Mwanamitindo maarufu Naomi Campbell atangazwa balozi wa 'Magical Kenya International'

Mwanamitindo maarufu Naomi Campbell atangazwa balozi wa 'Magical Kenya International'

Ikaria

Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
93
Reaction score
238
Mwanamitindo bingwa duniani Naomi Campbell sasa ndiye balozi wa ‘Magical Kenya International’, Wizara ya Utalii imethibitisha.

Makubaliano ya kuwa balozi yamefanikishwa na Mhe. Waziri wa Utalii Najib Balala leo jijini Mombasa.

Kenya inatazamia kujinadi kama sehemu na nchi bora zaidi ya kutalii katika bara la Africa. Ikumbukwe mataifa mengi duniani sasa hivi yapo mbioni kuendeleza uchumi ikizingatiwa kuwa mwaka wa 2020, shughuli za Utalii zilitatizika know kutokana na janga la virusi vya Corona.

Akihutubia wanahabari, Mhe Waziri Balala amesema ni bahati kubwa kwamba Campbell ameridhia kuwa balozi wa ‘Magical Kenya International’ hususan katika katika kipindi ambapo nchi zinajizatiti kufufua uchumi.

“Tunashukuru Sana kwa bahati hii kubwa ya kumnasa Naomi. Naamini atatangaza uzuri wa taifa letu” amesema Waziri Balala.

Kwa upande wake Naomi Campbell amesema kwake ni heshima kubwa pia kupata nafasi ya kutangaza Kenya.

“Kenya bila shaka ni sehemu pazuri. Sote tunafahamu hilo. Ni wakati mwafaka sasa kuwakumbusha watu kote duniani kuwa wakitaka kutalii wazingatie kutalii Kenya” amesema Campbell.
  • 20210112_115148-819x1024.jpg
 
Mambo ya kuchukua vizee ili basi kuiga Tanzania ambayo imetoa ubalozi wa heshima kwa celebrities!
[emoji1][emoji1][emoji1] Hivi Tz mna brand ipi au packaging ya kueleweka ya kufanya promotion ya utalii kimataifa ili muigwe? 'Equivalent' ya Magical Kenya nchini Tz ni nini, au ndio ile kauli yenu ya ubabaishaji ya hapa kazi tu. 😀 I can feel your pain, yes it is,
web9-01-e1505228537361.png
.
 
Kizee cha kale kinataka kujifananisha na pisi kali
 
[emoji1][emoji1][emoji1] Hivi Tz mna brand ipi au packaging ya kueleweka ya kufanya promotion ya utalii kimataifa ili muigwe? 'Equivalent' ya Magical Kenya nchini Tz ni nini, au ndio ile kauli yenu ya ubabaishaji ya hapa kazi tu. 😀 I can feel your pain, yes it is,
web9-01-e1505228537361.png
.
Tanzania Unforgettable...
 
Huyu mwanamama huwa ananikosha sana. Nawaza sijui ni lini atashuka ndani ya Dsm sema tu Basata ndio kikwazo, sio kwa picha zake zile ninazoziona mitandaoni.
 
Back
Top Bottom