Mwanamuziki Rosa Ree Aibeba Tena Tanzania Kwa Hii Video yake Mpya...Itazame Hapa

Mwanamuziki Rosa Ree Aibeba Tena Tanzania Kwa Hii Video yake Mpya...Itazame Hapa

Udakuz

Member
Joined
Feb 4, 2013
Posts
85
Reaction score
51
Rapper wa kike kutoka Tanzania Aitwaye Rosa Ree usiku wa Jana ameendelea kuonyesha kuwa yeye ndio mkali wa Kurap kwa upande wa wadada Afrika baada ya kuachia Video kali ya wimbo wake unaitwa Dow na TV Kama Trace na MTV na Zingine Kuucheza...

Itazame Hapa Chini video Hiyo:

 
Beat limembeba. Kwenye ku rap na utunzi bado kuna vitu anamiss kuufanya muziki wake unoge kama Hiphop.
Alafu bado hajajua kucheza na camera, swaga za kubinua midomo, ili uonekane ndio mgumu au unafanya muziki wa kigumu zilishapitwa na wakati.
 
Beat limembeba. Kwenye ku rap na utunzi bado kuna vitu anamiss kuufanya muziki wake unoge kama Hiphop.
Alafu bado hajajua kucheza na camera, swaga za kubinua midomo, ili uonekane ndio mgumu zilishapitwa na wakati.
Sure kuna sometimes uandishi wake unazingua...
Lakini up in the air ilikuwa dope beat mpaka michano
 
Aungane na mm tu tukalime,Anaupenda mziki lkn Mziki haumpendi.
 
Beat limembeba. Kwenye ku rap na utunzi bado kuna vitu anamiss kuufanya muziki wake unoge kama Hiphop.
Alafu bado hajajua kucheza na camera, swaga za kubinua midomo, ili uonekane ndio mgumu zilishapitwa na wakati.
Wivu!
 
Beat limembeba. Kwenye ku rap na utunzi bado kuna vitu anamiss kuufanya muziki wake unoge kama Hiphop.
Alafu bado hajajua kucheza na camera, swaga za kubinua midomo, ili uonekane ndio mgumu zilishapitwa na wakati.
Wimbo wako uliowahi kuuimba ni download please, kukosoa mwaweza ila kutengeneza ndo zero.
 
Anajitahidi sana ila sifa anazopewa bado hajafikia, akazanie Mziki wake uzidi kupenya kwenye Soko la Bongo na Afrika Mashariki kabla ya kuitwa Rapa bora wa Kike Afrika!
 
Beat limembeba. Kwenye ku rap na utunzi bado kuna vitu anamiss kuufanya muziki wake unoge kama Hiphop.
Alafu bado hajajua kucheza na camera, swaga za kubinua midomo, ili uonekane ndio mgumu zilishapitwa na wakati.
Nadhani ushauri wako ataupokea. Unashauri afanye nini ili afike kwenye hivyo vinamiss kwake??

Binafsi, nakubaliana na mchangiaji mmoja hapo juu, huyu binti angekuwa mbele ingekuwa habari ingine.
 
Nadhani ushauri wako ataupokea. Unashauri afanye nini ili afike kwenye hivyo vinamiss kwake??

Binafsi, nakubaliana na mchangiaji mmoja hapo juu, huyu binti angekuwa mbele ingekuwa habari ingine.
Sure angekuwa habari nyingine ila hata hapa akiamua anaweza kuwa habari nyingine pia. Mungu aliyefanya awe hapa anakusudio lake na nzuri zaidi ameweza kujua anakipaji gani.

Kuhusu nini afanye? Hili swali nitalijibu kwa ujumla. Aina ya muziki anaofanya kama sitakuwa nje ya mstari na mawazo yake ni muziki aina ya Hiphop
Mara nyingi aina ya Muziki huu ili uwe bora zaidi unahitaji utunzi wa "mistari inayoishi". Na hapa ndipo utakapo acha legacy yako katika jamii inayokuzunguka.

Mpaka leo tunaona, mfano Mtu kama 2pac bado anaongelewa kwenye fikra za watu na baadhi ya tungo zake zinafanyiwa remix mpaka kesho, si kwamba alikuwa "bora sana" kuliko wengeni katika kurap, ni vile tu aliweza kuandika "mistari inayoishi"

Hapa Tanzania kuna watu walifanya Muziki na wakapendwa sana na kulipwa pesa nyingi, vile waliweza kuandika "Kuku kapanda baiskeli", ila leo huo muziki ukichezwa tena sijui kama utaweza kukusanya kijiji kama hapo mwanzo.

Tujiulize tena ni kwanini Muziki wa Msondo ukichezwa leo bado unavuta hisia kwa msikilizaji japo unabezwa ni Zilipendwa?

Natumai nitakuwa nimeeleweka kwa kiasi fulani nilichokuwa namaanisha, katika kukosoa kwangu.
 
Huu ni wimbo na video ya kwanza ya Rosa Ree toka alipotoka kwenye label ya The Industry ya Nahrel.
Mi naona amejitahidi japo haijafikia zile nyimbo zilizopita.

Kuna mdau kasema hawezi kucheza na kamera. Labda hajaiangalia hiyo video vizuri. Amecheza kamera vizuri sana.

Kuhusu Flow na mistari. Huyu dada sio mtunzi mzuri wa Kiswahili. Hii inaweza changia.
 
Back
Top Bottom