Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,176
- Thread starter
-
- #41
Acha chuki binafsi ndugu lete data kumdiscredit badala kulazimisha JK akusikilize au mzee unampigia debe mtu wako nini ashike nafasi yake?
vigezo viliwekwa na kutangazwa, kama hukutimiza isiwe nongwa. Hata sisi mitaani hatugombei kwa kuwa baadhi ya vigezo hatunavyo. Uongozi sio kitu cha kukimbilia. Kuana nini huko?
kama kuna kampuni inaongoza kwa ku-hire na ku-fire mameneja, hakuna nyingine. ni hii ya mawe ma3. muulizeni kati ya 2000 na 2010 kaajiri mameneja wangapi? ana kauli mbiu yake: "we can hire anybody by any cost". hii ni kauli ya kinyanyasaji. unyanyasaji kwa kuwa yeye ana pesa. anataka watu wafunge midomo. wasidai haki. huyu mzee bwana, dah!
siyo kiongozi wa kustahili kupewa uwaziri.
hapo ninadiriki kumkosoa JK nikiwa kifua mbele.
JK inabidi anisikilize. kama alivyosikiliza maoni ya wadau. akamtosa mama meghji ishu ya uwaziri. licha ya kumbatiza jina la 'mwanamke chuma'. hata mimi ni mdau. JK nisikilize.
Kilicho fanyika ni kuwafanyia HILA NA UDHALIMU wanawake wa kutoka kanda zingine. Hivi inakuwaje mtu kama Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA, ambae ana sifa za kuwa kwenye cheo hicho kikubwa kutuambia eti alikosa sifa za kuwa mbunge wa viti maalum ndio maana hakuchaguliwa, hii inaingia akilini kweli ? Kwa mwendo huu wa UKABILA, UDINI, UKANDA etc CHADEMA hakina muda mrefu kitabaki kuwa historia aisee.
Huna kitu bana JERUSALEM , JK hawezi kukusikiliza maneno yako haya ya kubomoa bana !
sibomoi.
ninamuomba JK azibe ufa. mawe ma3 ni ufa. Asipoziba(JK) ufa atajenga ukuta.
mimi ni mzalendo. hoja yangu ni ya kizalendo. ina mashiko.
ninapigania haki. wapo watu walipaswa kupewa hiyo wizara. siyo mawe ma3.
data nilizonazo ndiyo hizo. huu ni ushuhuda.
ushuhuda huwa hauhusishi makaratasi wala mihuri.
ni mtu kuzungumza kweli kama kweli ya Mungu.
Hivyo ndivyo ninavyomfahamu huyu kiumbe anayeitwa mawe ma3.
Aliyemshinda kura za maoni alizidiwa dau tu. nasikitika kwanini hakuenguliwa na NEC kama alivyofanyiwa mwakalebela.
watu wa jimboni kwake hawampendi. wanapenda pesa zake. sasa itakula kwao. 5 years.
Mkuu sasa naona unakoelekea siko unataka kutuambia tuyaamini maneno yako kwavile umeapa kwa mungu. Usinichekeshe watu wanaapa mbele ya pilato na wanasema uongo mbele ya hakimu sembuse wewe unayetaka kutuaminisha mbele ya mungu. Mie nakuachieni na umbeya wenu nilikuwapo
Nakumbuka sana. JK wakati anaanza kuitwa Rais (kwa sifa na majivuno, si kwa utendaji) alijigamba serikali yake 'haina ubia na mtu'. akaendelea zaid kusema ufike wakati wa 'kutenganisha biashara na siasa'
Sass huyu JK? Vipi?
Mbona Kitwanga aka Mawe Matatu ni mfanya biashara? Mbona amempa uwaziri? Au ndiyo kupozana? Kwa sababu 2005 alimwagwa kwenye kura za maoni?
Eeeh? Nauliza.
JK huyuhuyu hivi majuzi alikuja na staili ya kuwa atatuchagulia mawaziri 'waadilif na wachapakazi'. Vipi? Mbona Kitwanga siyo muadilifu? Mtu aliyevuruga kampuni aliyoanzisha na wenzake anafaa vipi kuwaongoza WaTz? Amesababisha kampuni kupoteza ma-Engineer na kupoteza wateja wakubwa kama NMB? Amesababisha mmoja wa wakrugenzi walioanzisha kampuni kujitoa licha ya mkurugenzi huyo kusaidia kupiga debe k=kampuni kupewa hadhi ya kuwa wakala wa DELL Tanzania? Kama ameshindwa kuongoza kampuni ya watu wasiozidi 100 ataweza Wizara inayotazamwa na WaTz 4 000 000?
Kama kuna uteuzi wenye utata uliofanywa na JK ni huu wa kumpa Kitwanga wizara. Ni urafiki na kujuana tu. Amempa ili iwe rahisi kupata tenda za kuuza computer za DELL kwenye taasisi za serikali....siasa na biashara damdam.
Hapo tu huwa simuamini JK.
Ni mtu wa hongo.
mtu wa mlungula
mtu wa kitu kidogo
alikuwa mwenyekiti wa ERB pamoja na kwamba kampuni yake ametimua wahandisi wote wenye akili na uwezo.
alikuwa mwenyekiti wa ERB lakini muda wote kulikuwa na hadithi za kweli za maghorofa kuvunjika. yeye ilimradi umpe kitu kidogo poa tu. hata ujenge ghorofa kwa nondo za fito au kwa matope poa tu.
Tz tumekwisha.
