Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MWENGE WA UHURU MUSOMA VIJIJINI: MIRADI YA THAMANI YA TSH 3.5 BILIONI YAKAGULIWA NA KUKUBALIKA
Mwenge wa Uhuru ulipokelewa kwa shangwe nyingi mno kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC) yenye Jimbo la Musoma Vijijini. Hiyo ilikuwa juzi, Jumatano, 31.7.2024
Miradi yote 7 ilikaguliwa na kukubalika. Miradi hiyo ni ya ujenzi wa shule (miradi 2), zahanati, na barabara. Mingine ni ya usambazaji wa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria (miradi 2) na kikundi cha vijana (uchumi).
Wananchi wa Musoma Vijijini walitoa shukrani nyingi za dhati kwa Serikali yetu inayoongozwa vizuri na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Tafadhali sikiliza VIDEO/CLIP iliyoambatanishwa hapa.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Tarehe:
Ijumaa, 2.8.2024