Pride Tanzania
New Member
- Dec 19, 2024
- 2
- 22
Aliyekuwa makamu mkuu wa Chuo cha kilimo Sokoine SUA kuanzia mwaka 1989 mpaka 2006 na Mwenyekiti BODI ya MIKOPO kuanzia 2008 mpaka 2016...amefariki DUNIA hapo Jana tarehe 18dec2024 mkoani Morogoro...!
Ikumbukwe marehemu alifanya kazi na Marais wastaafu Mwl Julius Kambarage Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete..na pia alikuwa mjumbe wa BODI mbalimbalj ikiwemo necta, na nk
Marehemu alikuwa ni msomi na mhadhiri mbobevu kwenye sekta ya kilimo, akitokea idara ya crop science akiwa ni Professor wa fani ya pasture Agronomy...!
=======================
BURIANI MWANAZUONI NA MWANASAYANSI PROF. ANSELM BISEKO LWOGA:*
MAFANIKIO YA CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) NI MATOKEO YA UONGOZI WAKE ULIOTUKUKA;
ALIKUWA DVC (TAALUMA) WA KWANZA SUA NA VC WA PILI, IKIWA NI MIAKA MINNE (4) TU TOKA SUA IWE CHUO KIKUU;
ALISTAAFU MWAKA 2006 SUA IKIJULIKANA DUNIANI KOTE KAMA TAASISI KUBWA YA ELIMU NCHINI.
Na Derek MURUSURI, Dodoma.
19 Disemba, 2024
Jana (18 Disemba, 2024), nimeona tangazo la kulala usingizi wa mauti, Prof. Anselm Biseko LWOGA (78), aliyewahi Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wa pili na Naibu Makamu wa Mkuu Mkuu wa Chuo Kikuu (Taaluma) wa kwanza.
Mwenyezi Mungu amrehemu Prof. Lwoga, ambaye hajaondoka kizembe, la hasha. Ana rekodi ya kipekee sana katika utumishi wake kwa umma wa Watanzania.
Katika uga wa elimu ya juu, hasa katika sayansi, Prof. Anselm Biseko Luoga ni SHUJAA.
Prof. Anselm Biseko Lwoga ndiye aliyeisuka SUA kufikia mafanikio makubwa ambayo yamepatikana hadi leo.
Ni kwa sababu ya uadilifu, ubunifu, uchapa kazi na maono ya Prof. Lwoga, ambaye pia ni Baba mzazi wa Mkuu wa Chuo cha CBE, Prof. Edda Lwoga. Hakika maji hufuata mkondo.
Ukuaji wa SUA, kwa zaidi ya asilimia 99, unatokana na uongozi mahiri wa Prof. Anselm Biseko Lwoga.
Aliaminiwa na kufanywa Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu (SUA) wa kwanza na miaka minne tu baada ya SUA kuwa Chuo Kikuu kamili.
Akaaminiwa kuwa VC, tena VC wa pili na kukiongoza Chuo kikuu hicho kwa miaka 18 hadi tarehe 15 Juni, 2006 alipostaafu.
Alikuwa miongoni mwa viongozi waadilifu sana nchini tena wale wasiopendezwa kabisa na aina yo yote ya rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma
Ikumbukwe marehemu alifanya kazi na Marais wastaafu Mwl Julius Kambarage Nyerere, Ally Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete..na pia alikuwa mjumbe wa BODI mbalimbalj ikiwemo necta, na nk
Marehemu alikuwa ni msomi na mhadhiri mbobevu kwenye sekta ya kilimo, akitokea idara ya crop science akiwa ni Professor wa fani ya pasture Agronomy...!
=======================
BURIANI MWANAZUONI NA MWANASAYANSI PROF. ANSELM BISEKO LWOGA:*
MAFANIKIO YA CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) NI MATOKEO YA UONGOZI WAKE ULIOTUKUKA;
ALIKUWA DVC (TAALUMA) WA KWANZA SUA NA VC WA PILI, IKIWA NI MIAKA MINNE (4) TU TOKA SUA IWE CHUO KIKUU;
ALISTAAFU MWAKA 2006 SUA IKIJULIKANA DUNIANI KOTE KAMA TAASISI KUBWA YA ELIMU NCHINI.
Na Derek MURUSURI, Dodoma.
19 Disemba, 2024
Jana (18 Disemba, 2024), nimeona tangazo la kulala usingizi wa mauti, Prof. Anselm Biseko LWOGA (78), aliyewahi Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wa pili na Naibu Makamu wa Mkuu Mkuu wa Chuo Kikuu (Taaluma) wa kwanza.
Mwenyezi Mungu amrehemu Prof. Lwoga, ambaye hajaondoka kizembe, la hasha. Ana rekodi ya kipekee sana katika utumishi wake kwa umma wa Watanzania.
Katika uga wa elimu ya juu, hasa katika sayansi, Prof. Anselm Biseko Luoga ni SHUJAA.
Prof. Anselm Biseko Lwoga ndiye aliyeisuka SUA kufikia mafanikio makubwa ambayo yamepatikana hadi leo.
Ni kwa sababu ya uadilifu, ubunifu, uchapa kazi na maono ya Prof. Lwoga, ambaye pia ni Baba mzazi wa Mkuu wa Chuo cha CBE, Prof. Edda Lwoga. Hakika maji hufuata mkondo.
Ukuaji wa SUA, kwa zaidi ya asilimia 99, unatokana na uongozi mahiri wa Prof. Anselm Biseko Lwoga.
Aliaminiwa na kufanywa Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu (SUA) wa kwanza na miaka minne tu baada ya SUA kuwa Chuo Kikuu kamili.
Akaaminiwa kuwa VC, tena VC wa pili na kukiongoza Chuo kikuu hicho kwa miaka 18 hadi tarehe 15 Juni, 2006 alipostaafu.
Alikuwa miongoni mwa viongozi waadilifu sana nchini tena wale wasiopendezwa kabisa na aina yo yote ya rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma