Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Mtangazaji na Mwandishi maarufu wa Habari za Michezo nchini Cameroon Anye Nde Nsoh, ameuawa katika mji wa Bamenda uliopo Kaskazini Magharibi mwa nchi.
Ripoti zinasema kuwa Nsoh alikuwa kwenye baa alipovamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa kwa risasi.
Kwa miaka mingi sasa Bamenda imekuwa moja ya maeneo yaliyoathirika vibaya zaidi na migogoro iliyopo kati ya wazungumzaji wa lugha ya Kiingereza waliojitenga.
Nsoh alikuwa mtangazaji wa Dream FM Radio ya Bamenda na Mwandishi wa habari za michezo katika majukwaa mbalimbali mitandaoni.
Waandishi wengine wawili wa Cameroon waliuawa katika miezi ya hivi karibuni katika mji mkuu wa nchi hiyo Younde.
Ripoti zinasema kuwa Nsoh alikuwa kwenye baa alipovamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa kwa risasi.
Kwa miaka mingi sasa Bamenda imekuwa moja ya maeneo yaliyoathirika vibaya zaidi na migogoro iliyopo kati ya wazungumzaji wa lugha ya Kiingereza waliojitenga.
Nsoh alikuwa mtangazaji wa Dream FM Radio ya Bamenda na Mwandishi wa habari za michezo katika majukwaa mbalimbali mitandaoni.
Waandishi wengine wawili wa Cameroon waliuawa katika miezi ya hivi karibuni katika mji mkuu wa nchi hiyo Younde.