Mwanaume mmoja nchini Kenya akaa gerezani miaka 17 kimakosa

Mwanaume mmoja nchini Kenya akaa gerezani miaka 17 kimakosa

Loading failed

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2023
Posts
2,603
Reaction score
7,501
Daniel Wanyeki Gachoka mwenye umri wa miaka 59 kutoka Kenya ameachiwa huru baada ya kukaa gerezani kwa miaka 17 na baadae kugundulika kuwa alifungwa kimakosa

Wanyeki alikuwa akitumikia kifungo cha maisha jela katika Gereza la Kamiti Maximum Security kwa madai ya kuwanajisi binti zake wawili wa umri mdogo.

Hata hivyo, wiki jana, Mahakama Kuu ya Kiambu ilibatilisha hukumu yake, ikitoa uamuzi kwamba alikuwa amehukumiwa kimakosa.

Uamuzi wa mahakama ulifuatia mabadiliko makubwa ambapo binti za Wanyeki, ambao sasa ni watu wazima, walifichua kuwa walilazimishwa kumshtaki baba yao kwa uwongo mwaka wa 2007.

Wanawake hao wawili walitoa ushahidi mahakamani kwamba walikuwa wameshinikizwa na bibi yao kutoa ushahidi wa uongo dhidi ya Wanyeki ambapo mahakama ilikubaliana na ushahidi huo

Hata hivyo Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) imependekeza Wanyeki asubiri hadi Desemba 4 mwaka huu ili kesi hiyo ifanyiwe ukaguzi na kuona kama ni kweli anastahili kuachiwa huru

FB_IMG_1732952684040.jpg
 
Kwa nchi za wenzetu kesi kama hizi wahusika hupata fidia ya kiasi cha pesa, Bima ya afya, mafunzo ya kazi fulani,na huduma za kisaikolojia.
 
Kiasi fulani ukizaliwa mwanaume ulimwengu unakuwa katili kwako.
Hasa nyakati hizi za women empowerment. Wanasikilizwa sana bila kuzingatia wasemacho ni sahihi?
Shule nyingi za bweni zinazo toa elimu bora na huduma nzuri ni kwa ajili ya watoto wakike.
Mwanaume na mwanamke mkishindania nafasi ya chuo au ajira mkilingana au ukimzidi kidogo mwanamke anapewa yeye nafasi.
Hili aliizungumzia mahali fulani aliyekuwa Spika wa Binge Job Ndugai, and he was right 100%.
 
Kwa nchi za wenzetu kesi kama hizi wahusika hupata fidia ya kiasi cha pesa, Bima ya afya, mafunzo ya kazi fulani,na huduma za kisaikolojia.
Marekani pia kuna mzee mmoja juzi kati kaachiwa alikuwa kafungwa kimakosa ila yeye akapewa fidia nahisi billion 13 za tz sikumbuki kiasi vzr ila kapewa hela nyingi tu
 
Kiasi fulani ukizaliwa mwanaume ulimwengu unakuwa katili kwako.
Hasa nyakati hizi za women empowerment. Wanasikilizwa sana bila kuzingatia wasemacho ni sahihi?
Shule nyingi za bweni zinazotoa elimu bora na huduma nzuri Ni kwa ajili ya watoto wakike.
Hili aliizungumzia mahali fulani aliyekuwa Spika wa Binge Job Ndugai, and he was right 100%.
Kabisa tena ukiwa masikini ndo balaa
 
Kwa nchi za wenzetu kesi kama hizi wahusika hupata fidia ya kiasi cha pesa, Bima ya afya, mafunzo ya kazi fulani,na huduma za kisaikolojia.
Sio wote mkuu.. kuna scenarios wamejiwekea ili wasikulipe pia. Nishaona kesi kibao IDx watu wamekaa gerezani kuanzia ujana wao hadi uzee kimakosa na hawalipwi chochote.
Shida huwa inaanzia pale ambapo wapelelezi wanaanza upelelezi wakiwa tayari na suspect kichwani ambapo huwa inawafanya wawe vipovu kuona suspect wengine na ushahidi mwingine. So kupitia kile wanachoamini wanaanza kutengeneza scenario zao na kutafiti ushahidi wa kuunga mkono wanachokiamini.
 
Alipwe fidia na nani kama huyo bibi na wajukuu zake ni hohehahe? Labda kama kesi hiyo ilikuwa ni ya jamhuri imlipe fidia
 
Back
Top Bottom