Mwanasheria wa Yanga: Mchezaji Yusuph Kagoma alisaini mkataba wa miaka mitatu na Yanga

Mwanasheria wa Yanga: Mchezaji Yusuph Kagoma alisaini mkataba wa miaka mitatu na Yanga

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwanasheria wa Yanga, Simon Patrick, ametoa ufafanuzi juu ya umiliki wa mchezaji Yusuf Kagoma baada ya mazungumzo marefu na klabu ya Singida Fountain Gate. Patrick alisema, "Tulianzisha maongezi ya muda mrefu na Singida Fountain Gate kwa lengo la kununua rasmi Yusuf Kagoma."

Kwa mujibu wa Patrick, Singida ilitoa masharti ya kulipa shilingi milioni 30, na Yanga ilikubaliana kufanya malipo hayo kwa awamu mbili. Malipo ya kwanza yalifanyika tarehe 30 Aprili, na baada ya hapo, klabu ya Yanga ilipewa ruhusa ya kuzungumza na mchezaji kuhusu maslahi yake binafsi.
1726134957575.png
Baada ya makubaliano hayo, Yanga ilimtumia Kagoma tiketi ya ndege ili afike Dar es Salaam kwa ajili ya kusaini mkataba. Kagoma alifuatana na wakili wake, Bwana Léonard, na akaweka saini yake rasmi.
Mkataba wa makubaliano kati ya Mchezaji wa @simbasctanzania  @kagoma_21  na klabu @yangasc  ul...jpg
Kwa mujibu wa Patrick, "Tunaweza kusema Kagoma bado ni mchezaji wetu."
Mkataba wa makubaliano kati ya Mchezaji wa @simbasctanzania  @kagoma_21  na klabu @yangasc  ul...jpg

Snapinsta.app_459557903_18076646449538650_7941931185451300355_n_1080.jpg
Chanzo: Crown FM

Soma pia;
=> Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama
=> Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba
=> Ahmed Ally atoa kauli kuhusu sakata la Yusuph Kagoma na Yanga SC
 

Attachments

  • 1726135042004.png
    1726135042004.png
    2.9 MB · Views: 10
Mwanasheria wa Yanga, Simon Patrick, ametoa ufafanuzi juu ya umiliki wa mchezaji Yusuf Kagoma baada ya mazungumzo marefu na klabu ya Singida Fountain Gate. Patrick alisema, "Tulianzisha maongezi ya muda mrefu na Singida Fountain Gate kwa lengo la kununua rasmi Yusuf Kagoma."
Kwa mujibu wa Patrick, Singida ilitoa masharti ya kulipa shilingi milioni 30, na Yanga ilikubaliana kufanya malipo hayo kwa awamu mbili. Malipo ya kwanza yalifanyika tarehe 30 Aprili, na baada ya hapo, klabu ya Yanga ilipewa ruhusa ya kuzungumza na mchezaji kuhusu maslahi yake binafsi.
Baada ya makubaliano hayo, Yanga ilimtumia Kagoma tiketi ya ndege ili afike Dar es Salaam kwa ajili ya kusaini mkataba. Kagoma alifuatana na wakili wake, Bwana Léonard, na akaweka saini yake rasmi.

Kwa mujibu wa Patrick, "Tunaweza kusema Kagoma bado ni mchezaji wetu."

Chanzo: Crown FM

Soma pia;
=> Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama
=> Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba
=> Ahmed Ally atoa kauli kuhusu sakata la Yusuph Kagoma na Yanga SC
Mtuache kidogo tupo bize na albadir ya Tanga ambayo kuna watu watakua vichaa ndani ya prado.
 
