Mwanaharakati Deusdedith Soka ametoa wito kwa vijana wote Tanzania kuungana katika kupinga vitendo vya utekaji vinavyoendelea

Mwanaharakati Deusdedith Soka ametoa wito kwa vijana wote Tanzania kuungana katika kupinga vitendo vya utekaji vinavyoendelea

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Agosti 5, 2024 - Mwanaharakati Deusdedith Soka, akizungumza kwa niaba ya vijana wa CHADEMA, ameeleza changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana nchini Tanzania. Katika mkutano na waandishi wa habari, Soka ameonesha wasiwasi kuhusu ukosefu wa ajira kwa vijana, akisema kwamba licha ya vijana wengi kumaliza masomo yao, Serikali haijaweka mipango madhubuti ya kuunda ajira.

Aidha, Soka amegusia suala la ubadhilifu wa fedha za umma, akisisitiza kwamba watu waliotajwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kuhusika na ubadhilifu bado hawajachukuliwa hatua. Amesema hali hii inachangia umasikini nchini kwani fedha zinazotengwa kwa ajili ya miundombinu ni kidogo sana.

Kuhusu tukio la binti aliyebakwa na wanaume watatu, Soka ameahidi kwamba yeye na wenzake watamsaidia binti huyo kupata matibabu na haki zake. Amesema, "Ninamtaka IGP amuhakikishie usalama wa yule dada ambaye anakaa Yombo Vituka. Mimi ni mkazi wa Temeke, nitaendelea kumfuatilia suala hili hadi mwisho."

Soka pia amezungumzia Tume Huru ya Uchaguzi wa Madiwani, Wabunge, na Rais, akielezea mashaka yake kuhusu uhalali wa tume hiyo. Alisema kuwa inaonekana kama tume hiyo inataka kutumia njia zile zile za zamani na watu wale wale, jambo ambalo halitaweza kuleta matokeo tofauti.

Aidha, Soka amekemea vitendo vya utekaji vinavyoendelea katika maeneo mbalimbali nchini, akiwataka vijana wote kuungana kupinga vitendo hivyo. Alisema, "Kama tutaendelea kusema mimi ni chama fulani na kutoonyesha ushirikiano, basi matukio haya yataendelea na yanaweza kumkuta yeyote kati yetu."

Pia, Soka ameeleza kuwa ameungana na mawakili na wanaharakati wengine wa haki za binadamu ili kumsaidia binti aliyebakwa. Amemwomba binti huyo kuwatafuta ili apate msaada wa kisheria na matibabu bila gharama yoyote.

Mwisho, Soka ametoa wito kwa vyombo vya usalama kuwakamata mara moja watu wote waliohusika na tukio la ubakaji, akisema kwamba picha na video zao zimeonekana wazi.

Soma pia: Jumanne Sagini: Serikali inafuatilia kwa ukaribu matukio ya utekaji yanayoendelea Jijini Dar es Salaam/ Tamko la Masauni Waziri wa Mambo ya Ndani kuhusu madai ya kusambaa kwa matukio ya utekaji wa Watoto, asema Nchi ipo salama

Soma pia: Maboresho juu ya washukiwa wa Ripoti ya CAG

 
Vijana wa CHADEMA wakiongozwa na Deusdedith Soka wanazungumza na waandishi wa habari, leo Agosti 5, 2024

Mwanaharakati Deusdedith Soka amesema tukio la Dada aliyebakwa na zaidi ya wanaume watatu watalisimamia kwa kumtafuta Binti huyo ili apate matibabu kupata haki zake. Pia amesema "ninamtaka IGP amuhakikishie usalama wa yule dada ambaye anakaa yombo vituka na mimi ni mkazi wa Temeke nitaendanalo bampa tu bampa".

"Pia nimeshazungumza na Mawakili wengine, Wanaharakati wengine na watetezi wa Haki za Binadamu na wapo tayari kumsaidia yule dada kwa kila kitu. Kama anaisikia hii video aendelee kututafuta sehemu tulipo na atapata galamtim ya kila kitu."

Lakini watu wote waliofanya hule unyama, kwa sababu video zao na picha zao zinaonekana wakamatwe mara moja.

kufilisika kisiasa hua kuna unyonge na upweke mbaya sana.

hata hivyo hakuna namna nyingine, ni lazma kutumia fursa zote zinazojitokeza at least kua relevant kidogo kwenye medani.

ila bado sana katika kukonga nyoyo za wanainchi, kwasababu mamlaka zinadeal na jambo lenyewe sasa.
lakin pia impact yake ni duni sana na itachochea tu video hizo kusambaa zaidi, hususan kwa wasiojua chochote kutaka kuona kilichotokea 🐒

sasa hapo itakua ni kumsaidia au kumdhalilisha zaidi 🐒
 
Mzee Mbowe kiboko aisee,ameshamjenga kijana mwingine wa kichagga kuhusu kupayuka.
 
CDM hoja za majukwaani zimeisha na uhakika wa kurudi bungeni mwakani hauonekani.
 
Lakini Katiba Mpya si waliikataa wenyewe Wapinzani,waka- walk out.
Ajabu! Lipumba ambaye ndiye alikuwa mtu wa kwanza kudai Katiba Mpya, ndiyo aliyeongoza wall-out.
Kuhusu swala la ukiukaji wa Haki za Binadamu katika nchi hii.
Upo kweli ukiukaji wa Haki za Binadamu au is the matter is being overblown?
Is it correct to call this country politically immature,ambapo ukiukaji wa Haki za Binadamu ni jambo la kawaida?
 
Gen-z waitisha maandamano kusema fullstop kwa utekaji
 

Attachments

  • Screen_Recording_20240805_195126.mp4
    35.3 MB
Back
Top Bottom