Mwananchi inapumulia mashine

Mwananchi inapumulia mashine

Joined
Jun 10, 2020
Posts
11
Reaction score
15
Kampuni ya Mwananchi inayochapisha Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikiaminika kwa kuhabarisha kwa uwazi iko kwenye msukosuko.

Pamoja na kushuka kwa biashara ya habari nchini, hali ya hewa so nzuri Mwananchi. Wafanyakazi wa idara ya matangazo wanasema kwamba kipindi cha mwaka mmoja, wamepunguza mamia ya wafanyakazi kwa takribani robo tatu, huku wakifikia hatua ya kutokulipa mishahara kwa wakati.

Hata ukiangalia habari zao zimekuwa ni kusifia, kujipendekeza ili waonewe huruma na serikali. Wafanyakazi wanasema tatizo ni uongozi wa Watanzania, kwani wakubwa wako kimaslahi zaidi na wanaishia kujigawia tenda za kampuni wapige pesa huku Waandishi wa Habari wakisota kwa mishahara kiduchu na wengine wakifanya kazi miaka zaidi ya kumi bila kupewa mkataba.

Waandishi wazuri wameondoka; hasa vijana kutokana na ubinafsi wa wahariri wao, ambao nao wameshajipandishia mishahara mpaka wafanyakazi wanaona hasira.

Wafanyakazi wanasema bora CEO Mkenya ama Tido Mhando waliisogeza kampuni kwenye mafanikio makubwa, lakini huu uongozi mpya uko busy na mambo yao binafsi na kampuni inadorora.

Hii inaonyesha kwamba, bila kujikomba, basi miaka mitatu ijayo hawatakuwa tena kwenye biashara.
 
Kiuhalisia sector binafsi kwa ujumla inahali tete sana.
hata hivyo print media imekuwa kwenye hali mbaya kutokana na mabadiliko ya teknolojia ya habari na mawasiliano watu wanapata habari kwemye vyanzo vingine vya habari na ili hizi zisimame labda kama itabidi wawe na makala za kiuchambuzi zenye kuandikia makala mbalimbali kwa weredi wa hali ya juu kwani kuripoti taarifa pekee hakutoshi kwa sasa
 
Uongo, Marekani na Ulaya kwenye top ya teknolojia ya mawasiliano ya mtandao magazeti bado yanauzwa sana
hata hivyo print media imekuwa kwenye hali mbaya kutokana na mabadiliko ya teknolojia ya habari na mawasiliano watu wanapata habari kwemye vyanzo vingine vya habari na ili hizi zisimame labda kama itabidi wawe na makala za kiuchambuzi zenye kuandikia makala mbalimbali kwa weredi wa hali ya juu kwani kuripoti taarifa pekee hakutoshi kwa sasa
 
Uongo,marekani na Ulaya kwenye top ya teknolojia ya mawasiliano ya mtandao magazeti bado yanauzwa sana
Fanya uchunguzi na bahati mimi ni mdau wa print media, mfano magazeti mengi licha ya kutegemea mauzo ambayo yameshuka hutegemea matangazo na kwa kiasi kikubwa watangazji wengi wanatumia platform nyingine kuliko magazeti kwa sasa mtu ni bora apeleke tangazo kwa millard ayo kuliko kuweka gazetini.

Na ndiyo maana hata redio kubwa kama BBC, DW nk ziaanza kutumia mitandao ili kuendana na hali ya mabadiliko sasa na bahati kuna siku waliendesha mjadala kama huu kwenye radio mojawapo na kukiri kwa changamoto hiyo ingawa bado magazeti na radio ndo vyanzo vinavyoaminka zaidi.

Mauzo yanapungua hata kwenye magazeti ya udaku cha pili hulka ya watanzania ya kujisomea huwezi ilinganisha na ya hao ulio wataja kwani hata mazoea ya kusoma bado yanachangia wao kuendelea kusoma kwa vyovyote vile online subscription services ndiyo mwelekeo mpya kwa kutumia digital mediums na devices kama jamiiforums ,Facebook, YouTube, Twitter, iPads, mobile phones NK
 
hata hivyo print media imekuwa kwenye hali mbaya kutokana na mabadiliko ya teknolojia ya habari na mawasiliano watu wanapata habari kwemye vyanzo vingine vya habari na ili hizi zisimame labda kama itabidi wawe na makala za kiuchambuzi zenye kuandikia makala mbalimbali kwa weredi wa hali ya juu kwani kuripoti taarifa pekee hakutoshi kwa sasa
Print media bado ipo na itendelea kuwepo hata dunia ya kwanza digitization inaleta changamoto sana
 
Fanya uchunguzi na bahati mimi ni mdau wa print media, mfano magazeti mengi licha ya kutegemea mauzo ambayo yameshuka hutegemea matangazo na kwa kiasi kikubwa watangazji wengi wanatumia platform nyingine kuliko magazeti kwa sasa mtu ni bora apeleke tangazo kwa millard ayo...
Umemaliza Kila kitu mkulu hasa hapo mwisho
 
Utawala mbovu huu sijapata kuona alafu kuna wajinga huko wanapongeza hizi juhudi.
 
Print media bado ipo na itendelea kuwepo hata dunia ya kwanza digitization inaleta changamoto sana
Ina survive ila kwa mbinde Sana. Mfano kupitia hapa JF tunapata habari za moto moto tu, WhatsApp tunasambaziana habari za moto moto tu, Nani atasubiri mpaka kesho aje anunue Gazeti lenye habari za leo?

Magazeti yatabaki kwa Matumizi machache tu
 
Sasa mkuu
Uongo,marekani na Ulaya kwenye top ya teknolojia ya mawasiliano ya mtandao magazeti bado yanauzwa sana
Unataka kutuambia Ulaya na Tanzania tuko sawa kwenye nyanja ya usomaji wa magazeti au vitabu mmh?
 
Back
Top Bottom