Pre GE2025 Mwanamke anahaki ya kuongoza taifa hili. Watu waelewe nchi yetu haiongozwi na Dini wala Mila na desturi bali Katiba ya Nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama ni utashi wako upo Sahihi kabisa lakini kiuhalisia unapofika level za kitaifa utashi wako hauna tija.

Kipi kinakufanya ufikiri Mwanamke hatakiwi KUONGOZA isipokuwa Mwanaume.
Nitajie mambo matatu makuu kutetea upande wako
Hata wewe kwa utashi wako ni sahihi, lakini ukifika level za kitaifa, utashi wako hauna Tija vile vile.

Mwanamke ni kiumbe dhaifu, hilo moja linatosha kabisa.
 
Punguza unuaji kwenye mambo mtambuka!
 


..tatizo ni uwezo mdogo alionao Ssh.

..she does not have the intellect to lead a country as big, and strategically important as Tanzania.
 
TUMIENI AKILI KAMA MNAZO ...KUKUBALI KONGOZWA NA WANAWAKE NI UANITHI WA AKILI KWA SABABU WANAWAKE HAWANA AKILI YOYOTE YA MAANA...
 
Ndio maana nikasema tusipangiane. Una mtazamo wako ninao mtazamo wangu.

Sheria tunazieshimu lakini haimaniishi sheria zote tunakubaliana nazo mfano wewe kwenye andiko lako umesema haukubaliani na nafasi za vitu maalumu kwa sababu ni utaratibu ambao unamu-underestimate mwanamke

Lakini ni utaratibu ambao unatambulika kisheria kwaiyo ni lazima uuheshimu. Nsicho nilichokisema mimi mtazamo wangu binafsi ni kwamba mwanamke sio kiongozi lakini sheria za nchi zina mpa mwanamke haki ya kuwa kiongozi. Kwaiyo naheshimu sheria iyo ingawa sikubaliani nayo.
 
Kwahiyo umeamua kumpinga mama! Mama amekuwa akiyaambia mataifa makubwa kuwa kila nchi inaongozwa na mila, desturi na tamaduni zake, wewe unampinga.
 
Kakae uandike tena! Una hoja lakini namna ya uwasilishaji wako haijakaa kwa namna ulivyotaka ujumbe ufike! Tafuta angle na muktadha sahihi. Kuna namna umeshindwa kuwianisha hoja na msingi wa kuweka hitimisho!
Uongozi+ Mila na Desturi+ Mwanamke+ Haki ya kuongoza+ kuzikwa kwa Mila na Desturi. Yoyote hayo kwa uhusiano pia wa aliyetoa mada hiyo!
1. Ukweli ni kwamba Tanzania Bado itabakia ni Taifa Moja lenye makabila zaidi ya 132, Kila kabila kuwa na Mila na Desturi zake ambazo zinapaswa kuheshimiwa na Kila kabila katika hayo 132. Kama taifa hatuna Mila Moja au Desturi inayootuunganisha. Ila ndani yake Kuna watu wenye Mila na Desturi ambazo zinakataza taratibu au Desturi za watu wengine katika kabila zao.

2. Kwakua Mila na Desturi ni sehemu ya utamaduni. Kuna mambo ambayo katika utamaduni wa Mtanzania ambayo yanakubalika katika kabila zote kwa sababu ya kukubali kama taifa kwamba tuna haja ya kuziweka kando Mila na Desturi zetu na kuziacha katika msingi wa kabila na jamii zetu na linapokuja swala la Mama Tanzania hazikubaliki na hazitatumika. Hapa tunakubaliana kwamba hatujaziua au kuziacha miala na Desturi za makabila yetu Ila tumekubaliana kuwa na mipaka katika matumizi yake.

2. Kuna baadhi ya jamii au makabila ambayo, Mwanamke hawezi kushika mamlaka ya kiuongozi na kuwa mtawala. Jamii hizo tangu kabla ya ukoloni na baada ya ukoloni hazionekani kumsimika mwanamke kuwa kiongozi wao. Lakini zinalazimika kukubaliana na mfumo wa kikoloni uliowekwa kwao kwamba Mwanamke anaweza kuwa kiongozi kwa sababu sio jinsi inaongoza Bali ni misingi ya taratibu zilizowekwa kumpata kiongozi ambazo tunaziita katiba.

3. Kwa Desturi ya waislamu (dini ni sehemu ya Desturi) na ni sehemu ya utaratibu wa maisha ya watu ya Kila siku. Katika dini hii mwanamke hapaswi kushika mamlaka ya uongozi kwani amejengwa kuongozwa na sio kuongoza. Na kwakua Tanzania katika mambo ya secularism, tumekubaliana kwamba dini zibakie na watu wanaozifuata, Ila kama taifa hatuwezi kuweka dini kama utambulisho wetu. Kwa sababu Mila na Desturi ni sehemu ya utambulisho wa taifa. Tofauti na mataifa kama Iran na Afghan! Kwahiyo hatuwezi kuwanyima Haki ya kuongea wale wanaoamini kwamba kuongozwa na mwanamke kwao sio sahihi.

3. Hoja yangu ya pili hapo juu inajengwa katika msingi wa katiba yetu inayotoa uhuru wa maoni lakini kukubaliana juu ya multicultural existence of the Tanzania society.

