Mwaunda kamati ya kuongeza posho?

Mwaunda kamati ya kuongeza posho?

MKEHA

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
716
Reaction score
1,143
Nakua kama naota vile, sijui ni kweli au naota mchana jamani, eti Pandu Kificho mwenyekiti wa muda wa bunge maalum ameinda kamati ya kuchunguza kama malipo ya laki tatu 300,000 wanazolipwa wajumbe wa bunge la katiba ichunguzwe kama inafaa au iongezwe. Jamani mbona tunafanyia hivyo, mimi nimwalimu kwa taaluma na nimeajiriwa halmashauri ya Bagamoyo nalipwa 470000 kwa mwezi pamoja kuwa na shahasa ya chuo kikuu, tena naidai serikali mishahara yangu miwili kwa sababu wakati naanza kazi sikulipwa miezi 2 na toka mwaka 2011 nimekua nazisotea hizo pesa bila mafanikio, siyo mimi peke yangu, kwenye kituo napofanyia kazi walimu wote 14 tunaidai serikali malimbikizo hayo ya mishahara na wengine fedha ya uhamisho.Chama cha walimu wakiitisha mgomo ili serikali itupe hela yetu mawakili wa serilaki wanakwenda kuweka pingamizi tena usiku wakati majaji wamelala eti kubatisha mgomo lakini sioni hata mara moja bunge likiunda kamati ndogo kama hiyo kuangalia madai hayo, halafu mnategemea Big Results Now kutoka kwa walimu walionyimwa stahiki zao. Kumbukeni kwamba walimu wengi wanaishi kwa mikopo na wengine hupokea hata chini ya laki moja kwani wamekopa kwenye mabenki zaidi ya moja. Halafu wajumbe mnasema posho ya laki tatu kwa siku haiwatoshi jamani, huo ndio uzalendo na wito mnaoutaka walimu na waganga waunyeshe kwa jamii ilihali nyie hamna hata chembe ya uzalendo kiasi hicho? Jamani eti hamuwezi kulala kwenye guest za uchochoroni, wenzenu huku pamoja na madgree tuliyonayo tunalala kwenye nyumba za majani, hakuna maji, umeme, barabara, zahanati, mtandao, barabara wala huduma yoyote ya jamii unayoijua wewe lakini mbona tunaishi, tena ni kwenye jimbo la mheshimiwa rais. Kama kweli kamati ikija na pendekezo la kuongeza hiyo posho nitaacha kazi na niwe mkulima tu ili nisiendelee kuitesa nafsi yangu kwa manunguniko maana najua hata kama nikisema niendelee na kazi ufanisi utakua zero kwani muda wote nitakua nawaza unyonge wa kazi ya ualimu. Bora nifanye kazi nyingine kuliko chukizo hili la ajabu kwa wachache kula nchi huku mimi nikiidai serikali bila dalili zozote za kulipwa.
 
DUH! i can smell your pain! vumilia tu mkuu,nakushauri usiache kazi ila unaweza tafuta mtaji kwa kazi ya ualimu baadaye ukarudi mjini,nawe ukiwa kama slave master!
 
duu!kwel nao wanataka wafaidike kutokana na hilo!!
 
Mlitegemea nini kama Bunge Lina wawakilishi wa wauaji wa Alibino? Na sijaona albino walimpiga Kingunge ?
 
kamati yeyenye ya kuangalia posho....ikikaa vikao nao wanalipwa posho.....ni posho kila mahali...dk analala hospitali unampa elfu kumi
 
Hivi hao kamati waliounda wao awataki posho. Mnafikiri kunajipya hapo kesi ya nyani unampelelea ng'endere shamba litaisha
 
watu wana lalamika mishahara midogo, hii mikubwa mizima eti laki 3 ndogo....walaaniwe tu!
 
Unajua mwanzoni sikuelewa vizuri mambo ya posho ya hili bunge maalum. Nilidhani ni laki3 kwa mwezi ndo maana wanalalamika....kumbe ni mil21 kwa mwezi?!?!?!?!?!?!!!!.......Hawa watu wanataka kuleta madhara..............Kwa haraka napendekeza hili zoezi lisimame kwanza.
 
Unajua mwanzoni sikuelewa vizuri mambo ya posho ya hili bunge maalum. Nilidhani ni laki3 kwa mwezi ndo maana wanalalamika....kumbe ni mil21 kwa mwezi?!?!?!?!?!?!!!!.......Hawa watu wanataka kuleta madhara..............Kwa haraka napendekeza hili zoezi lisimame kwanza.
hapa najisikia kufa kufa. mil21 na bado wanataka wongezewe?
mimi nashauri serikali iwaongezee iwe laki 7 ila wakatwe kodi 80%.
 
Hivi mlimsikia Lukuvi akiongea leo kwenye PB ya clouds ?

Kiufupi watanzani tuna laana ya ubinafsi, uroho na roho mbaya.......ndio maana kila anayepewa dhamana anachofikiria ni atoke vipi.

Miradi ya maji ambayo ni uhai wa watu utaambiwa bajeti ni finyu......lakini kundi fulani la watanzania wanakaa mahali na kulipana milioni 21 kwa mwezi.

Ndio maana kuna wakati unawaangalia jamaa wa Ukraine unapata picha inauma kiasi gani pale ambapo kundi fulani la watu kujiona wa maana kuliko wengine ndani ya nchi hiyohiyo moja.
 
Unajua mwanzoni sikuelewa vizuri mambo ya posho ya hili bunge maalum. Nilidhani ni laki3 kwa mwezi ndo maana wanalalamika....kumbe ni mil21 kwa mwezi?!?!?!?!?!?!!!!.......Hawa watu wanataka kuleta madhara..............Kwa haraka napendekeza hili zoezi lisimame kwanza.

naunga MKONO hoja, hili zoezi lisimame, hawa asasi za kiraia waliozungumzia kwenda mahakamani kwa ajiri ya kulisimamisha ili Bunge bora wakafanikiwe tu..
 
naunga MKONO hoja, hili zoezi lisimame, hawa asasi za kiraia waliozungumzia kwenda mahakamani kwa ajiri ya kulisimamisha ili Bunge bora wakafanikiwe tu..

Yataka moyo sana kuwasikiliza hawa jamaaa.......moja kwa moja hata wakikubali inamaanisha watakuwa na kinyongo kwa sababu shamba la bibi limegoma. Kuna uwezekano mkubwa wakapitisha katiba yoyote ili mradi liende
 
Back
Top Bottom