Mwenge wabaini ufisadi wa TZS 65B kwenye miradi 49 ya halmashauri 38 Je, nini kitaendelea?

Kukimbiza huo moto ni upotevu wa muda, pesa, nguvu na kuongeza maambukiza ya ukimwi
 
Napongeza kilichoandikwa,

Mungu mbariki Rais Samia
 
Kwani CAG hakupita mwaka jana?

Kwani Mwenge ndio utambue huo ubadhilifu?
Hebu naomba uniambie mwenge kama mwenge na shughuli zake vinafanyaje fanyaje katika kuvumbua au kukamata uhalifu na ubadhirifu wa fedha na mali za uma?!

Maana me naona mnachofanya ni kupamba kwa maneno kittu ambacho ni wazi kwasasa kimeshamaliza maudhui yake na kimebakia kama kificho cha upigaji wa pesa nyuma ya pazia.

Shughuli za mwenge zinatakiwa zifike tamati. Tuandae hafla maalumu hapo dodoma ili mwenge ukabidhishwe kwa uongozi wa makumbusho ukachongewe shelfu basi.

Anaetaka kumulikwa na mwenge aende pale alipe kiingilia apewe na kiberiti awashe um'mulikeeee weeeeeee kisha arudi home kwa raha zake.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Ule mwenge Kuna jambo si bure, ukute kuna matambiko ya kufa mtu, kama unaamini kwenye uchawi huna budi kuamini kwenye Mwenge...
Sina uhakika lakini, haiwezekani watu watumie gharama kiasi hiko...
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
Ule mwenge Kuna jambo si bure, ukute kuna matambiko ya kufa mtu, kama unaamini kwenye uchawi huna budi kuamini kwenye Mwenge...
Sina uhakika lakini, haiwezekani watu watumie gharama kiasi hiko...
Uoga tu. Ndio maana na wao wanajua mwisho wao unakaribia wanakuja na visababu vya kipuuzi kama hivyo eti kumulika mafisadi sijui nini na nini?!

Wewe koroboi inamulika vipi mafisadi. Wanachofanya ni kuupotezea heshima yake kwa kizazi kipya sababu wanashangaa kitu cha kihistoria hadi leo bado kipo tu kwenye shughuli za kiserikali kina umuhimu gani?!
 
Wewe waulize tu faida za Mwenge ni zipi?
 
Ninapoandika kwamba wewe ni "kiazi", kamwe sikuonei hata kidogo. Wewe ni 'Kiazi' hasa!

Kwa hiyo wewe unaona hii ndiyo kazi muhimu ya mwenge? Hao walioajiriwa kufanya kazi hiyo wewe unadhani hawana uwezo wa kuifanya kwa ufanisi zaidi kuliko mazingaombwe hayo unayoshangilia hapa?

Sema basi, kwa vile kuna mwenge, fanya huo mwenge urejeshe hiyo pesa unayosema imeliwa.

Yaani unataka kusema hujui taratibu za kufanya kazi serikalini? Walioko huko wameshindwa nini kufanya kazi hizo kwa ufanisi!

Ngoja niachane na wewe, mwishowe nami nitaonekana kuwa mpuuzi kujibishana na mtu kama wewe.
 
Wakimbiza mwenge ambao sio wataalam,technocrats wanapotumika kama ofisi ya CAG,ni kupoteza muda tu.
 
Mwenge ni kitu gani tena.
 


Amelifanyia mengi mno na mazuri sana taifa letu

Aendelee kupumzika kwa amani baba wa taifa Julius Kambarage Nyerere


EDIA=youtube]eGh8RK-y0t0[/MEDIA]
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Ule mwenge Kuna jambo si bure, ukute kuna matambiko ya kufa mtu, kama unaamini kwenye uchawi huna budi kuamini kwenye Mwenge...
Sina uhakika lakini, haiwezekani watu watumie gharama kiasi hiko...
Kipindi nasoma shule ya msingi 1967 sasa nimestaafu. babu aliniambia.Ukiona watu wengi wanakimbiza kijinga cha moto, kaa mbali nao wala usikitazame utakuwa mjinga.Kwa tafsiri ya dini yetu ni kuabudu miungu mingine wakati tayari tuna Mungu tunayemuamini.Ni kweli ni hivyo.Hakuna tafsiri nyingine.Kama ipo, weka hapa.

