The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kennedy Mgani, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 12:30 asubuhi katika Mtaa wa SIDO, Buhangija.
Kwa mujibu wa Kamanda Mgani, marehemu alikuwa akitoka nyumbani asubuhi akielekea kwenye Misa ya Asubuhi katika Kanisa Katoliki Parokia ya Buhangija, lakini alikutana na watu wasiojulikana waliomshambulia kwa visu na vitu vyenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.
"Baada ya kushambuliwa, alianguka chini na wasamaria wema walimkimbiza katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo, alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi," alisema Mgani.
Chanzo: Nipashe