kwa uelewa wangu mdogo wa masuala ya sharia or sorry sheria kuna kitu kinaitwa expert evidence hii ni aina ya ushahidi inayotolewa na mtu mwenye mafunzo maalum ya fani husika mfano daktari/ama ripoti ya daktari itahitajika kuthibitisha vina saba (dna) ndivyo hivyo pia kwenye uhalifu wa kimtandao kwa mwanasheria wa kawaida nachojua mimi jukumu lake kubwa ni kukusanya ushahidi ambao utakuwa una kubalika na sheria ya nchi husika (admissible) huko unapokwenda kwenye computer forensics hayo ni mambo ya IT kwa wewe mwanasheria ukipeleka hata ushahidi wa picha mahakamani lazima aitwe mtu mwenye taaluma yake athibitishie mahakama pasi na shaka lolote (beyond reasonable doubt) kwamba hiyo picha ni ya kupiga na wala siyo ya kutengeneza (photoshop), siku hizi kuna sahihi za kielektroniki kama imefojiwa inabidi pia mtu mwenye uelewa aithibitishie mahakama kwamba sahihi hiyo ni ya kufoji....mtazamo wangu kama unataka kujiendeleza unaweza uka specialize kwenye cyber laws kwa kuendelea kusoma lakini kama ni mwanasheria wa kawaida inabidi focus sana kwenye DEA yani digital evidence analysis .....pole kwa lugha za kigeni binafsi natokea kanda ya ziwa