Mwenye tatizo kuhusu magari

Ni vema uchangie na usaidie watu kuliko kuleta dharau.

Mimi hapa sipo kuhitaji hata shiling mia ya mtu, nipo kutoa kile kichopo akilini mwangu baada ya kuisomea hii taaluma. ,hivo kama kuna kitu changia sio kuanza KUVURUGA UZI

Haileti maana ,
achana nae, hukusema mtu asifanye engine diagnosis Bali ulichosema kabla hajakimbilia huko basi aangalia kwanza Gas cap! Huyo jamaa ni mpuuzi, yy alichotakiwa ni kuongezea kitu gani kifanyike na sio personal attacks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini kinachangia engine kuchelewa kuwaka? Yaani inachukua sekunde 20 na zaidi umeshikilia ufunguo kwenye start ndo inawaka hasa wakati wa asubuhi na usiku ikiwa imetulia muda mrefu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na hili wengi mafund wa mtaani hawalijui, zaidi wanabuni au wanahisi tatizo ni VVTI, Ila tatizo la CHECK ENGINE kuwaka huwa ni gas cap kuwa loose hivo hufanya mafuta ku evaporate,

Hivo badilisha kama kimeharibika
Hhahaaha pole sana mkuu unawaona mafundi wa mtaani kama hawajui wakati na wewe mwenyewe pia haujui.unahisi jibu lako ulilolitoa la gas cap ni sahihi wakati sio sahihi.

Hembu nishawishi kwa kutetea hoja yako kitaalam.

Mahusiano ya taa ya chek engine kuwaka na kusababishwa na gas cap.
 
J
Nini kinachangia engine kuchelewa kuwaka? Yaani inachukua sekunde 20 na zaidi umeshikilia ufunguo kwenye start ndo inawaka hasa wakati wa asubuhi na usiku ikiwa imetulia muda mrefu?

Sent using Jamii Forums mobile app
hembu fanya unyooshe maelezo ili upewe jibu sahihi.

Sema ni gari aina gani. Na linatumia engine aina gani.

Gari ya disel tofauti na ya petrol
 
Tatizo ni gas cap inaloose pia linaweza kuwa ktk catalyc conveter anza na hayo
Si kweli mkuu mashine imesema vvti wewe unasema mambo ya gas cap.

Ingekuwa gas cap ingeleta fault ya systerm too lean bank 1.

Yaani hapo bora hata ungenambia kuwa engine oil cap ungenishawishi .

Vvti huwa ina endana na oil.siku zote fault zake zote humalizana na oil.oil ikiwa ndogo,au mda wa service ukipita inasoma pia vvti au hata kama ukiwa umefanya service lkn engine ni chafu ina ukoko ndani.

Na hasa wabongo wanaweka sana oil za bei rahisi ndio shida yake.
 
Mkuu usibadili engine bali fanya ubadilishe mfumo tu hapo kutoka kwenye carburetor kwenda kwenye injection ni rahisi na garama itakuwa chini kidogo usawa wa anko magu huu nipe mm hilo dili
 
Upo sahihi sana mkuu.

Harafu kwa haraka nishamtambua kuwa huyu jamaa si fundi umeme hata masuala ya diagnosis bado hajayatambua vizuri sababu unaweza pima na mshine lkn usijue nn au ukabadikisha kiti ambacho sio tatizo.

Huyu ni fundi wakufanya service na kubadili brake pad tuu
 
Unamshambulia sana mleta mada utadhani anapokea malipo kwa ushauri anaoutoa,sidhani kama ni haki.

Toa maoni yako kuboresha alafu umwache aendelee na Uzi wake la na wewe anzisha wako. Kwanza sijui ulikuwa wapi kuanzisha uzi kama huu kama unahisi unaijua sana hiyo fani! @$

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aiseee wewe jamaa ni janga.aisee wewe katika hii fani sio mbobezi kama unavyosema achana na ma google yatakupoteza.

Kwenye gari kuna aina mbili kwanza shida za hard ware na softwere.

Shida za softwere solution yake kubwa ni diagnosis hapo utaluka weee ukipima umemaliza kila kitu..

