Mwanangu hawezi kuongea wala kutambaa

UWOGA=UMASKINI

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
2,399
Reaction score
1,014
Wadau wa hapa nisaidieni cha kufanya mwanangu ana mwaka na miezi saba lakini hawezi zungumza au kutembea na anatambaa na matako yaani anasota na nimemmpeleka kwenye mazoezi toka mwaka jana na kwa maombi sana.

Kama kuna mtaalama ana kitu kingine aniongezee ili huyu kijana wangu wa kiume afanye yale yampasayo kufanya na umri alionao.
 
pole sana mkuu mara nyingi watoto wanaotambaa kwa kusota wanachelewa sana kusimama hasa inawakuta watoto wa kiume. Endelea kumfanyisha mazoezi ya kutambaa ikiwezekana mnunulie kigari kile cha mbao ili atamani kukishika na itapelekea atamani kukisimamia, usichoke mkuu hata wa kwangu alikuwa hivyo
 
Mkuu pole sana!!,mimi mwenyewe mwanangu alitambali matako na alichukua muda mrefu,amekuja kutembea akiwa na mwaka mmoja na miezi sita,Yaani cha msingi mtafutie kibaiskeli cha miti au vipo Vigari fulani vya dukani ambavyo mtoto akikaa vinamlazimisha kutembea hatimaye unakuta ameshatembea,Usikate tamaa Mungu ni Mwema atatembea tu najua utasikia sana maneno ya watu lkn Wala usitishike mwenyewe yalinikuta hayo lkn nashukuru Mungu Dogo alitembea na leo hii anakimbia km swala.
 

nimemtengenezea hakitaki hata kukigusa je wewe ulifanyaje bro na wako alitembea au kuongea na umri gani
 
Pole sana mkuu..mimi kama mzazi pia ninasikia uchungu
kwa ulichokieleza hapo juu...cha kukushauri wewe
muendelezee mazoezi ya kutembea kama hana matatizo
ya kilema cha kutembea basi amini kuna siku atasimama
na kutembea tu...
kwani kuna hata watoto wengine waliisha chelewa kuongea
mpaka mzazi anadhani labda mtoto atakuja kuwa bubu ila
mwisho wa siku mtoto anakuja kubonga kama chiriku au watu wa dar....na kisha wanaanza
kubonga kwa sana tu.
 
nimemtengenezea hakitaki hata kukigusa je wewe ulifanyaje bro na wako alitembea au kuongea na umri gani

Atakitamani tu hata wa kwangu mwanzoni alikuwa anakiogopa sana, kwenye kuongea mara nyingi mtoto huanza kuita jina la mama au baba au sitaki maana ndio maneno anayoyasikia kila siku. Kama anaweza kuyatamka basi muache ataongea taratibu tu. Kama hawezi kutamka basi kamkate kile kidude kilichoko chini ya ulimi
 

kweli kaka coz ukiangalia wenzake wanakimbia kabisa na hata waliozaliwa mwaka huu wameanza dede then wangu mwaka na miezi 7 bado yupo yupo to pain
 
Pole sana jamani,ngoja wazazi wenza watakushauri vizuri tu, Mungu ni mwema atamsaidia
 

Pole sana.
Ni vyema mwanao ukampeleka kwa daktari bingwa wa watoto. Daktari atafanya majumuisho ya mwenendo wa mapokeo ya ukuaji wa mwanao(milestones).

Inawezekana kuna tabia nyingine pia zilichelewa lakini hukuweza kuzitambua.

Hivyo, daktari pia atamkagua mtoto kuona kama ana tatizo lolote.

Mwisho, utashauriwa kama mtoto ana tatizo lolote nyuma ya hili linaloonekana au ni kuchelewa tu.
Na ni nini ufanye ili kumsaidia.

Ahsante.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…