Mwanasiasa nchini Tanzania ambaye kamwe hawezi kuhama chama chake ni Rais pekee

Mwanasiasa nchini Tanzania ambaye kamwe hawezi kuhama chama chake ni Rais pekee

Wafuasi wa Rais

Senior Member
Joined
May 31, 2023
Posts
151
Reaction score
147
Kila siku kumbuka kuwa mfuasi binafsi wa Rais. Rais hawezi kukusaliti. Rais ni nchi. Nchi ni Rais.

Urais ndio cheo cha juu cha kisiasa kote Duniani. Hakuna zaidi ya hapo. Chama cha Rais ni nchi yake. Hawezi kuisaliti.

Mwanasiasa yeyote anaweza kuisaliti itikadi ya chama chake cha siasa na kuhamia kwingine. Rais hawezi.

Mwanasiasa anaweza kuwasaliti wenzake muda wowote na kuwaacha solemba wasijue la kufanya. Rais hawezi.

Mwanasiasa anaweza kuwaachia wenzake maumivu makali sana ya moyo. Anaweza kuwakatisha wengine tamaa pa kubwa mno.

Achana na itikadi ya vyama vya kisiasa. Zitakuumiza moyo. Zitakuua kwa presha. Zitakukatisha tamaa ya maisha.

Daima kuwa mfuasi binafsi wa Rais bila kujali chama chake cha siasa. Maadam ni Rais kuwa nyuma yake bila kuangalia chama chake.

Msaidie Rais. Ukimsaidia Rais unasaidia nchi. Unawasaidia wananchi.

Rais kamwe hawezi kukusaliti. Kila siku eleweni hili. Anaweza kuwa na changamoto zake katika utendaji wake lakini hana dhamira ya kukusaliti na kukuacha moja kwa moja kama wanasiasa wengine wafanyavyo. Isitoshe majukumu ya uRais ni changamoto sana hasa ukizingatia aina ya wasaidizi wake.

Kimsingi kabisa Rais wala sio mwanasiasa basi tu ni kwa kuwa hakuna jina la kum frame aitweje nje ya ulingo wa kisiasa.

Nadhani Dunia inapaswa itafute namna gani Rais atambulike nje ya ulingo wa kisiasa maana Rais sio mwanasiasa.

Rais ni nchi. Nchi ni Rais. Rais ni wananchi.

Achana na itikadi za kisiasa bali kuwa mfuasi binafsi wa Rais aliyepo madarakani bila kujali chama chake cha siasa.

Wafuasi wa itikadi za kisiasa poleni sana na yanayowapata. Wengine tumeshtuka kitambo. Shtuka na wewe hujachelewa.

Karibu, ungana nasi. Tuendelee kumsaidia Rais azidi kukubalika zaidi mitaani.

====

Pia soma: Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM
 
Inasemekana rais wa nchi jirani anafanya kazi kwa maslahi ya Marekani, huku akiwasahau raia wake mwenyewe.

Hapo unasemaje?
 
..nadhani Levy Mwanawasa wa Zambia alikuwa Raisi na akahamu chama chake.

..Bingu wa Mutharika wa Malawi alikuwa Raisi na akaanzisha chama kipya.

..Naweza kuwa nimekosea, lakini kumbukumbu zangu zinanielekeza kwamba wako Maraisi waliohama vyama.
 
..nadhani Levy Mwanawasa wa Zambia alikuwa Raisi na akahamu chama chake.

..Bingu wa Mutharika wa Malawi alikuwa Raisi na akaanzisha chama kipya.

..Naweza kuwa nimekosea, lakini kumbukumbu zangu zinanielekeza kwamba wako Maraisi waliohama vyama.
Halafu kuna wale ambao wamo mulemule chamani hawatoki wala hawaendi popote, lakini kamwe hawatekelezi dira ya taifa kwa maslahi ya wananchi.

Hao tuwaweke kwenye kundi lipi eti?
 
Halafu kuna wale ambao wamo mulemule chamani hawatoki wala hawaendi popote, lakini kamwe hawatekelezi dira ya taifa kwa maslahi ya wananchi.

Hao tuwaweke kwenye kundi lipi eti?

..Na unaweza kuta ni Raisi.🤣🤣
 
🥹
Huyu huyu 🌝….
Ndio wa kumfuataaa….??
Watu walikuwa wafuasi wa chuma,,,,
 
🥹
Huyu huyu 🌝….
Ndio wa kumfuataaa….??
Watu walikuwa wafuasi wa chuma,,,,
 
Back
Top Bottom