Pre GE2025 Mwenyekiti CCM Taifa naomba uruhusu kuchapisha fomu nyingi za kugombea Urais ndani ya chama kukuza Demokrasia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2019
Posts
9,863
Reaction score
20,806
Nitofautiane na makada wenzangu kwenye swala Zima la desturi kuifanya sheria ndani ya chama!

Hatuna Cha kuogopa Wala kupoteza kwenye mchakato wa ndani wa kumpata mgombea mpya hapo 2025, ninaamini katika kudra za mwenyezimungu kuhusu hatma Yako ya urais wa 2025 -2030 kuliko kulazimisha kama makada wengi wanavyokushauri! kuchapisha fomu Moja ni uchuro kama wa mtangulizi wako alivyofanya, Mja mnyenyekevu ni yule anaethamini mchango wa wengine ndani ya chama kuliko kujiamini wewe ni Bora kuliko wengine!

Makosa aliyoyafanya Hayati Magufuli usiyarudie, yametuonyesha hatma mbaya kwa njia aliyokua ameichagua!!

Naamini hupendi Ile hatma ikatokea na ili kuibadili hatma lazima uanzishe njia mpya itakayoleta hatma Yako mpya kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025!

Ukichagua njia Ile ile aliyopita mtangulizi wako ni dhahiri asili itajitahidi kuleta hatma ile ile ambayo ilimpata mtangulizi wako!

Naandika haya kama mwanaccm mwenye akili timamu ninaeamini katika asili na matokeo yake juu ya Yale tuyafanyayo ndio huamua hatma yetu kama binadamu/waja wasioijua kesho!

Ruhusu mchakato ili asili ikusaidie kuiendea hatma Kwa amani kuliko kulazimisha hatma yako!

Naamini usiposoma wewe mwanao Abdul atasoma na kukusaidia kwenye maamuzi mazito yajayo!

Iache kudra na hatma Yako itegemee mwenyezi mungu na sio kibri na majivuno ambayo yatatuletea hatma isiyotarajiwa kama mtangulizi wako alivyofanya!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki mwenyekiti aweze kuona uhalisia na chawa wasiharibu focus ya kiuongozi!
 
We bwege waza mambo ya manyumbu wenzio, CCM ni next level kwako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…