4. Kimsingi hoja Yako ingekua na nguvu kama ingetolewa na vyama vya siasa vinavyolenga kutwaa madaraka ya nchi. Lakini kwakua umeweka katika Hali fiche, kauli hii imetolewa na kiongozi wa waislamu. Kwahiyo katika mfumo wa uendeshaji wa nchi yetu Haina mashiko na haiwezi kukubalika. Hii ni kutokana na ukweli kwamba tumekubaliana jinsi sio kigezo Cha uongozi.

5. Hoja ya viti maalumu, ni kweli kwamba kama wanawake wanataka hamsini kwa hamsini ambayo haiwezekani katika utekelezaji wake (practicability) wakubali kuachana na huu utamaduni. Utamaduni huu umeletwa na watu wa magharibi kama sehemu ya kuendelea kupika madaraka na nguvu ya asili ya Mwanaume katika uongozi kuanzia ngazi ya familia. Na hii imesababisha mtanziko mkubwa katika jamii yetu ya sasa.

6. Tumelazimishwa kufanya kinachoitwa uwezeshaji wa mwanamke na kuacha kumwandaa mwanaume kuishi na mwanamke aliyewezeshwa, matokeo yake tumezaliaha janga la Sheria na kanuni ambazo zinammaliza mwanaume na aspects zake zote. Ndio maana hata wewe umekuja hapa kumtetea mwanamke ambaye akipata nguvu iwe ya fedha au kiuchumi atakuinukia tu!

Let women be subjects of men for it is God's creation
 
Umejirudi mkuu 🤣post moja umewakandia "huwezi kuwaungisha" sahivi unaomba msamaha indirect kwa mbili mbili kwa mbili mbili imeisha unaambiwa 2+2 na 2x2=4 1+1=2 lakini 1x1=1
Nawafikishia ujumbe wanaolalamika kwanini Tanzania rais wake ni mwanamke, wakati ule JPM anamchagua kuwa mgombea mwenzake walitakiwa wajue madhara na ukubwa wa maamuzi yale.

Leo wanapolialia humu jukwaani haiwasaidii chochote.
 
Nchi yetu haina dini ila watu wake wanazo dini zao - Mwalimu Julius Nyerere March 1995.
 
Kwahiyo unabishana na aliyoyaamrisha ALLAH (S.A.W) ? Wewe kama nani?

Mwanamke hajaumbwa kumuongoza Mwanaume, hivyo ndivyo Quran aliyoshishiwa Mtume Muhammad (Rehma zimfikie) itakavyo
Ndio Rais wetu huyo na ikiwezekana mpaka 2030, nyinyi mnaotanguliza masuala ya ALLAH siburini atakapoondoka madarakani ndio muje tena na hoja zenu za kidini.
 
Asili ya Mungu haikwepeki na sio nimeunganisha na siasa na dini ndio ukweli. Biden aliamua kumpa usaidizi Kamala na sasa Biden huyo huyo yupo hoi kiafya.

JPM aliamua kumpa usaidizi Samia na kwa bahati mbaya akawa na betri moyoni mwake, akashindwa kufika 2025, kama sio asili ya Mungu tunaweza kuuitaje urais wa Samia?.

Kwa bahati tu Kamala anaweza kuwa Rais wa USA sawa na bahati ilivyomuangukia SSH hapa Tanzania.

Wa kugombea na Samia wanazidi kupungua kwa namna anavyofanya kazi ya maana huko mikoani kwa kipindi cha miaka mitatu aliyochukua kijiti kutoka kwa RIP Magufuli.
 
Tangu uumbaji mwanamke hakuumbwa kama kiongozi, asili inapinga. ASILI ina nguvu kuliko haki. Ikiwa haki ni sawa, Kwa nini tusigawane Koo Kwa watoto wanaozaliwa?!
 
Kwanza tukurebishe kidogo..

1. Mila na desturi za makabila hayajafutwa na kitu hiki unachosema "baada ya kuundwa Tanzania..."

2. Makabila na mila za makabila haya ndani ya Tanganyika bado zipo na zitaendelea kuwepo....

3. Kuhusu mwanamke kuwa kiongozi ndani ya familia kubwa ya Tanganyika ktk ngazi ya u - Rais. Hili ni baya na lilifanyika kosa tangu mwanzo kiasi cha huyu aliyepo kupata nafasi hiyo. Kosa hili linapaswa kurekebishwa mara moja...!!

4. Tunajua umeandika haya ktk muktadha wa kujaribu kuleta utetezi wa nusu uchawa kwa Samia Suluhu Hassan.

Huyu licha ya kuwa mwanamke, huyu si Mtanganganyika. Ni ujinga na ni kutojitambua kwa Watanganyika kuruhusu mtu wa Taifa jingine tena mwanamke kutawala ktk taifa jingine...

Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari. Sisi ni Watanganyika. Hatutaki tena huu upuuzi huu kuendelea. Huko kwao Zanzibar hawawezi kuruhusu mwanamke kuwa kiongozi mkuu wa Taifa lao la Zanzibar...

Kama hujui, waulize watakwambia ni kwanini...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…