GAZETI LA MWANAHALISI LILITABIRI KILA KITU KINACHOTOKEA HIVI SASA SOMA HAPA CHINI. MWANAHALISI YA OCTOBER 6.2010.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetwishwa tuhuma nzito za kuandaa mipango ya kuchakachua matokeo ya uchaguzi mkuu ili kionekane kimeshinda, MwanaHALISI inaweza kuripoti.
Taarifa zilizosambazwa kwa maandishi katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Moshi na Mwanza mwishoni mwa wiki iliyopita, zinadai kuwa CCM imefanikiwa kupenyeza wachakachuaji kura katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Maandishi hayo hayana saini na yamechapishwa kwenye karatasi za ukubwa wa A4.