Ukipata fault code kuna mara mbili inakwambia shida ni nn.so ukishindwa kulekebisha au kuelewa shida ni nn hapo tatizo ni ww fundi tatizo sio diagnosis..

Wengi huwa wanashindwa kuzielewa fault code vizuri ndio maana huwa wanakimbilia kubadilisha vitu.

Mfano maneno haya kwenye mashine range performance na manlfucture yana maana tofauti.
 
Hahhaahaha pole sana mkuu..kwahiyo anapokosea unataka watu wanyamaze..hivi ww ukiwa na gari yako ukakutana na fundi akakuingiza mkenge akitokea mtu anayefaham kuwa kakuingiza mkenge asikwambie.

Mm nipo.kwanza kwa fundi kukosolewa ni jambo zuri sana..yeye anaweza kuwa fundi mzuri sana zaidi yangu lkn sio kwa kila kitu.

Kwenye mfumo mmoja tuu wa umeme kwenye gari huwezi kubobea kwenye mfumo huo ukawa bora kwa mfumo mzima bali utakuwa mbobezi kwenye sehem flani ktk mfumo
 
Nina Honda Stream 2001 LA-RN3 ilianza kublink taa ya D, fundi ambaye amekuwa akiijali hii gari akasema kuna leakage kwa gearbox akashauri iwe welded nikamruhusu, akaifungua gearbox kafanya anavyojua kuirudishia mjapan kamgomea kwenda mbele wala nyuma. Akashauri gearbox imekufa mazima tununue nyengine! Hii iko sawa mtaalam? Au alikuwa akibahatisha ufungaji wake? Hii kitu no CVT. Nitarudi baada ya hili jibu mkuu ikibidi niulete huu mchuma ofisini kwako unisaidie zaidi
 
Mkuu habari. Shukrani kwa uzi huu. Gari yangu ni ist na inashida nikiendesha accelerator speed haizid 3 au 4 na ikizid zaid hapo kama unakanyaga mafuta sana inatoa mlio flani....kama pa.pa.pa.pa.pa..... na ukiwa unapanda mlima inakosa nguvu kiasi kwamba haizidi 30km/hr kilimlima chochote...yaaaani mwinuko wowote. Ni nini shida mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu.kabla ya yote ungetafuta mashine na ukaipima ingekupa jibu sahihi hapo ndio umhim wa mshine unapoonekana.

Honda ipo hivi gari ikiwa na shida yoyote kwenye transmission lazima taa ya D ita blink.
So ungepima ungepata jibu sahihi.

Kwakuwa mwanzo gari ilikuwa inatembea vizuri.basi hiyo gearbox sio mbovu bali fundi ndio kaitia ubovu hapo kuna vitu kashindwa kuvirudishia vizuri.inawezekana kuna seal za pressure kazi weka vibaya.
Au kafunga vibaya pump yake.

Kwa haraka fanya hivi kuna pipe mbili huwa zinaingia kwenye rejeta zichomoe then mwambie mtu awashe gari uone kama hydrolic inatoka kwa pressure kubwa kama hamna basi ni shida ya kwanza kama inatoka kwa pressure kuna vitu kakoroga.

Kama upo dar unaweza kunitafuta
 
Ina
Hapo ina maana ina piga back fire na back fire mara nyingi husababishwa na mafuta kidogo,au hewa chache kwa haraka na kuanzia fanya hivi,kwanza service ulifanya lini mara ya mwisho sio ya kumwaga oil na kubadili filter.

Bali kubadili plug na air filter?. Hapo cheki plug,air clener,fuel filter ukiona vyote viko powa basi chunguza catalic converter halijaziba .

Kama fuel filter chafu basi safisha na nozel pia
 
Habari mkuu,nina Teriors engine K 3,inatatizo,nikiwa kwenye foleni nimeweka drive D na kuanyaga brake gari inashuka silencer na kuzima.
Mpaka niweke P niwashe ndio niweze kuondoka.
Tatizo ni nini haswa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Asante mkuu nitakutafuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…