Israel haina chochote zaidi ya kupaisha F 16 kupiga maghorofa kitu ambacho hata sisi na zile Mig zetu za mwaka 47 tunaweza.
Jeshi la Israel lipo weak, wachambuzi wote wa masuala ya kijeshi wanadhihirisha hilo, watu wana billion dollar weapons wanakuja kupelekeshwa na migambo ambao wakiwa watano wanapokezana AK 47 moja.
Ilipaswa waingie mtaa kwa mtaa kuwatafuta hao Hamas, wenyewe si jeshi bora? wana Intel, wana commandos na kizuri zaidi Gaza imezungukwa na Israel, wangeingia Gaza kale kaeneo ni ukubwa wa wilaya ndogo tu, ni kama Tanzania nzima inaelemewa na migambo wanakaa wilaya ya Temeke, yani JWTZ na ndege zote, vifaru, bulldozers, air defense system na kila aina ya silaha ya gharama.
Achilia mbali mmekali excuse ya wanajificha kwa raia, Hezbollah akarusha drone imeingia Israel 30 km ndani kabisa imepiga picha ya maeneo yote ya kimkakati, base za jeshi, sehemu za silaha n.k, imekuwa aibu na hakuna mtu kaamini hadi wengine wakasema ni photoshop.
USA ameionya Israel isijaribu kuingia vitani na Hezbollah kwani iron dome haitowasaidia, US imewaambia mifumo ya ulinzi itazidiwa.