upupu255
Senior Member
- Sep 4, 2024
- 119
- 144
Mkoa wa Pwani umeteuliwa kuwa mwenyeji wa shughuli ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zitakazozinduliwa Aprili 2, mwaka huu katika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Pwani sherehe zitakazohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa, mikoa jirani na wilaya zote za Mkoa wa Pwani pamoja na wananchi.
Kauli mbiu ya Mwenge mwaka huu ni "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa Amani na Utulivu" ikihimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi kwa utulivu, mshikamano na uzalendo ili kudumisha amani na maendeleo ya taifa kwa ujumla na wakimbiza Mwenge watatoa ujumbe unaombatana na kauli mbiu hiyo.
"Hii ni fursa kubwa kwetu sote wana-Pwani, uzinduzi huu ni chachu ya maendeleo ya mkoa wetu na hasa katika suala la kiuchumi kama vile huduma za malazi, chakula, usafiri, vinywaji, utalii na mengineyo mengi. Nawaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo," amesema Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Alhaji Abubakar Kunenge.
Kunenge amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika halmashauri zote tisa za mkoa ambapo utakagua, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Kauli mbiu ya Mwenge mwaka huu ni "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa Amani na Utulivu" ikihimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi kwa utulivu, mshikamano na uzalendo ili kudumisha amani na maendeleo ya taifa kwa ujumla na wakimbiza Mwenge watatoa ujumbe unaombatana na kauli mbiu hiyo.
"Hii ni fursa kubwa kwetu sote wana-Pwani, uzinduzi huu ni chachu ya maendeleo ya mkoa wetu na hasa katika suala la kiuchumi kama vile huduma za malazi, chakula, usafiri, vinywaji, utalii na mengineyo mengi. Nawaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo," amesema Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Alhaji Abubakar Kunenge.
Kunenge amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika halmashauri zote tisa za mkoa ambapo utakagua, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.