Elections 2010 mwenye akili na apime

chakubanga

Member
Joined
Dec 27, 2006
Posts
6
Reaction score
2
Zamani, mababu zetu kabla ya kwenda kuposa, walikuwa wanafanya uchunguzi wa binti, familia yake na tabia zake. cha msingi walikuwa wanaangalia kama kwao huko kuna matatizo ya wizi wizi ,umbeya, gubu , uwezo wa kuzaa nkZ Wakiridhika posa inapelekwa na taratibu zingine zinafuatilia.

Nimekuwa nikifuatilia mazungmzo kadha wa kadha kuhusu uchaguzi wa mwaka huu.
Watu wamekuwa wakipayuka payuka kama vuvuzela. mabishano yao na majibu yake yamekuwa sasa kuhusu watu na sio sera, kuhusu ubinafsi kuliko utaifa n.k.

hii inaonyesha jinsi kama taifa tulivyofilisika. Tunaona mshindi ni yule ambaye atapiga kelele sana au atatumia mapesa mengi.

Nafikiri kwa wenye akili uchaguzi huu sio tu nani anashinda ila ni mkabala la taifa letu kwenda karne zijazo .Watanzania tukumbuke tunataka toa posa, tuchunguze , tuangalie na tuchague kwa hekima. Hatutapata mtakatifu ila tupate kiongozi ambaye atalipa taifa tumaini,mabadiliko, kuwezesha na kuboresha mifumo ya uongozi kwa ajili ya wote.

Ili kuliangalia suala la nani anafaa kutuongoza, tunahitaji mgombea anayejua mambo haya matatu,
  • kwanza: anayajua matatizo ya Tanzania ya leo vizuri?
  • Pili; Sera za chama zake zinatatatua matatizo haya in a SMART(specific, measurable, achiavable, Realistic and Timely) way na binafsi ana uono (vision) ya uongozi?
  • Tatu : anaaminika ? amefanya vitu huku nyuma vinanvyotufanya tumwamini ? au naye vuvuzela tu ?


my 2 pence
 
"Fools talk, cowards are silent, wise men listen."
— Carlos Ruiz Zafón (The Shadow of the Wind)
 
"Fools talk, cowards are silent, wise men listen."
- Carlos Ruiz Zafón (The Shadow of the Wind)

Karibu Chakubanga.

Naona umejizatiti na mkakati wa kufunda tu kama kungwi ....au ni ID ya nyongeza!!
 
Asante kwa post 'dogo' karibu kwenye JF. Umeanza vizuri, Big Up!
 

Tushajuwa juwa ueolekeo wako ... Kwani mimi nina akili alafu nishapima .. Tuimia ID yako ya kawaida tu ya siku zote:becky:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…