Mwenye Copy ya Barua ya POSA

Mmoja ajitolee jameni kuandika hapa.

Walio oa tiyar plz. Ili tusijaze Saver bila barua.
GENTAMYCINE
 
Tulipokuwa chuo kuna kitu tulikuwa tunaita kibomu (kikaratasi kidogo chenye majibu unaingia nacho kwenye mtihani).... Nimecheka kidogo maana nimeona kama jamaa anataka kibomu ya barua ya posa..... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Reactions: a45
Tulipokuwa chuo kuna kitu tulikuwa tunaita kibomu (kikaratasi kidogo chenye majibu unaingia nacho kwenye mtihani).... Nimecheka kidogo maana nimeona kama jamaa anataka kibomu ya barua ya posa..... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
hahaha..
 
Ngoja tuitunge hapa hapa live!

Kwa familia ya Bwana na Bibi XYZ.
Ninayofuraha kuwaandikia barua hii nikileta maombi ya kumposa binti yenu ABC XYZ.
Hili limekuja baada ya jitihadi za muda mrefu za kutafuta mwenza wa maisha. Baada ya zoezi hili kukwama kwa kutumia nguvu zangu mwenyewe, nilionelea vyema kumshirikisha mwenyezi Mungu kwa njia ya sala na maombi. Na hatimaye Mungu amesikia maombi yangu na kunikutanisha na binti yenu huyu.
Katika kipindi ambacho tumefahamiana, tumeweza kushirikana na kusaidiana katika mambo mbali mbali ya kiuchumi, kijamii na kadhalika na tumeona tunapofanya mambo haya kwa pamoja tunakuwa na baraka tele na mafanikio.
Tumeweza kutatuta changamoto ndogo ndogo zinazotukabili kwa kuunganisha nguvu zetu. Kwa kweli kiwango cha urafiki wetu kimekuwa cha hali ya juu kiasa kwamba tunaona hatuwezi kuishi mbali mbali na hivyo kuonelea vyema kufunga ndoa takatifu ili tuweze kuishi pamoja katika maisha ya shida na raha, ugonjwa na uzima na hadi hapo kifo kitakapotutenganisha.
Hivyo ninaleta ombi langu mnipokee kama mtoto wenu na kunipa baraka zenu katika kumposa binti yenu na hatimaye kufunga naye ndoa siku za hivi karibuni.
Basi mtakapoitikia wito huu ninaomba kujulishwa taratibu za kufuata ikiwa ni pamoja na kupangiwa kiwango cha mahari ili niweze kuzikamilisha taratibu hizo panapo majaaliwa!

Wenu

DDA
 
Hii inamaanisha ulishaanza "kum'bomoa" binti wa watu kabla alooo!!
 
Afadhali umetoa mwongozo mkuu!
 
nimepata mwongozo Mkuu
 
Umetisha mkuu,
 
unatoa posa laki 8 kuowa mwanamke wakati aliyemtoa bikra alipiga mzigo kwa buku. .
 
Hahahaha lol umenikumbusha aisee wakati naenda kumposa wife ukiandika mkuu ambatanisha na kiasi chochote cha fedha mie niliweka 50k tukakaribishwa gonga vyuku kwa sana nini sahv we are happily married and blessed with one beautiful girl called praise
Bado unaishi na mke wako?

Watoto mmefikisha wangapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…