Mwanariadha wa kimataifa Gabriel Geay avunja rekodi ya taifa

Melubo Letema

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
416
Reaction score
414
GABRIEL GERALD GEAY AVUNJA REKODI YA TAIFA Huko Milano , Italy na kufuzu kushiriki mashindano ya Olimpiki (Japan) kwa kukimbia kwa Muda wa saa mbili dakika nne na sekunde hamsini na tano (2:04:55) na kushika nafasi ya Sita.

Hadi Sasa Tuna wanariadha watatu waliofuzu viwango vya olimpiki.
1. Alphonce Felix Simbu
2. Failuna Abdi Matanga
3. Gabriel Gerald Geay

Tunawasubiri Wengine
 
Pongezi kwao.

Riadha wawe serious tu watatutoa kimasomaso sio hawa akila "tielfuelfu"
 
Ndiyo, kama ilivyo pangwa itafanyika kuanzia tarehe 23 July hadi 8 August 2021.
Jana nilikuwa naangalia habari nikaona Wajapani wanafanya protest hawataki Olympic kwa kuhofia mfumuko wa Covid-19.

Kati ya asilimia 60- 80 ya Wajapani wanapinga Olympics kufanyika mwaka huu.

Wajapani 350,000 wamepiga saini azimio la kutaka michezo hii isifanyike mwaka huu.


Chama cha Madaktari wa Japani tqkribqni 6,000 kimetoa wito michezo hii isifanyike mwaka huu kwa kuhofia mlipuko wa Covid-19.


Wajapani wanakataa kuwa wenyeji wa wana Olympic.

 
Tutawasikiliza Maamuzi Yao, uzuri walio qualify wataruhusiwa kucheza, hapo itakapotangazwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…