Mwanakwaya auawa kikatili kwa kucharangwa na vitu vyenye ncha kali

Mwanakwaya auawa kikatili kwa kucharangwa na vitu vyenye ncha kali

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
1741676693752.png
Mwanakwaya wa Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, Manispaa ya Shinyanga, Agatha Nyahuma (32), mkazi wa Bugayambelele, Kata ya Kizumbi, amefariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana waliomtaka kwa vitu vyenye ncha kali katika maeneo ya mabega, mgongoni na mkono wa kulia.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kennedy Mgani, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 12:30 asubuhi katika Mtaa wa SIDO, Buhangija.

Kwa mujibu wa Kamanda Mgani, marehemu alikuwa akitoka nyumbani asubuhi akielekea kwenye Misa ya Asubuhi katika Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, lakini alikutana na watu wasiojulikana waliomshambulia kwa visu na vitu vyenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.

"Baada ya kushambuliwa, alianguka chini na wasamaria wema walimkimbiza katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo, alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi," alisema Mgani.

Chanzo: Nipashe
 
Mambo hayaeleweki hata nini: Jana nimerudi salama na mchepuko mida ya saa 9 usiku, huyu binti kauliwa anaenda kanisani.
 
View attachment 3266339Mwanakwaya wa Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, Manispaa ya Shinyanga, Agatha Nyahuma (32), mkazi wa Bugayambelele, Kata ya Kizumbi, amefariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana waliomtaka kwa vitu vyenye ncha kali katika maeneo ya mabega, mgongoni na mkono wa kulia.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kennedy Mgani, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 12:30 asubuhi katika Mtaa wa SIDO, Buhangija.

Kwa mujibu wa Kamanda Mgani, marehemu alikuwa akitoka nyumbani asubuhi akielekea kwenye Misa ya Asubuhi katika Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, lakini alikutana na watu wasiojulikana waliomshambulia kwa visu na vitu vyenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.

"Baada ya kushambuliwa, alianguka chini na wasamaria wema walimkimbiza katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo, alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi," alisema Mgani.

Chanzo: Nipashe
Kwa mujibu wa Kamanda Mgani, marehemu alikuwa akitoka nyumbani asubuhi akielekea kwenye Misa ya Asubuhi katika Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, lakini alikutana na watu wasiojulikana waliomshambulia kwa visu na vitu vyenye ncha kali sehem😭😭😭
 
Back
Top Bottom