Mpaka leo ninaendelea kuamini hivyo.Hivi kweli inakuingia akilini mtu na elimu ya Phd. Anakimbiza kibatari kinachowaka tena mchana kweupe tena anakiimbia na kukisifia.(ngoma kwa mganga wa kienyeji usiku)

Kuna mtawala mmoja Mtanzania kweli kweli alikipiga marufuku akakifungia kabatini.Nilitamani akifukie kabisa ardhini. Lakini naona kimefufuliwa tena.Ila kwa sasa naona kama kuendelea na hili ni sawasawa na kuipeleka Tanzania kwa mganga wa kienyeji mchana kweupe bila aibu.

Nadhani hii ni mitambiko ya hicho chama.Ndiyo maana wapo mbelembele sana kukimbiza hicho kibatari.Mimi hata kukitazama kwenye picha mwili unanisisimka.Ni sawa na kukutana na shetani mchana kweupe uso kwa uso.

Hizo fedha zooote zinazotumika zinatokana na matozo tunayokatwa kila mahali, Tulishakataa kuchangia.sasa wanazichukua kwa nguvu.Tena walisema ni za maendeleo.Leo nakatwa hapa Mtwara,wanajengewa zahanati Mkwajuni, Mbamba,Kisekela.Kwa nini kama hapa Mtwara nimetozwa 500,000/- kwanini zisijenge barabara hapa kwetu Mtwara na badala yake zinapelekwa Zanzibar kuwaletea maendeleo wapate umeme wao,sisi tuliotozwa tubaki gizani.Its not fair.

Hasara za hiki kibatari ni nyingi kuliko faida zake.Fanyeni utafiti.Hapa tunadanganyana eti umegundua ubadhirifu katika miradi ya maendeleo, kumbe huo mwenge ndio unaobadhirifu na unatakiwa kuchunguzwa.Unavunja sheria kwa kumkamata aliyefuata sheria kwa mujibu wa katiba.Mambo ni mengi.

Wapo wahusika wenye utaalamu wa mahesabu ya miradi, wapo wakaguzi chini ya CAG au Controlar And Auditor General. Wa serikali, wewe kibatari usiye na utaalamu wowote hujafanya utafiti wowote,kwa kuwa umeona tu msimamizi wa ule mradi mnatofautiana na kwa sababu upo nyuma ya hicho kibatari unaropoka tu kuna ubadirifu.Kila taasisi ina kazi yake.Wewe umeamua kukikimbiza kibatari ongeza kasi.

Otherwise, hizo taasisi zooote za ukaguzi wa hesabu za serikali zifutwe ili hiyo nafasi kibatari kibebe.Ila wanajaribu kulazimisha kwa kutoa taarifa zisizothibitishwa. ili kibatari kiendelee kuwepo.Kama ni kweli muda wote kilikuwa wapi mpaka hayo yote yatokee.
 
Mwenye ni development stimulus mkuu

Kama umefanya kazi serikalini utaelewa hili
Mwenge unamwilika mafisadi kila kona
Unaleta umoja na amani ya nchi ndio maana" unasalamu ya Utii"

Mwenge bado unahitaji sana kuliko unavyotuhitaji
 
Ni ngumu mtu kuhonga timu nzima Ya mwenge ili ufisadi wake upitishwe ila nirahisi kufanya hivyo kwa mkaguzi mmoja toka kwa CAG,

KUHUSU IMANI NCHI HAINA DINI ILA MIMI NA WEWE MZEE WANGU TUNADINI ZETU
 
Amelifanyia mengi mno na mazuri sana taifa letu

Aendelee kupumzika kwa amani baba wa taifa Julius Kambarage Nyerere


EDIA=youtube]eGh8RK-y0t0[/MEDIA]
Hakika mzee wetu na wenzake our beloved Dk Mkapa na Dk Magufuli
 

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…