Kwenye medicine huwa tunasema 'never say never'.....na huwa tunatumia zaidi neno 'very unlikely'! kaitak situation yako hii, tarehe 24 (aliyoanza bleeding) mpaka tarehe 30 (lilipofanyika tendo la uumbaji) ni jumla ya siku 7. It is very unlikely...extremely unlikely kupata mimba!
Kwa kawaida wanawake wengi huwa wanatoa yai 'ovulation' siku ya 14 au 15 tangu kuanza bleeding yaani kati kati ya mzunguko ambao kwa kawaida ni siku 28 (wengine huwa na mzunguko mfupi wa siku 26 au 25 ambapo kati kati itakuwa ni siku ya 12 au 13). Mbegu za mwanaume zinaweza kuishi mpaka siku 3, kwa hiyo ukitoa 3 hapo unakuta siku za mwanzo sa kuweza kupata mimba ni kuanzia siku ya 9 kwa mzunguko mfupi au siku ya 11 kwa mzunguko wa kawaida!
Kwa hiyo it is very unlikely mwanamke kupata mimba kama tendo limefanyika siku ya 7....lakini kama una uhakika na tarehe ulizotoa hapo juu!