Mwanamke: zijue siri za mwanaume mfujaji katika ndoa…………………..

Mwanamke: zijue siri za mwanaume mfujaji katika ndoa…………………..

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
Wanaume wengi wafujaji au watesaji wa wake zao hujitahidi sana kumtenganisha mke na ndugu zake. Wanapofanikiwa kuwatenganisha, wanaume hao huwa wamejitengenezea wigo mpana zaidi wa kuwadhibiti wake zao. Kama mjuavyo lengo la ufujaji kwenye ndoa ni kudhibiti. Mwanaume anapomkosanisha mkewe na ndugu zake anakuwa na uhakika kwamba, mke huyo hana nafasi ya kuondoka kwake kwa sababu hana pa kwenda.

Lakini kwa kumgombanisha na ndugu zake, mwanaume anapata nguvu ya kumfanya mkewe ahisi kushtakiwa na dhamirana kuanza kuhisi kwamba, ni yeye mwenye matatizo na siyo mumewe, kwani hata ndugu ameshindana nao. Mume pia humkumbushia kwamba ameshindwa hata kuelewana na ndugu zake, yeye ataweza wapi. ‘Ndugu zako tu wamekushindwa , mimi nitaweza wapi?' anaweza kusema hivyo.

Kwa mwanaume mfujaji, kumgombanisha mkewe na ndugu zake ni jambo la kawaida sana na hufanywa kwa sura mbalimbali. Kwa mfano, mume anaweza kuwaambia ndugu wa mke kwamba mkewe amebadilika sana kwani amekuwa ni mchoyo na hapendi wageni. Na ili kujenga mazingira ya kuthibitisha hilo anaweza kumkataza mkewe kuwahudumia ndugu zake kwa kinywaji chochote wanapokuja nyumbani kuwatembelea. Kwa hiyo ndugu wanapofika hapo nyumbani wakati mume akiwepo, mume huyo kusubiri hadi kiasi cha nusu saa halafu humwambia mkewe, ‘vipi, wageni hawanywi hata soda?' hapo mkewe atawaletea wageni soda, na wageni hao watakuwa wamethibitisha yale maneno waliyoambiwa na mume wake.

Njia nyingine ni ile ya mume kusaidia sana ndugu wa mke lakini wakati huo huo akitia sumu mbaya dhidi ya mkewe. Anaweza kumpa fedha shemeji au hata baba au mama mkwe na kusema, 'lakini mwenzangu asijue kwa sababu kidogo mambo ya kusaidia hayapendi sana, lakini msimwambie.'

Nyingine ni ile ya kuwaambia ndugu mambo mabaya dhidi yao ambayo mkewe alimwambia katika mazungumzo ya kutaka aijue familia yake vizuri. ‘Sasa hayo mambo ya kifamilia mimi ningeyajua vipi?' mwanaume atahoji, na itakuwa ni kweli.

Kuna njia ya kumwambia mke kuhusu ubaya wa ndugu zake. Anaweza kusema kwamba, dada wa mkewe amemwambia kwamba, zamani huyo mkewe alikuwa muhuni . ‘huna haja ya kumuuliza, kaa naye mbali tu, mwepuke huna haja ya kumpa msaada mtu kama huyo. Amenikera sana.' Anaweza kumuonya mkewe. Kwa sababu mke anamwamini mume na hataki mume huyo akasutana na dada yake, hunyamaza tu. Lakini hujenga chuki dhidi ya dada yake.

Mwanamke anashauriwa kuwa mwangalifu sana na mwanaume mfujaji, hasa linapokuja suala la kumgombanisha na ndugu zake. Kama mume akimwambia mkewe mambo mabaya kuhusu ndugu wa mke huyo, inabidi uchunguzi ufanyike. Mwanamke hapaswi kuamini kila kitu anachoambiwa na mumewe kuhusu ndugu zake……………………………
 
1. Ufujaji unatokana na mawenge.....umeoa lakini bado hujiamini.
2. Mwanamke hadhibitiwi bana,wao hujidhibiti wenyewe wakiamua, hao wafujaji sana sana ni kama wanacheza makida.
 
Mfujaji wa pesa au mali?
Au mfujaji wa duduz kupeleka kwenye mashimo mengine?
 
Kesho naomba uje na ya mwanamke mfujaji.

ONYO: Kushindwa kufanya hivi kutapelekea maandamano ya mimi na wanaume wengine wafujaji kupinga upendeleo uliouonesha wa kutusema sisi bila kuwasema wake zetu. Maandamano yataanzia kila kona ya mji mpk kwenye server za JF.
 
Kesho naomba uje na ya mwanamke mfujaji.

ONYO: Kushindwa kufanya hivi kutapelekea maandamano ya mimi na wanaume wengine wafujaji kupinga upendeleo uliouonesha wa kutusema sisi bila kuwasema wake zetu. Maandamano yataanzia kila kona ya mji mpk kwenye server za JF.
Hiyo kwenye Bold, ni kwamba unaweza kuigeuza hiyo maneno ya wanaume wafujaji vise versa......................
 
Mwanamke hapaswi kuamini kila kitu anachoambiwa na mumewe kuhusu ndugu zake……………………………
Na Mwanaume hapaswi pia kuamini kila kitu anachoambiwa na mkewe kuhusu ndugu zake.........................!

Mkuu salama?
Naona jana uliwanadi binti zako kwa Tajiri Mweusi! Vipi haukubahatika hata mmoja, waondoe kiwingu hapo home?
 
Kesho naomba uje na ya mwanamke mfujaji.

ONYO: Kushindwa kufanya hivi kutapelekea maandamano ya mimi na wanaume wengine wafujaji kupinga upendeleo uliouonesha wa kutusema sisi bila kuwasema wake zetu. Maandamano yataanzia kila kona ya mji mpk kwenye server za JF.

Hata mimi ninasubiri hii. Kwa kuheshimu huu uzi mzuri bila ya kuuchakachua, tunasubiri huo uzi wa she mfujaji nikitumai kuwa mbinu zao zitakuwa tafauti.
 
Mkuu salama?
Naona jana uliwanadi binti zako kwa Tajiri Mweusi! Vipi haukubahatika hata mmoja, waondoe kiwingu hapo home?
Dili lilikataa mkuu, yaani angekuwa ni msaada kwangu kuniongezea mtaji kama angekubali ule mpango wa IVF..................LOL
 
Back
Top Bottom