TANZIA Mwandishi wa Habari wa Redio Moshi FM amelala Usingizini wa Umauti

TANZIA Mwandishi wa Habari wa Redio Moshi FM amelala Usingizini wa Umauti

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Tunatoa pole kwa familia

Moshi. Mwandishi wa habari wa redio Moshi FM, Deogratius Kessy (26) amefariki dunia katika ajali baada ya gari alilokuwa amepanda kuacha njia na kugonga bajaji.

Kessy alikuwa akitangaza kipindi cha burudani cha The base show katika redio hiyo.

Kifo cha mwandishi huyo kimetokea ikiwa zimepita siku 35 tangu mwandishi mwingine wa habari wa redio Kili FM mjini Moshi, Benedick Kuzwa kufariki dunia katika ajali.

Akizungumza leo Jumamosi Desemba 12, 2020 kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Emmanuel Lukula amesema ajali hiyo imetokea jana saa 2 usiku katika barabara ya Getifonga eneo la kona ya kibao cha kuelekea Kahe.

Amesema gari aina ya Noah lililokuwa limepakia watu zaidi ya wawili likitokea Newland kwenda mjini Moshi ilipofika katika kona hiyo liligonga bajaji na kuwajeruhi watu watatu na mwandishi huyo kufariki dunia wakati akipatiwa matibabu hospitali ya rufaa Mkoa wa Kilimanjaro.

“Kwenye ile Noah watu wawili walipata zaidi majeraha na waliwahishwa hospitali ila mmoja ndio amefariki. Kwenye ile bajaji mama mmoja alivunjika miguu yote miwili na majeruhi wote wanaendelea na matibabu,” amesema.

Akizungumza na Mwananchi Digital meneja vipindi wa redio hiyo, Rodrick Makundi amesema, “tumepokea taarifa hizi kwa masikitiko makubwa hakika tutamkumbuka Deogratius kwa mambo mengi mazuri kwani alikua mchapakazi mzuri. Alikuwa anatoa ushauri pale unapohitajika pia tulijifunza mambo mengi mazuri kutoka kwake kutokana na ubunifu wake kwenye vipindi alivyokua akifanya.”

1607789564619.png
 
Pole kwa familia na hongera kwake kwa kufanikiwa kuchomoka gerezani
 
Kuna ajali pia jana mida ya saa nane pale sam nujoma mataa ya mbele ya mawasiliano duuh niseme ukweli sijawahi shuhudia live ajali nilitetemeka balaa!

Wakati nasubiria taa ziruhusu, Kuna mgari wa jeshi mkubwa ulikaparamia ka vitz ulikaponda ponda sijui kama watu walipona mlee![emoji1745][emoji1751][emoji26]

Mliopita jana pale mida ya saa kumi mliona huo msala [emoji26]

RIP mwandishi
 
Tunatoa pole kwa familia


Moshi. Mwandishi wa habari wa redio Moshi FM, Deogratius Kessy (26) amefariki dunia katika ajali baada ya gari alilokuwa amepanda kuacha njia na kugonga bajaji.

Kessy alikuwa akitangaza kipindi cha burudani cha The base show katika redio hiyo.

Kifo cha mwandishi huyo kimetokea ikiwa zimepita siku 35 tangu mwandishi mwingine wa habari wa redio Kili FM mjini Moshi, Benedick Kuzwa kufariki dunia katika ajali.

Akizungumza leo Jumamosi Desemba 12, 2020 kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Emmanuel Lukula amesema ajali hiyo imetokea jana saa 2 usiku katika barabara ya Getifonga eneo la kona ya kibao cha kuelekea Kahe.

Amesema gari aina ya Noah lililokuwa limepakia watu zaidi ya wawili likitokea Newland kwenda mjini Moshi ilipofika katika kona hiyo liligonga bajaji na kuwajeruhi watu watatu na mwandishi huyo kufariki dunia wakati akipatiwa matibabu hospitali ya rufaa Mkoa wa Kilimanjaro.

“Kwenye ile Noah watu wawili walipata zaidi majeraha na waliwahishwa hospitali ila mmoja ndio amefariki. Kwenye ile bajaji mama mmoja alivunjika miguu yote miwili na majeruhi wote wanaendelea na matibabu,” amesema.


Akizungumza na Mwananchi Digital meneja vipindi wa redio hiyo, Rodrick Makundi amesema, “tumepokea taarifa hizi kwa masikitiko makubwa hakika tutamkumbuka Deogratius kwa mambo mengi mazuri kwani alikua mchapakazi mzuri. Alikuwa anatoa ushauri pale unapohitajika pia tulijifunza mambo mengi mazuri kutoka kwake kutokana na ubunifu wake kwenye vipindi alivyokua akifanya.”
Huyo Kuzwa alifariki kwa ajali au aliuwawa? Si ndo huyo alikuwa anajiita Zangii Koroboi ya Nishati? Hicho kituo kichunguzwe

Sent from my EVA-L19 using JamiiForums mobile app
 
Bajaji & pikipiki mtatumaliza jamani.. sawa yawezekana likawa kosa la dereva noah lakini ukiwa barabarani never use ur 100%, weka balance walau kidogo incase!! Uhai haurudi ila kuchelewa unakokwemda kunaweza kurekebishika in team ya finance, kuwahi home ..etc

RIP, ulikiwa abilia huna kosa!!
 
Mambo ya kufa siyapendi kisenge Yani....Yani ukifa unakua huoni sura Tata za akina joashi onyango...polepole...juma kaseja.....n.k

Mambo ya kufa siyapendi kisenge Yani....Yani ukifa unakua huoni sura Tata za akina joashi onyango...polepole...juma kaseja.....n.k
Kufa kisemhe pia ni kosa..at age of 25 to 35 kijana lazima ujilinde sana...kijana akipita age hii kufa kijinga huwa ni ngumu.
 
Back
Top Bottom