Tetesi: MWANDISHI NA MFUGAJI

Tetesi: MWANDISHI NA MFUGAJI

ally pazy

Member
Joined
May 24, 2014
Posts
17
Reaction score
27
MWANDISHI:Habari yako mzee, kwani Ng'ombe wako huwa unawalisha nini?
db2bb8f5c2d80d0f09b1fc87ac077d63.jpg

MZEE:Ng'ombe yupi unamuulizia,? Mweupe au mweusi?
MWANDISHI:Mweupe.
MZEE:Huyo namlisha majani.
MWANDISHI:Na mweusi!!!?
MZEE:Namlisha majani pia.
MWANDISHI:Umeanza kufuga lini hawa Ng'ombe wako?
MZEE:Ng'ombe yupi unamuulizia? Mweupe au mweusi?
MWANDISHI: Mweupe.
MZEE:Huyo nimeanza mwaka jana.
MWANDISHI:Na Mweusi!!!?
MZEE:Mwakajana pia.
MWANDISHI:Hivi Ng'ombe wako huwa wanalala wapi?
MZEE:Ng'ombe yupi mweupe au mweusi?
MWANDISHI:Mweupe.
MZEE:Analala hapo kwenye boma.
MWANDISHI:Na mweusi analala wapi!!?
MZEE:Analala kwenye boma pia.
MWANDISHI:*kwahasira* Kwanini nikikuuliza kuhusu Ng'ombe wako naww unaniuliza mweupe au mweusi alafu unatoa majibu sawa????
MZEE:Kwasababu Ng'ombe mweupe ndo wakwangu.
MWANDISHI:Enhe! Na huyo mweusi ni wanani??
MZEE:Ni wangu pia.
 
Back
Top Bottom