Mwendelezo wa kesi ya Dkt. Slaa Mahakama Kuu, leo Januari 24, 2025, Wakili Madeleka ataka Mahakama ifute kesi

Mwendelezo wa kesi ya Dkt. Slaa Mahakama Kuu, leo Januari 24, 2025, Wakili Madeleka ataka Mahakama ifute kesi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam leo, Ijumaa Januari 24.2025 shauri lililofunguliwa Mahakamani hapo na Mwanaharakati Dkt. Willbroad Slaa dhidi ya Jamhuri, akiiomba Mahakama hiyo kufuta kesi ya jinai aliyofunguliwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Ameeleza kuwa ni kutokana na kile anachodai kuwa kesi hiyo haijakidhi matakwa ya kisheria na Kikatiba, limesikilizwa Mawakili wa Dkt. Slaa wakiongozwa na Peter Madeleka, Hekima Mwasipu, Mwanaisha Mndeme, Edson Kilatu, Paul Kisabo na wengineo wameieleza Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam ni kwa namna gani mteja wao amekuwa akisota rumande kwa muda mrefu bila kupatiwa dhamana.

Huku wakitumia jukwaa hilo kueleza wasiwasi wao kwamba huenda 'danadana' zinazoendelea kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zina 'maelekezo'.

Video: Jambo TV
Soma: Pre GE2025 - VIDEO: Dkt. Slaa ndani ya Kizimba cha Mahakama Kuu, akikabiliwa na kesi ya kusambaza taarifa za Uongo mtandaoni
 
Dah!!! Huyu mzee wamuonee huruma sasa!
Mwanzoni niliotabuta ni ila naanza kumwonea huruma mzee huyu, CCM ukila hela zao afu ukawageuka ni wabayaa!!
Pole sana Balozi wa Sweeden.
 
Tunataka utawala unaofuata sheria na sio utawala wa visasi.
 
Kwa mliokaa jela naomba kuuliza hivi mzee kama huyu nae anachuchumalishwa pal getini kuingia gerezani? Na je naye anavulishwa nguo na kuinama kuangaliwa kama ameficha kitu makalioni?
 
Back
Top Bottom