Mwenye uelewa wa maneno haya ya kiuchumi anisaidie

Umejitahidi kuelezea ila Kuna makosa kwenye maelezo yako.
Mfano neno liquidity.
Liquidity-ni hali ya kitu/mali kuweza kubadilishwa kwa pesa kiurahisi bila kuathiri thamani yake.
Mfano wa mali zenye liquidity-dhahabu,hisa.
Sure sure mkuu
 
Liquidity ni hali ya kuwa na vitu vinavyoweza kubadilishwa kwa urahisi na uharaka kuwa pesa ikiwemo pesa yenyewe mifani ni (1) pesa iliyopo mpesa, bank, kwenye mfuko (2).mzigo wa dukani (3) wadaiwa wenye uhakika wa kulipa pindi pesa itapohitajika (4)fidia ya ushuru (tax refunds)

Asset: hizi ni rasilimali za zinazomilikiwa na mtu, biashara au serikali, Kuna asset zinazoshikika na kuonekana kama majengo, mzigo, magari, mashine,n.k na kuna asset zisizoshikika kama hakimiliki,listi za wateja, uhusiano mzuri na wateja, software za komputa au simu.

Liability: kwa ligha nyepesi ni madeni yanayonyonya mali zako mfano madeni ya Benki, madeni ya watu waliokuuzia mzigo kwa mkopo, waranti za bidhaa ulizouza zinazoweza kufanya umbadilishie mteja bidhaa mpya, huduma ulizotumia ila bado hujazilipa, n.k

Equity; huu ni mtaji unaopatikana kwa njia ya kuuza hisa...kwa mfano kampuni ikiuza hisa moja kwa 200 na hisa milioni moja zikauzwa basi mtaji utakuwa ni milioni 200, wanunuzi wa hisa ndio wamiliiki, faida inayobaki baada ya kulipa ushuru na riba za madni itagawanywa na kupewa kwa wamiliki kulingana na asilimia za hisa wanazomiliki

Bonds - huu ni mtaji unaopatikana kwa mfumo wa mkopo, kampuni au serikali inaweza ikawa inahitaji kiasi fulani kwa hio itatoa hizi bondi kwa watu ambao watazinunua kwa makubaliano ya kwamba kila baada ya kipindi fulani kuna riba italipwa kwa walionunua hizi bondi na kurejeshewa pesa yao waliyonunulia bondi (ukiachana na riba) baada ya kipindi fulani....Wamiliki wa bondi hupewa kipaumbele cha kulipwa kabla ya wanaomiliki equity.

KWA HISANI YA MACHOZI YA SIMBA
-CPA (T)
-Bachelor of Accountancy (I.A.A - Arusha)
-Form six - E.C.A
 
❌❌ ❌

majibu sahihi yapo kwenye post namba 24
 
Umejitahidi kuelezea ila Kuna makosa kwenye maelezo yako.
Mfano neno liquidity.
Liquidity-ni hali ya kitu/mali kuweza kubadilishwa kwa pesa kiurahisi bila kuathiri thamani yake.
Mfano wa mali zenye liquidity-dhahabu,hisa.
Hata wewe umeijibu liquidity kwa limitation wakati ina maana tofauti,inategemea unazungumzia nini.kama ni kwenye assert,liability au financial market.
 
Toa maana zingine za neno liquidity ambazo unahisi hazitakuwa na limitations.
Nimesema inategemea unazungumzi nini.mfano kwenye assert liquidity ni kuwa na uwezo wa kulipa madeni kwa haraka/kutumia current assert,inamaana una cash ya kutosha na kwenye financial market inakuwa tofauti kama ulivyoelezea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…