Mwanza: Mama akamatwa kwa kumzika mwanaye akiwa hai ili apate utajiri

Mwanza: Mama akamatwa kwa kumzika mwanaye akiwa hai ili apate utajiri

Dr. Wansegamila

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2012
Posts
2,968
Reaction score
8,139
Kutoka mkoani Mwanza Jeshi la Polisi inamshikilia Zawadi Msagaja (20) na wenzake wawili akiwemo mganga wa kienyeji, kwa tuhuma za kumzika mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili akiwa hai, kwa lengo la kumtoa kafara ili apate utajiri.

Watuhumiwa wengine ni dada yake Zawadi, Elizabeth Kaswa na mganga wa kienyeji, Mussa Mazuri.

Tukio hilo lilitokea Novemba 13, mwaka huu, katika Mtaa wa Kisundi, Kata ya Bugogwa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mganga huyo alimpa Zawadi maagizo ya kutekeleza kitendo hicho, huku akimtishia asipofanya hivyo angemtoa yeye kafara.

"Mwanamke huyo alikuwa akiishi kwa dada yake, alifanya unyama huo baada ya kutishwa na mganga wa kienyeji ambaye ni shemeji yake Mussa James Mazuri (31), amtoe kafara mtoto wake wa kike Neema Claud mwenye umri wa miezi miwili, wote watatu wapate utajiri, endapo angekataa angemtoa yeye kafara." amesema Kamanda Mutafungwa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.
FB_IMG_1670134290173.jpg
 
Hao Wasukuma Ni washenzi Sana,juzi hapo wameua Askofu mstaafu wa Anglicana na kumtupa kando ya Ziwa achilia mbali kwamba wameanza kuua Tena Albino.
 
Hao Wasukuma Ni washenzi Sana,juzi hapo wameua Askofu mstaafu wa Anglicana na kumtupa kando ya Ziwa achilia mbali kwamba wameanza kuua Tena Albino.
Hii unageneralize sana mkuu... Kwani sababu ya Askofu kuuwawa ni nini? Sio tu labda ujambazi au visasi vya mambo binafsi?
 
Hii unageneralize sana mkuu... Kwani sababu ya Askofu kuuwawa ni nini? Sio tu labda ujambazi au visasi vya mambo binafsi?
Huyu jamaa huwa anajitoa ufahamu hivyo jua kuwa unajadiliana na mtu aina ya Shaka wa CCM. All in all, uhalifu hauna kabila wala kanda. Nchi nzima inanuka imani za kishirikina. Na pia ujambazi au sababu binafsi siyo tiketi ya mauaji bila kufuata sheria.
 
Yote inaonesha hamna ustaarabu hata kidogo
Ni kweli kabisa. Ila suala la ujambazi, ushirikina na mauaji ni suala ambalo lipo sehemu nyingi za Tanzania na sio kuwa la kusema kuwa ni la wasukuma tuu. Uhalifu hauna kabila wala ukanda mkuu.
Jamii nyingi za Kitanzania kwa asilimia kubwa zimejaa sana imani na tabia za kishirikina.
 
Ila wataroga na hawatafungwa.
Ile kesi nyingine kama hii iliishia kwa dpp kufuta shitaka lao . "Serikali haina nia ya kuendelea na kesi hii". DPP alisema hivyo
 
Wasukuma kama kawaida yao
Mbona haya matukio ya mauaji na ushirikina yapo sehemu nyingi tu za Tanzania mkuu? They are not unique kwa wasukuma tuu, haya mambo tunayaona na kuyasikia kila siku kwenye jamii zetu nyingi.
 
Mbona haya matukio ya mauaji na ushirikina yapo sehemu nyingi tu za Tanzania mkuu? They are not unique kwa wasukuma tuu, haya mambo tunayaona na kuyasikia kila siku kwenye jamii zetu nyingi.

Wasukuma wapo juu sana kwenye ushirikina, si wa mauaji pekee...
 
Kutoka mkoani Mwanza Jeshi la Polisi inamshikilia Zawadi Msagaja (20) na wenzake wawili akiwemo mganga wa kienyeji, kwa tuhuma za kumzika mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili akiwa hai, kwa lengo la kumtoa kafara ili apate utajiri.

Watuhumiwa wengine ni dada yake Zawadi, Elizabeth Kaswa na mganga wa kienyeji, Mussa Mazuri.

Tukio hilo lilitokea Novemba 13, mwaka huu, katika Mtaa wa Kisundi, Kata ya Bugogwa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mganga huyo alimpa Zawadi maagizo ya kutekeleza kitendo hicho, huku akimtishia asipofanya hivyo angemtoa yeye kafara.

"Mwanamke huyo alikuwa akiishi kwa dada yake, alifanya unyama huo baada ya kutishwa na mganga wa kienyeji ambaye ni shemeji yake Mussa James Mazuri (31), amtoe kafara mtoto wake wa kike Neema Claud mwenye umri wa miezi miwili, wote watatu wapate utajiri, endapo angekataa angemtoa yeye kafara." amesema Kamanda Mutafungwa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.
View attachment 2435256
Je mtoto aliokolewa au la? Ccm kama mnajali, okoeni hili taifa!
 
Kutoka mkoani Mwanza Jeshi la Polisi inamshikilia Zawadi Msagaja (20) na wenzake wawili akiwemo mganga wa kienyeji, kwa tuhuma za kumzika mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili akiwa hai, kwa lengo la kumtoa kafara ili apate utajiri.

Watuhumiwa wengine ni dada yake Zawadi, Elizabeth Kaswa na mganga wa kienyeji, Mussa Mazuri.

Tukio hilo lilitokea Novemba 13, mwaka huu, katika Mtaa wa Kisundi, Kata ya Bugogwa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mganga huyo alimpa Zawadi maagizo ya kutekeleza kitendo hicho, huku akimtishia asipofanya hivyo angemtoa yeye kafara.

"Mwanamke huyo alikuwa akiishi kwa dada yake, alifanya unyama huo baada ya kutishwa na mganga wa kienyeji ambaye ni shemeji yake Mussa James Mazuri (31), amtoe kafara mtoto wake wa kike Neema Claud mwenye umri wa miezi miwili, wote watatu wapate utajiri, endapo angekataa angemtoa yeye kafara." amesema Kamanda Mutafungwa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.
View attachment 2435256
Inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom