Suip
JF-Expert Member
- Sep 21, 2010
- 1,353
- 815
Wataalam wa humu JF napenda kuomba msaada wenu, kuna mwanangu anasumbuliwa na ugonjwa wa kuota sugu katika unyayo wa mguu na hupata shida wakati wa kutembea akanyagapo ardhini hapo mahali hapo panauma sana.
Ukichokora ni kama ungaunga unatoka na ukiendelea kuchokora ndani zaidi hutoa damu, Iliota ya kwanza na baadaye ya pili. Hofu yangu ni kwamba bila kupatia tiba sugu hiyo itaenea unyayo wote na kumwia vigumu kutembea.
Nategemea kupata ushauri na tiba iwe ya kitaalamu au asilia.