manispaa ya Morogoro, akiwa katika pikipiki aina ya SanLG aligongwa na gari isiyofahamika na kufariki papo hapo.

Kamanda Chialo alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:00 usiku eneo la Makunganya, baada ya ajali hiyo kutokea mwenye gari alikimbia na polisi inaendelea na uchunguzi zaidi

 
MWANAFUNZI wa Chuo cha Uandishi wa Habari Morogoro, Hemed Athuman (21), amejinyonga kw akutumia shuka baada ya kufeli mitihani.

Kamanda wa polisi mkoani hapo, Adolphina Chialo, alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:30 usiku nyumbani kwao, eneo la Mafiga.

Chialo alisema mwanafunzi huyo alikuwa anasoma Chuo cha Uandishi wa Habari Morogoro ngazi ya cheti, baada ya majibu kutoka ya kuingia semista ya pili, ilionekana hakufanya vizuri.

Kwa mujibu wa ndugu, Athuman aliacha barua ujumbe kuwa hakutendewa haki katika mitihani yake na asihusishwe mtu yeyote na kifo chake, kwani ameamua mwenyewe.

Alisema ameamua kujiua kutokana na kutotendewa haki kwenye mitihani yake huku akisema alijitahidi kusoma kwa bidii kutokana na kwamba, ndugu ndiyo waliokuwa wakimsaidia kwa sababu wazazi wake walishafariki, lakini ameona ndoto yake haiwezi kutimia.

Hata hivyo, Chialo alisema uchunguzi zaidi wa kifo hicho unaendelea. Katika lingine, mtu asiyefahamika amefariki dunia baada ya kugongwa na gari.

Chialo alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:00 usiku eneo la Makunganya barabara ya Morogoro – Dodoma, gari isiyofahamika ilimgonga mtu huyo na kusababisha kifo chake papo hapo.

Wakati huohuo, Martine Emilly (38), mkazi wa Kihonda, Manispaa ya Morogoro, akiwa katika pikipiki aina ya SanLG aligongwa na gari isiyofahamika na kufariki papo hapo.

Kamanda Chialo alisema tukio hilo lilitokea Machi 22, mwaka huu saa 2:00 usiku eneo la Makunganya, baada ya ajali hiyo kutokea mwenye gari alikimbia na polisi inaendelea na uchunguzi zaidi


Makubwa haya. Kutotendewa haki ndio ajiue! Siku zake za kukaa ktk sayari hii, labda zilikuwa zimetimia!!
 
Makubwa haya. Kutotendewa haki ndio ajiue! Siku zake za kukaa ktk sayari hii, labda zilikuwa zimetimia!!

Amejitakia mwenyewe. Kama kweli siku zake zingekuwa zimetimia kweli Mungu angemchukua kwa njia zake mwenyewe bila ya hata yeye kujiua.
 
Hiyo nayo ni njia Mkuu,kwani we unajua mipango/njia zake Mungu?

Sijui mipango yake. Ila Mungu sio mjinga wala yeye si kigeugeu. Haiwezekeni Mungu aweke amri ya kusema usiue halafu yeye achukue uhai wako kwa kujiua mwenyewe.
 
Habari za ndani ni kwamba waliomlipia hada walimwambia akifeli awawezi kumlipia tena hada
 
Denti kaenda kupiga zake field kuzimu,subirini ataibukia hapa JF na HABARI TOKA KUZIMU.
 
Suicides zinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Utafiti unahitajika ili kubaini chanzo na pia kuona namna
ya kuwasaidia watu wanaopatwa na msongo wa mawazo na kukata tamaa.
Inasikitisha sana kuona kijana mdogo kama huyu akiamua kujiua
kama njia ya kukimbia matatizo.

Kushindwa mitihani siyo kushindwa maisha ndivyo tulikua
tunaamini huko nyuma.Inaelekea siku hizi kushinda mitihani ni
kila kitu na ndio maana tunaona wizi wa mitihani na kuibia wakati
wa mtihani vikishika kasi na kuleta matokeo mabaya sana!

Wazazi na walezi wasaidie katika kutoa elimu ya kujiamini
kwa vijana na watoto. Kadhakika viongozi wa dini na hata
viongozi wengine wakiwemo wa kijamii wasaidie kutoa elimu
kuhusu ubaya wa kujiua.
 
