BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
Dampo la Buhongwa lipo eneo la Manispaa ya Nyamagana Jiji Mwanza, rekodi za Serikalini zinaonesha lilijengwa kwa gharama ya shilingi Milioni 8.87.
Licha ya ukubwa wa Dampo hilo ambalo awali wakati linajengwa Mwaka 2020 lilisifiwa kuwa ni sehemu sahihi ya kuhifadhi taka lakini mambo yamebadilika sana ndani ya muda mfupi kutokana na uchafu uliokithiri eneo hilo.
Kutokana na uchafu kuzidi eneo hilo kuna wakati mamlaka zinazohusika zilianza kumwaga kemikali fulani kwa lengo la kukata harufu na mara kadhaa kutumia kemikali hizo kuchoma taka lakini hilo halijasaidia.
Kinachotia shaka zaidi ni kuwa karibu na dampo hilo kuna soko maarufu kwa jina la Soko la Dampo, hivyo usalama wa dampo unapoyumba inamaanisha kiafya pia sio salama.
Katika dampo hilo na maeneo yote ya jirani kuna harufu kali na mbaya ambayo imesababisha wengi wetu tuwe tunaumwa vifua, matumbo ikiwemo kuharisha.
Magari ya taka yanayofika hapo kumwaga yanamwaga kiholela, ni kama kila mtu anafanya anavyojua yeye, hakuna utaratibu wa kueleweka.
Mvua zinaponyesha hali inakuwa mbaya kuliko maelezo, uchafu unasambaa na hata vile vyakula vinavyouzwa katika soko lililopo jirani na Dampo navyo sio salama kiafya.
Kuna kikundi cha Watu kinafanyabiashara ya kuuza mchanga eneo hilo la kwa ndani na inapotokea wanajua kuna Kiongozi anaenda eneo hilo, wanachofanya ni kuziba mashimo yaliyochibwa kwa kuweka mbolewa zinazozalishwa humo inamaanisha wanaziba mashimo.
Pia ukionekana tu unafika eneo hilo kwa ukaribu maswali yanakuwa mengi unakwenda wapi na mengineyo hii inaleta taswira hasi ya kile kuinachoendelea kwenye dampo hilo.
Hii tabia haijazungumzwa kwa wingi lakini inaweza kuwa chanzo cha kuharibu mazingira zaidi na zaidi.
Kemikali zinaumiza Watu
Mbali na hapo uchomaji taka unapokuwa unafanyika hasa kwa kuwa unahusisha nia ya kupunguza harufu kali, moto unachukua muda mrefu kuzima, moshi unakuwa ni kero na athari kubwa kwetu.
Vyoo havitumiki inavyotakiwa
Licha ya kuwa kuna vyoo lakini baadhi ya Watu katika Soko la Dampo wamekuwa wakijisaidia sehemu ambazo sio rasmi, ukijumlisha na uwepo wa Dampo na hizo changamoto zake kinachotokea ni uharibifu mkubwa wa usafi wa mazingira.
Pamoja na yote hayo kumekuwa na ahadi nyingi za viongozi kuhusu maboresho ya Dampo hilo lakini hakuna kinachofanyika cha maana.
PICHA ZIKIONESHA UJENZI WA DAMPO ULIVYOKUWA
Licha ya ukubwa wa Dampo hilo ambalo awali wakati linajengwa Mwaka 2020 lilisifiwa kuwa ni sehemu sahihi ya kuhifadhi taka lakini mambo yamebadilika sana ndani ya muda mfupi kutokana na uchafu uliokithiri eneo hilo.
Kutokana na uchafu kuzidi eneo hilo kuna wakati mamlaka zinazohusika zilianza kumwaga kemikali fulani kwa lengo la kukata harufu na mara kadhaa kutumia kemikali hizo kuchoma taka lakini hilo halijasaidia.
Kinachotia shaka zaidi ni kuwa karibu na dampo hilo kuna soko maarufu kwa jina la Soko la Dampo, hivyo usalama wa dampo unapoyumba inamaanisha kiafya pia sio salama.
Magari ya taka yanayofika hapo kumwaga yanamwaga kiholela, ni kama kila mtu anafanya anavyojua yeye, hakuna utaratibu wa kueleweka.
Mvua zinaponyesha hali inakuwa mbaya kuliko maelezo, uchafu unasambaa na hata vile vyakula vinavyouzwa katika soko lililopo jirani na Dampo navyo sio salama kiafya.
UUZWAJI WA MCHANGA
Kuna kikundi cha Watu kinafanyabiashara ya kuuza mchanga eneo hilo la kwa ndani na inapotokea wanajua kuna Kiongozi anaenda eneo hilo, wanachofanya ni kuziba mashimo yaliyochibwa kwa kuweka mbolewa zinazozalishwa humo inamaanisha wanaziba mashimo.
Pia ukionekana tu unafika eneo hilo kwa ukaribu maswali yanakuwa mengi unakwenda wapi na mengineyo hii inaleta taswira hasi ya kile kuinachoendelea kwenye dampo hilo.
Hii tabia haijazungumzwa kwa wingi lakini inaweza kuwa chanzo cha kuharibu mazingira zaidi na zaidi.
Mbali na hapo uchomaji taka unapokuwa unafanyika hasa kwa kuwa unahusisha nia ya kupunguza harufu kali, moto unachukua muda mrefu kuzima, moshi unakuwa ni kero na athari kubwa kwetu.
Vyoo havitumiki inavyotakiwa
Licha ya kuwa kuna vyoo lakini baadhi ya Watu katika Soko la Dampo wamekuwa wakijisaidia sehemu ambazo sio rasmi, ukijumlisha na uwepo wa Dampo na hizo changamoto zake kinachotokea ni uharibifu mkubwa wa usafi wa mazingira.
Pamoja na yote hayo kumekuwa na ahadi nyingi za viongozi kuhusu maboresho ya Dampo hilo lakini hakuna kinachofanyika cha maana.
PICHA ZIKIONESHA UJENZI WA DAMPO ULIVYOKUWA