Pre GE2025 Mwandishi wa habari, Khalifa Said: Hakuna dalili yoyote inayoashiria kuwa CHADEMA kweli watazuia uchaguzi usifanyike

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Iwe itakavyokuwa cdm inatakiwa iendelee kutoa elimu kuonyesha hakuna haja ya kushiriki uchaguzi kiinimacho. Na wahakikishe wanaweka wazi upuuzi wote unaofanyika kwenye chaguzi. Hali hiyo itachangia uchaguzi kuwa na wapiga kura wachache sana, na itaondoa heshima ya viongozi watakaopatikana kwenye uchaguzi huo wa kihuni.

Wahakikishe wanamwaga sumu kwa wananchi kutoshirikiana na viongozi watakaopatikana kwa chaguzi za kihuni. Hali hii itawafanya viongozi watakaoingia madarakani kuwa na wakati mgumu kushawishi wananchi kuwaunga mkono.
 
Lissu atatumia nguvu ya Umma.
Ataongoza Umma tokea Ubelgiji.
No reforms no election
 
Hoja yao chadema inamashiko kuwa unashirikije uchaguzi ukijua wazi kuwa kura zitaibiwa? ingawaje mbinu na mikakati ya kutoka hapo ni changamoto
 
Rubbish
 
..kushiriki uchaguzi ktk mazingira ya sasa hivi ni kupoteza muda.

..haijalishi Chadema watazuia uchaguzi, au la, mazingira yaliyopo hayatoi nafasi kwa uchaguzi halali.
 
Mtu yoyote anayezungumzia wapinzani kushinda hata kiti cha udiwani kwa kile kilichotokea 2019,2020 na 2024 basi huyo akapimwe akili.
 
Tatizo la Jamaa kikishanuka anakimbia....Hakuna kususia uchaguzi wapambane hivyo hivyo ,mbona Heche alitangazwa kukiwa na vifaru baada ya kutishia wasipomtangaza wanapiga kiberiti mjengo mzima wanateketea wote.

Sisiemu hawahitaji tantalila ,mnatakiwa muwafanyie action za kweli na si za kutishia.
 
Swala la uchaguzi ni swala lakimuafaka kati ya wananchi na serikali yao, swala la uchaguzi halipawi kuwa swala la mashaka mashaka na mfumo mzima wa uchaguzi. Serikali inajua fika wapiga kura wanapungua siku baada ya siku na sababu kubwa nikutokuuamini mfumo mzima na michakato mizima ya uchaguzi. Sasa kukitokea mivutano iliyo wazi kama hii inapaswa kwanza itatuliwe la sivyo ukisema kuwa lolote na liwe uchaguzi utafanyika mtake msitake hiyo inaleta uwalakini katika mchakato mzima wakuwapata wawakilishi halali wawananchi.Tufike mahali Aidha tukubali kufanya uchaguzi au kutofanya tuhalalishe tu watakao teuliwa na wateuzi ndiyo watuongoze zote ni Demokrasia. Sidhani kama ni busara tutumie mabilioni ya fedha kwenye chaguzi kisha tusipate watu sahihi tuliowachagua. Najua watanzania ni wapole na wastaarabu ndiyo maana wanafanyiwa vitimbwi hivi. Tunajua fika uchaguzi hakuna mtu yoyote anaweza kuuzuia ila je hui ndiyo uchaguzi watanzania wanao utaka uchaguzi wakusimamiwa na vifaru na magari ya washawasha. Naamini kabisa jamaa na wagombea ambao wanauhakika wakupita ktk uchaguzi huu wapo tayari kwa lolote lile ili washinde hata kwa kuwanunua watu. Ila hao viongozi wanamna hiyo wana tija kwa taifa? Na unadhani kwanini wapinzani wale wanao onekana wananguvu za uhamasishaji ktk baadhi ya maeneo yao au kwenye vyama vyao wanapotea. CCM bado kinanafasi kubwa ya kushinda hata kutakapo kuwa na chsaguzi huru kutokana na mifumo ya chama chao jinsi walivyo jipanga tatizo lao wanataka washinde kwa asilimia kubwa hapo ndipo ugomvi unapokuja. Upinzani upo sana mijini vijijini hakuna kabisa upinzani hasa mikoa ya Tanga, Mtwara, ruvuma, pwani, Dodoma, Shinyanga, Nk. Nishauri kama CDM haitagombea vikabaki CCM na vyamahivyo vidogo C.c.m isiengue mgobea hata mmoja na uchaguzi kwa upande wa bara usifanyewe manuva yoyote ila manuva wfanyiwe ACT kwa upande wa Zanzibar.
 
Umemaliza ! 🙏
 
Yaani upande wa Zanzibar ndio manuva ifanyike 🤣🤣
Ili Zanzibar ibaki kuwa chini ya Bara dahari na dahari ???!
Wenyewe watakuelewa kweli. ??!
Au unawachokoza ??
Naona hili ni jiwe limerushwa gizani !
Wazanzibari naamini na wao wanaamini kwamba IF it’s not now then it’s NEVER 👎 😳🙄 !
 
CCM DAIMA SAMIA MITANO
 
Kisaka unaonekana hamnazo!! Ukiwauliza how hili jambo litatokea wanakwambia tutahamasisha watu ukiuliza kina nani watashiriki kuzuia wanakwambia wananchi!!

Uchaguzi ni tukio la kikatiba ambapo ni lazima limuliwe kisheria na kikatiba na taratibu zipo wazi!! Nchi Ina vyama 18 Vya siasa na kuna vilivyothibitisha kushiriki chaguzi na vina wafuasi!! Ni Vipi CHADEMA pekee inaweza zuia jambo hili na kwa grounds zipi?

Kingine ni kuwa uongozi mpya umedoda sana mtaani tofauti na ilivyokua wakati wa uchaguzi wao!! Yaani umaarufu wa viongozi umetota vibaya sana!!
 
Na kitu ambacho Lissu hajui ni kwamba John Heche (nikisoma nae SAUT akiitwa Wegesa Charles) sio mtu wa kumuamini kabisa. Ni muoga zaidi ya maneno yake mnayoyasikia.
Na kwa asilimia kubwa miradi mingi binafsi ya Madini aliyotekeleza Biteko huko kanda ya Ziwa inasimamiwa na John Heche!!

Heche ni mwoga, mlafi na mfitini sana!
 
Sasa uwoga wa heche una mahusiano gani na kinachojadiliwa hapa? Ukisoma SAUT Unakuwa mpumbavu hivi
Huna akili!! Ungekua na akili ungeweza unganisha kati ya woga wa kiongozi na utekelezaji wa maazimio. Ujasiri ni sifa moja wapo ya kiongozi!! Sasa mtu mwoga atasimamia vipi ajenda ya No reform No election??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…