Mwanasheria wa klabu ya Yanga Patrick Saimon ametoa ufafanuzi ishu ya Yusuph Kagoma na kusema mpaka sasa wamewalipa Singida Fountain Gate Fc shilingi milioni 60 zikiwa na mchanganuo kwa wachezaji wawili ambao ni Yusuph Kagoma milioni 30 pamoja na Fedha za Nickson Kimbabage milioni 30 ambazo zilikuwa ni deni"

"Mchezaji Yusuph Kagoma haruhusiwi kucheza timu yoyote kutokana na mkabata wake unasoma timu mbili, Hivyo mpaka sasa shauri letu lipo chini ya kamati ya sheria na hadhi ya wachezaji mpaka sasa hatujasikilizwa"

"Mpaka sasa tunaongea Yusuph Kagoma ni mchezaji halali wa Yanga Sc tulimsaini miaka mitatu na tukamtumia hadi tiketi ya ndege kutoka Kigoma nakuja Dar es salaam kuungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya msimu huu 2024 - 2025" - Patrick Saimon, Mwanasheria wa Yanga

Soma Pia: Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama


Hii sasa imeekaaje kama ushahidi wa mkataba upo simuoni Kagoma na Simba wakitoboa kwenye hili.
 
akina ubaya ubwela sasa wanapumulia ubwela maana ubaya tayari wanao...🤣
 
Mbona msemaji amesema mnacohitaji ni kuombwa msamaha tu na sio mchezaji, maana hawzi kupata namba hata ya kikosi cha tatu cha Yanga? Ilikuwaje mchezaji asiyewza kupata namba hadi timu C akapewa mkataba wa miaka mitatu yote hiyo?
Hujui kama wachezaji wana kazi za kufanya kama vile kubeba maji, koni za mazoezi n.k.
 
Huyu alikuwa na tabia za kitapeli na za kitamaa tokea Sekkndari.
 
Mwanasheria wa klabu ya Yanga Patrick Saimon ametoa ufafanuzi ishu ya Yusuph Kagoma na kusema mpaka sasa wamewalipa Singida Fountain Gate Fc shilingi milioni 60 zikiwa na mchanganuo kwa wachezaji wawili ambao ni Yusuph Kagoma milioni 30 pamoja na Fedha za Nickson Kimbabage milioni 30 ambazo zilikuwa ni deni"

"Mchezaji Yusuph Kagoma haruhusiwi kucheza timu yoyote kutokana na mkabata wake unasoma timu mbili, Hivyo mpaka sasa shauri letu lipo chini ya kamati ya sheria na hadhi ya wachezaji mpaka sasa hatujasikilizwa"

"Mpaka sasa tunaongea Yusuph Kagoma ni mchezaji halali wa Yanga Sc tulimsaini miaka mitatu na tukamtumia hadi tiketi ya ndege kutoka Kigoma nakuja Dar es salaam kuungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya msimu huu 2024 - 2025" - Patrick Saimon, Mwanasheria wa Yanga

Soma Pia: Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama

Hii sasa imeekaaje kama ushahidi wa mkataba upo simuoni Kagoma na Simba wakitoboa kwenye hili.
Mkataba wa awali huo ndugu......Kagoma alikubali kweli alisaini.......ila hawakumpatia pesa yake waliokubaliana. Na ukiangalia, Yanga iliwalipa pesa Singida na sio Kagoma. Kwanini Singida wasiwajibike kwa hili?
 
Kwa mujibu wa Patrick, Singida ilitoa masharti ya kulipa shilingi milioni 30, na Yanga ilikubaliana kufanya malipo hayo kwa awamu mbili. Malipo ya kwanza yalifanyika tarehe 30 Aprili, na baada ya hapo, klabu ya Yanga ilipewa ruhusa ya kuzungumza na mchezaji kuhusu maslahi yake binafsi.
Watu wasivyo serious, yaani milioni 30 nazo ni za kulipa kwa awamu mbili, na bado hazikumaliziwa!? 😀😀😀
 
