Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
WanaJF,
Mada hii itakuwa na 'Updates' za Matukio kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Mwanza. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka.Mkoa wa Mwanza ni moja ya mikoa muhimu nchini Tanzania, ukiwa katikati ya Kanda ya Ziwa na ukipakana na Ziwa Victoria. Ni mkoa wa pili kwa idadi ya watu baada ya Dar es Salaam na ni kitovu cha biashara, usafiri, na uchumi wa Kanda ya Ziwa.
MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA MWANZA
Katika muhtasari wa maeneo ya utawala, mkoa huu una halmashauri ambazo zimegawanyika katika mamlaka za miji na wilaya.
Idadi ya Watu
Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa na idadi ya watu katika Mkoa wa Mwanza ni 3,699,872; wanaume 1,802,183 na wanawake 1,897,689 ikiwa na walaya 8.Idadi ya Majimbo ya Uchaguzi
Mwanza ina jumla ya majimbo 9 ya uchaguzi:- Jimbo la Nyamagana
- Jimbo la Ilemela
- Jimbo la Magu
- Jimbo la Misungwi
- Jimbo la Kwimba
- Jimbo la Sengerema
- Jimbo la Buchosa
- Jimbo la Ukerewe
- Jimbo la Sumve
Katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, Mkoa wa Mwanza Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilifanikiwa kushinda kwa wingi katika ngazi zote.
Katika uchaguzi wa rais, Hayati John Magufuli wa CCM alipata kura nyingi zaidi mkoani Mwanza, huku wagombea wa upinzani wakipata kura chache kwa ujumla.
Kwa upande wa ubunge, CCM ilishinda majimbo yote ya mkoa huo, na mgombea mmoja alishinda bila kupingwa katika jimbo la Misungwi.
Kwa ngazi ya udiwani, CCM ilipata viti 189 kati ya kata 191 zilizopo mkoani Mwanza, huku kata mbili tu zikichukuliwa na CHADEMA katika jimbo la Sumve
Updates
January
February
- Pre GE2025 - Mzee Wasira apokelewa rasmi Mwanza, ateta na kamati ya siasa ya mkoa
- Pre GE2025 - Mzee Wasira: Hakuna anayeweza kuahirisha uchaguzi mkuu, watanzania wajiandae
- Pre GE2025 - Mwenyekiti BAVICHA Mwanza: Uchaguzi ukiwa huru, CHADEMA tunachukua nchi
- Pre GE2025 - Baba Levo atangaza kuzunguka nchi nzima kukagua miradi ya Samia kwenye kampeni ya "Mama Hana Deni". CCM ndo mmeishiwa kiasi hiki?
- Pre GE2025 - Video: Innocent Bashungwa naye atinga mtaani kula kwenye mgahawa pamoja na wananchi. Tunamshukuru Rais Samia!
- Pre GE2025 - Mwanza: Katibu wa UVCCM Sengerema aonya makada wa CCM ambao wameanza kuhujumu mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM
- Pre GE2025 - CHADEMA Mwanza kuandamana kesho Februari 19, 2025 hadi ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupinga mauaji na utekaji wa viongozi wao
- Pre GE2025 - RC Mtanda azungumzia suala la Katibu wa BAVICHA- Mwanza kupotea, asema serikali haina lengo la kumteka yeyote yule
- Pre GE2025 - Amani Manengelo, Katibu wa BAVICHA Mkoa wa Mwanza, ameripotiwa kutekwa na kupotea tangu tarehe 14.02.2025 huko Misungwi
- Pre GE2025 - Maandamano ya CHADEMA Mwanza kupinga kutoweka kwa Katibu wa BAVICHA yapigwa marufuku
- Pre GE2025 - CHADEMA, RC Mwanza na Polisi wajadili madai ya kutekwa kwa Katibu wa BAVICHA, Watatu wakamatwa
- Pre GE2025 - Eric Shigongo: Miaka mitatu ya Rais Samia Buchosa imeendelea sana
- Pre GE2025 - Ilemela Mwanza: Vikundi 60 vinatarajia kunufaika na mkopo wa Shilingi bilioni 1.13
- Pre GE2025 - Sekretarieti ya CCM mkoa yawataka Wazee wilaya ya Missenyi kuchagua viongozi wanaokubalika
- Pre GE2025 - UVCCM Mwanza waunga mkono NETO, Waitaka Serikali Itoe Ajira
- Pre GE2025 - Shigongo atoa milioni 10 kukamilisha ujenzi wa Zahanati uliosimama kwa miaka 15 Buchosa
ZINGATIA: Mikoa yote ina mada yake ya 'Update' ili kuweka wepesi katika ufuatiliaji.