KUNA WAKATI AZANI BANK ILIBIDI KUWEKWA CHINI YA BOT NAHISI NDIO AKINA SINGILI WAKAPELEKWA PALE KUSIAMIA KAMA WAFANYAKZI WA BOT. HIVI NI BENKI BINAFSI KAMA UNAVYOSEMA?Anarudi tena, hivi uadilifu wa mtu unapimwa kwa umasikini?.
Infosys ni moja ya makampuni yenye mafanikio makubwa kutokana na kuwa ndio sole agent wa Dell, na miradi yote inayofadhiliwa na Benki ya Dunia, computers lazima ziwe Dell.
Nijuavyo mimi, Kitangwa ni mmoja wa wakurugenzi, yeye ni mwajiriwa wa BOT. Kaka yake ni Singili mwenye Azania Bank, jamaa wana mafanikio sana kwenye kila wanapokanyaga, hebu angalieni lile jengo lao pale Msasani Beach lilivyo kivutia!.
Hakuna ubishi, Tanzania ni nchi masikini, na Watanzania wengi tunaishi kwa lindi la umasikini uliotopea, hii isitufanye kijenga chuki na kila mwenye nacho, simply because wengine hatuna.
Naamini mafanikio ya Infosys sasa yanahamishiwa pale wizarani.
wandugu kuna tofauti kati ya infosys na infotech. Jengo la infosys (infosys house) lipo kinondoni nyuma ya makao makuu ya stanbic bank, ni jengo nzuri sana, part of it, imekodishwa na nbc kitengo cha corporate. Binafsi nimeifahamu infosys tangu mwaka 2000 wakiwa jengo lililopo nyuma ya steers along samora evenue.
Mawe 3 ndiye managing partner wa infosys. Ni mchapakazi hodari na hana mzaha kwenye kazi. Kwanza nawapa hongera infosys kwa mafanikio yao kibiashara. Kama mnavyojua kampuni nyingi kubwa za it hapa bongo zinamilikiwa na wahindi. Wahindi wanachojua ni kuuza tuu, after sales support is zero!!, wanashinda tenda sababu wanauza kwa bei rahisi then ukipata matatizo hawajali.
Nafahamu matatizo yapo infosys lakini ni ya kawaida na hatuna budi kuwaunga mkono.
wandugu kuna tofauti kati ya infosys na infotech. Jengo la infosys (infosys house) lipo kinondoni nyuma ya makao makuu ya stanbic bank, ni jengo nzuri sana, part of it, imekodishwa na nbc kitengo cha corporate. binafsi nimeifahamu infosys tangu mwaka 2000 wakiwa jengo lililopo nyuma ya steers along samora evenue.
mawe 3 ndiye managing partner wa infosys. Ni mchapakazi hodari na hana mzaha kwenye kazi. Kwanza nawapa hongera infosys kwa mafanikio yao kibiashara. Kama mnavyojua kampuni nyingi kubwa za it hapa bongo zinamilikiwa na wahindi. Wahindi wanachojua ni kuuza tuu, after sales support is zero!!, wanashinda tenda sababu wanauza kwa bei rahisi then ukipata matatizo hawajali.
Nafahamu matatizo yapo infosys lakini ni ya kawaida na hatuna budi kuwaunga mkono.
binafsi sina matatizo yoyote na infosys especially if it is run by mzalendo. Hofu yangu ni kwanini kuacha biashara na kuingia katika siasa? Je ni kwa nia ya kuwasaidia wanyonge au kutuia nafasi yake ii kupata biashara zaidi. Time will tell sio vyema kumhukumu mtu.
angalau infosis all the time wamekuwa wakiajiri wazalendo na kutengeneza ajira lukuki kwa vijana. Leta give a him a chance. Mbona akina el, chenge and others ambao hawajafanya lolote la maan zaidi ya kutuibia walipata chance? Maybe wzalendo millionaires can make a difference in the government in terms of grand corrption kwa kuwa tayari wao wanazo wanataka kuwasaidi wengine/
mawe 3 ni moja ya partners hapo Infosys, nadhani jumla ya wamiliki ni wanne. Hata Masha ni Partners wa IMMMA na jumla ya wamiliki ni 4 na sasa amerudi IMMMA baada ya kuanguka siasa. Tukumbuke kuwa mawe 3 pamoja na kwamba ni mmoja wa wamiliki wa Infosys bado alikuwa mfanyakazi wa BOT. I can see your concern lakini naamini hata akiwa waziri influence yake haitamsaidia sana kushinda tenders za serikali sababu kuna proper procedures za tender na kama Infosys itashinda tender za wizara anayoiongoza ni rahisi kuwashitaki PPRA due to conflict of interest
Binafsi nakuona una matatizo ya msingi au utakuwa umetumwa kuja kuchafua watu ndani JF. Ushauri wa bure epukana na utumwa au kama panga liliwahi kukupitia anga zake basi tulia anza upya na usonge mbele, maana hii mada yako ipo wazi sana na inaonyesha umetumwa haswa, GREAT THINKERS wenzangu wameshakublast ulete data lakini huwaelewi, sidhani hata kama shule yako inakusaidia.
Na naomba wana JF wasikubali kupoteza mda kudiscuss upupu wa mtu aliyetumwaw. Hayo ndo maoni yangu.
alikuwa mwenyekiti wa ERB lini mkuu?
ninachojua wenyeviti wa ERB miaka ya hivi karibuni ni maprof wa UDsm ie. prof Masuha,Prof Mwamila,Prof Ninatubu Lema yeye alishika kipindi gani?