Mwanafunzi Umbwe boys afariki dunia akifanya mazoezi

Mwanafunzi Umbwe boys afariki dunia akifanya mazoezi

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Mwanafunzi wa kidato cha tano, katika Shule ya Wavulana ya Umbwe, iliyopo Kata ya Umbwe Onana, Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, Thomas Edward Kogal (19) amefariki dunia wakati akifanya mazoezi shuleni hapo.

Mwanafunzi huyo ambaye ni mwenyeji wa Mkoa wa Kigoma, anadaiwa kufariki dunia juzi jioni, Agosti 12, 2024.

Mkuu wa shule hiyo, Elirehema Mungaya akizungumza na Mwananchi jana Jumanne Agosti 13, 2024, amethibitisha kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo huku akisema alikuwa uwanjani akifanya mazoezi na wenzake.

Soma Pia:
"Ni kweli mwanafunzi wetu amefariki jana (juzi) jioni wakati akiwa uwanjani na wenzake wakifanya mazoezi, lakini alikuwa na tatizo la moyo," amesema mkuu huyo wa shule.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Agosti 14, 2024, amekiri kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo huku akisema taarifa zaidi atazitoa baadaye.
Snapinsta.app_455626508_866096488729671_8731166262999304746_n_1080.jpg
 
Hii shule ilikuwa mali ya kanisa. Irudishwe kwa wenyewe tu.
Kwamba kutokuwa ya wenyewe kunaifanya kutokea matukio kama haya?

Muhimu ni kuzingatia kanuni za afya labda washauriwe au shule zote nchini ziwe na jukumu la kuwapima kwa lazima maradhi mbalimbali wanafunzi kila mwaka ili ijulikane namna nzuri ya ku-deal na watakaogundulika kuwa na matatizo.
 
Kwamba kutokuwa ya wenyewe kunaifanya kutokea matukio kama haya?

Muhimu ni kuzingatia kanuni za afya labda washauriwe au shule zote nchini ziwe na jukumu la kuwapima kwa lazima maradhi mbalimbali wanafunzi kila mwaka ili ijulikane namna nzuri ya ku-deal na watakaogundulika kuwa na matatizo.
Warudishiwe wenyewe.
 
Ili kujirishisha. Polisi wachunguze, mtu kuumwa moyo na kifo sio mara zote vinahusiana

Hapo vimetajwa vitu vitatu katika mtiririko huu...

Matatizo ya moyo > Kufanya mazoezi > Kifo...

Sasa taarifa iliyokosekana hapa ni je hilo tatizo la moyo ni shida katika maumbile ya moyo, shinikizo la damu n.k?
 
Back
Top Bottom