Suicides zinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Utafiti unahitajika ili kubaini chanzo na pia kuona namna
ya kuwasaidia watu wanaopatwa na msongo wa mawazo na kukata tamaa.
Inasikitisha sana kuona kijana mdogo kama huyu akiamua kujiua
kama njia ya kukimbia matatizo.

Kushindwa mitihani siyo kushindwa maisha ndivyo tulikua
tunaamini huko nyuma.Inaelekea siku hizi kushinda mitihani ni
kila kitu na ndio maana tunaona wizi wa mitihani na kuibia wakati
wa mtihani vikishika kasi na kuleta matokeo mabaya sana!

Wazazi na walezi wasaidie katika kutoa elimu ya kujiamini
kwa vijana na watoto. Kadhakika viongozi wa dini na hata
viongozi wengine wakiwemo wa kijamii wasaidie kutoa elimu
kuhusu ubaya wa kujiua.

Ni kweli kabisa, kwa muda wa wiki hii inayoishia leo watu watatu imejulikana wamejinyonga,acha ambao habari zao hazijajulikana, Ilianza habari ya Mkufunzi msaidizi UDSM sweden,Ikafuatiwa na Auditor wa Mahakama kuu Kimara baruti,then Mwanafunzi wa uandishi wa habari. hali ni mbaya jamani.
 
jamani msaada usiwe namashariti,watu watajimaliza mno

Lakini huo ni ujinga wake. Mimi sioni sababu ya yeye kujiua eti kwa sababu ya kufeli au kutokulipiwa ada tena. Mbona mimi baba yangu mzazi alikataa kunisomesha nikasoma kwa shida kama chokoraa nikijishibisha kwa makombo na maji ya chooni lakini hata siku moja sikuwahi kufikiria kujia kwa namna yoyote ile.
 
Suicides zinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Utafiti unahitajika ili kubaini chanzo na pia kuona namna
ya kuwasaidia watu wanaopatwa na msongo wa mawazo na kukata tamaa.
Inasikitisha sana kuona kijana mdogo kama huyu akiamua kujiua
kama njia ya kukimbia matatizo.

Kushindwa mitihani siyo kushindwa maisha ndivyo tulikua
tunaamini huko nyuma.Inaelekea siku hizi kushinda mitihani ni
kila kitu na ndio maana tunaona wizi wa mitihani na kuibia wakati
wa mtihani vikishika kasi na kuleta matokeo mabaya sana!

Wazazi na walezi wasaidie katika kutoa elimu ya kujiamini
kwa vijana na watoto. Kadhakika viongozi wa dini na hata
viongozi wengine wakiwemo wa kijamii wasaidie kutoa elimu
kuhusu ubaya wa kujiua.

Na ndio maana hata ufanisi makazini unakuwa ni mbovu kwa sababu wengi wetu tunasoma si kwa ajili ya kujifunza na kuelimika bali kwa ajili ya kufaulu mtihani na hapo ndipo tunapokosea.
 
Uhai ni bora sana kuliko anything in this world even money...
 
Hiyo nayo ni njia Mkuu,kwani we unajua mipango/njia zake Mungu?

Mungu tusimzingizie kabisa tunafanya ujinga tunasema mapenzi ya Mungu! Mungu gani huyo anayeumba watu halafu akuchukue ungali mbichi hii kitu ndio inatumaliza waafrika, tunaishi ovyo, magari twaendesha speed ajali ikitokea ni Mungu, Mungu gani huyo mbona wajapan wanaishi miaka 80 huyo Mungu wao yukoje! tumheshimu Mungu, utu, na tufanye yaliyo mema uone kama hakutakuwa na vifo vya kizembe! watu haturespect uhai wa mtu kabisa!
 
Mungu tusimzingizie kabisa tunafanya ujinga tunasema mapenzi ya Mungu! Mungu gani huyo anayeumba watu halafu akuchukue ungali mbichi hii kitu ndio inatumaliza waafrika, tunaishi ovyo, magari twaendesha speed ajali ikitokea ni Mungu, Mungu gani huyo mbona wajapan wanaishi miaka 80 huyo Mungu wao yukoje! tumheshimu Mungu, utu, na tufanye yaliyo mema uone kama hakutakuwa na vifo vya kizembe! watu haturespect uhai wa mtu kabisa!

Usemayo ni kweli kabisa bibi.
 
Back
Top Bottom