makachu Makachu
New Member
- Jan 13, 2025
- 4
- 4
Watendaji idara ya maji Mkoa wa Mwanza Jitafakarini na chukueni hatua za haraka!Eneo Na mitaa ya Nyegezi stendi.
Mwanza ni jiji kubwa ambalo, kwa idadi ya watu, ni jiji la pili kwa Tanzania.
Kumekuwa na changamoto kubwa sana ya maji ambayo haieleweki, na watendaji wako wametulia kabisa bila kutoa majibu.
Kwa makadirio, baadhi ya maeneo ya mijini yanapata maji kwa takriban mara Moja kwa nayo yakitoka nikama tone ndani ya wiki mbili, na sehemu fulani hakuna maji kwenye mitaa; mfano, katika Nyegezi, stendi ambapo ni mijini hakuna maji kabisa katika mitaa mingi.
Serikali imekamilisha mradi wa maji butimba, lakini kumekua hadithi tu; maji hayupo, wala taarifa sahihi hazipo.
Enyi watendaji, tuambieni: mnalipwa kodi za nani?
Madharani Kila mwezi , bili za maji kila mwezi mnatuma Tena kubwa mnazotoa wapi?
Tunaomba viongozi wa idara ya maji, ngazi ya juu: tokeni ofisini, piteni mitaani, na ulizeni kwa raia hawa vijana michezo; hakuna maji!
Waziri husika, tunaomba ufanye ziara; tembelea mitaa. Usiende tu kwenye mitaa uliyo pangiwa, bali piga hatua kuelekea mitaa ambayo hawajakupangia. Utapata ukweli wa tatizo hili la maji.
Katika mitaa mingine, maji yanatoka kama tone la "Moja la Mvua". Kuna shida gani? Au mnasubiri ziara za viongozi wakubwa, mnafungulia maji mpaka mabomba yanapasuka?
Mfano, katika kila mtaa, katika kilele cha mwenge au ziara ya Mweshimiwa Raisi maji yanatoka Hadi mabomba yanapasuka watu wanauliza yanatokea wapi?
Tambueni , mnaishi kwa kodi zetu! Msisubiri uchaguzi, hapo ndipo mnatoka kutudanya katika mitaani.
Chukuni hatua ya haraka kusuluhisha jambo hili.
Cc: Waziri wa Maji & Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Pia soma > KERO - Idara ya Maji Nyegezi Mwanza (MWAUWASA) jitafakarini suala la ukosefu wa maji
Mwanza ni jiji kubwa ambalo, kwa idadi ya watu, ni jiji la pili kwa Tanzania.
Kumekuwa na changamoto kubwa sana ya maji ambayo haieleweki, na watendaji wako wametulia kabisa bila kutoa majibu.
Kwa makadirio, baadhi ya maeneo ya mijini yanapata maji kwa takriban mara Moja kwa nayo yakitoka nikama tone ndani ya wiki mbili, na sehemu fulani hakuna maji kwenye mitaa; mfano, katika Nyegezi, stendi ambapo ni mijini hakuna maji kabisa katika mitaa mingi.
Serikali imekamilisha mradi wa maji butimba, lakini kumekua hadithi tu; maji hayupo, wala taarifa sahihi hazipo.
Enyi watendaji, tuambieni: mnalipwa kodi za nani?
Madharani Kila mwezi , bili za maji kila mwezi mnatuma Tena kubwa mnazotoa wapi?
Tunaomba viongozi wa idara ya maji, ngazi ya juu: tokeni ofisini, piteni mitaani, na ulizeni kwa raia hawa vijana michezo; hakuna maji!
Waziri husika, tunaomba ufanye ziara; tembelea mitaa. Usiende tu kwenye mitaa uliyo pangiwa, bali piga hatua kuelekea mitaa ambayo hawajakupangia. Utapata ukweli wa tatizo hili la maji.
Katika mitaa mingine, maji yanatoka kama tone la "Moja la Mvua". Kuna shida gani? Au mnasubiri ziara za viongozi wakubwa, mnafungulia maji mpaka mabomba yanapasuka?
Mfano, katika kila mtaa, katika kilele cha mwenge au ziara ya Mweshimiwa Raisi maji yanatoka Hadi mabomba yanapasuka watu wanauliza yanatokea wapi?
Tambueni , mnaishi kwa kodi zetu! Msisubiri uchaguzi, hapo ndipo mnatoka kutudanya katika mitaani.
Chukuni hatua ya haraka kusuluhisha jambo hili.
Cc: Waziri wa Maji & Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Pia soma > KERO - Idara ya Maji Nyegezi Mwanza (MWAUWASA) jitafakarini suala la ukosefu wa maji