Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Watanzania tuna safari ndefu sana kufikia maendeleo ya fikra; majaji waliohusika katika hukumu hii wamefanya mambo mepesi kuwa magumu. Wameandika maamuzi yaliyojaa maneno ya kiingereza magumu bila hata sababu ya msingi.
Nikisoma hii hukumu nabaini hata maneno baadhi yaliyoandikwa wao wenyewe hawawezi kuyatamka... ukiwaalika kwenye mdahalo wa kiingereza, hiyo lugha uwezo kuwasikia wakiitoa, inaonekana wamecopy maneno ya kiingereza magumu na kuyaweka kwenye maamuzi kuonyesha wamefanya kazi kubwa.
Hizi aina za uandishi zilikuwa zamani, enzi za wasomi wachache ukitaka kuonekana unajua zaidi kiingereza. Nowadays mambo yameboreshwa, watu wanataka facts, siyo bombastics, kama vile tupo kwenye mashindano ya insha.
Niwatake majaji wetu wawe real, waache kucopy kila kilichokuwa kinafanyika na ancestors wetu...
Lakini pia, principally pale unapojadili rasilimali za nchi kwenye ngazi ya mahakama kuu, unategemea pia majaji wafanye research, siyo kukumbatia walicholetewa mezani. Majaji wanaposema wameletewa mikataba au makubaliano ya kimataifa, ina maana wanashindwa kuelewa wapo ngazi gani... wao walikuwa na nafasi ya kuverify hoja kwa misingi ya kilichowasilishwa na ambacho kijawasilishwa mbele yao, ila kipo applicable duniani... kwamba Dubai ni nchi, hizi siyo hoja ambazo majaji walipaswa kuziacha zinaelea? Kwamba kama siyo nchi, kwanini anayeingia mikataba pia siyo Mfalme au waziri, bali ni mkurugenzi wa kampuni, walipaswa kuja na facts.
Kuja na porojo za kufungwa mikono, zinasaidiaje kulinda rasilimali za nchi? Kama bunge linapitisha sheria na mahakama inatafsiri... unapodhani sheria zimevunjwa, kwanini ujipe nafasi ya kupima pia ukubwa wa uvunjwaji wa sheria? Wapi pameandikwa kwamba uvunjwaji mdogo unavumilika? Je, kama sheria zilivunjwa, ni njia gani itatumika kurekebisha hayo mapungufu, au ndio kusema tunakwenda kubadili sheria ziendane na matakwa ya huu mkataba?
Je, yakifanyika mabadiliko ya sheria, sasa taratibu makosa ya mikataba ya nyuma?
Nikisoma hii hukumu nabaini hata maneno baadhi yaliyoandikwa wao wenyewe hawawezi kuyatamka... ukiwaalika kwenye mdahalo wa kiingereza, hiyo lugha uwezo kuwasikia wakiitoa, inaonekana wamecopy maneno ya kiingereza magumu na kuyaweka kwenye maamuzi kuonyesha wamefanya kazi kubwa.
Hizi aina za uandishi zilikuwa zamani, enzi za wasomi wachache ukitaka kuonekana unajua zaidi kiingereza. Nowadays mambo yameboreshwa, watu wanataka facts, siyo bombastics, kama vile tupo kwenye mashindano ya insha.
Niwatake majaji wetu wawe real, waache kucopy kila kilichokuwa kinafanyika na ancestors wetu...
Lakini pia, principally pale unapojadili rasilimali za nchi kwenye ngazi ya mahakama kuu, unategemea pia majaji wafanye research, siyo kukumbatia walicholetewa mezani. Majaji wanaposema wameletewa mikataba au makubaliano ya kimataifa, ina maana wanashindwa kuelewa wapo ngazi gani... wao walikuwa na nafasi ya kuverify hoja kwa misingi ya kilichowasilishwa na ambacho kijawasilishwa mbele yao, ila kipo applicable duniani... kwamba Dubai ni nchi, hizi siyo hoja ambazo majaji walipaswa kuziacha zinaelea? Kwamba kama siyo nchi, kwanini anayeingia mikataba pia siyo Mfalme au waziri, bali ni mkurugenzi wa kampuni, walipaswa kuja na facts.
Kuja na porojo za kufungwa mikono, zinasaidiaje kulinda rasilimali za nchi? Kama bunge linapitisha sheria na mahakama inatafsiri... unapodhani sheria zimevunjwa, kwanini ujipe nafasi ya kupima pia ukubwa wa uvunjwaji wa sheria? Wapi pameandikwa kwamba uvunjwaji mdogo unavumilika? Je, kama sheria zilivunjwa, ni njia gani itatumika kurekebisha hayo mapungufu, au ndio kusema tunakwenda kubadili sheria ziendane na matakwa ya huu mkataba?
Je, yakifanyika mabadiliko ya sheria, sasa taratibu makosa ya mikataba ya nyuma?