Mchezaji ana leseni ya kuchezea Simba. Period. Na hao Singida walisema wameuza mchezaji Simba.
Za chini ya kapeti ni Yanga walichelewa kupeleka 30m ndani ya muda qaliokubaliana na Singida. Singida akafungua mazungumzo na Simba, wakakamilisha kila kitu
 
Mkataba wa awali huo ndugu......Kagoma alikubali kweli alisaini.......ila hawakumpatia pesa yake waliokubaliana. Na ukiangalia, Yanga iliwalipa pesa Singida na sio Kagoma. Kwanini Singida wasiwajibike kwa hili?
Kama Kagoma hakupewa chochote wakati alitumiwa ticket ya ndege ya go and return Kwenda Dar kusain mkataba ilo ni jambo jingine Tena la kushangaza kwa wenye akili timamu ila ukiwa mbumbumbu utaona ni kawaida.

Kwaiyo kama ni kweli hakulipwa chochote na Yanga, hoja iyo aitumie wakati wa usikilizwaji wa shauri lake pale Tff ili asikumbane na adhabu ya kufungiwa.
 
Hawa utopolo wametumwa na CCM kuzima sakata la mauaji ya kada wa Chadema
Kwanza unatakiwa uelewe pingamizi la Yanga liliwasilishwa lini pale Tff.
Kama Tff wangekuwa wanafuata utaratibu wa mpira wa miguu, hivi tunavyo andika Kagoma angeshakua amepewa adhabu muda mrefu ila kinacho fanyika ni yaleyale ya Lawi, Awesu Awesu, Valentino.

Kuna klabu ingekua imesha fungiwa kufanya usajili na faini juu.
 
Kama Kagoma hakupewa chochote wakati alitumiwa ticket ya ndege ya go and return Kwenda Dar kusain mkataba ilo ni jambo jingine Tena la kushangaza kwa wenye akili timamu ila ukiwa mbumbumbu utaona ni kawaida.

Kwaiyo kama ni kweli hakulipwa chochote na Yanga, hoja iyo aitumie wakati wa usikilizwaji wa shauri lake pale Tff ili asikumbane na adhabu ya kufungiwa.
Mdau...na wewe unaamini Kagoma alitumiwa tiketi ya ndege?.....Kitu fake kabisa hicho....huo ni utetezi wa kitoto sana. Yanga wenyewe wanakiri pesa wamewalipa Singida...mil.30. Yeye Kagoma wapi Yanga wamesema wamempatia pesa.
Halafu mkataba ni Transfer Agreement...kati ya Yanga (Seller) na Singada (Buyer) 🙂 🙂 🙂
 
Kwanza unatakiwa uelewe pingamizi la Yanga liliwasilishwa lini pale Tff.
Kama Tff wangekuwa wanafuata utaratibu wa mpira wa miguu, hivi tunavyo andika Kagoma angeshakua amepewa adhabu muda mrefu ila kinacho fanyika ni yaleyale ya Lawi, Awesu Awesu, Valentino.

Kuna klabu ingekua imesha fungiwa kufanya usajili na faini juu.
Hivi unamfahamu yanga walifungiwa na fifa kufanya usajili wa ndani, waendelee kuchonga tukawashitaki fifa.
 
Hivi unamfahamu yanga walifungiwa na fifa kufanya usajili wa ndani, waendelee kuchonga tukawashitaki fifa.
Ndugu mbumbumbu usajili ni TMS, kinacho lalamikiwa ni mchezani kufanya hadaa na kufanya signing ya timu mbili.
Swala la Yanga kufungiwa alihusiani na uhamisho wa mchezaji kutoka timu Moja kwenda nyingine.
Na wakati ayo yanafanyika Yanga alikua hajafungiwa kuingia mikataba kwakua ata dirisha la usajili lilikua Bado halijafunguliwa.

Na ata timu ikifungiwa ikisha lipa inaendelea kusajili.
Mikataba ya wachezaji inaingiwa muda wowote katika msimu mradi timu yake iwena taarifa.
 
Back
Top Bottom