Mwanasiasa yoyote kuwa na kesi ya kujibu sio kuwa na hatia. Tutambue na kuelewa 'legal issues'

Mwanasiasa yoyote kuwa na kesi ya kujibu sio kuwa na hatia. Tutambue na kuelewa 'legal issues'

Kamanda Asiyechoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2020
Posts
3,315
Reaction score
5,058
Watu wanachanganya mambo na kuwa waoga wa mambo sana.

Mwanasiasa yoyote yule akipata kushitakiwa, upande Mashitaka huwa wanaleta mashahidi na kama Hakimu au Jaji akiona huo ushahidi una mantiki basi huyo aliyeshitakiwa hutakiwa kukanusha huo ushahidi wa walioleta mashitaka.

Tuache sheria ifuate mkondo maana kuwa na kesi ya kujibu sio kutiwa hatiani bali ni kupewa nafasi ya kupinga ushahidi wa waliokushitaki ili uweze kuachiwa huru.
 
Kufikia kuwa na kesi ya kujibu, si inabidi pawe hapana doubt?

1. Wale mashahidi wewe binafsi hawajakupa doubt?
2. Kuwaacha mashahidi wengine, wasitoe ushahidi wao na huku walishasemwa kuwa watakuja kutoa ushahidi, wewe hakukupi doubt yoyote?
3. Unadhani, kwa vile kuna sehemu nyingine ya kupruvu beyond reasonable doubt basi huku kwa mwanzo kuburuzwe tu?
4. Hao mashahidi walioachwa, ina maana hawana kipya zaidi ya walichokwisha kukisema wenzao? AU wameona cross examination, kwa ushahidi walionao. WATATUPWA NJE VIBAYA?

NI UJINGA KUIPELEKA HII KESI MBELE ZAIDI YA ILIPOFIKIA... mawili
la kwanza, DPP aifute
au, la pili, Hakimu atoe amri kuwa watuhumiwa hawana kesi ya kujibu

Nje ya hapo, KUNA SAFU YA VIONGOZI INAENDA KUDHALILIKA
 
Back
Top Bottom