Pre GE2025 Mwenyekiti UVCCM Geita, Manjale Magambo: Ukipigwa kwenye Kura za maoni usikimbie, baki ujenge Chama chetu

Pre GE2025 Mwenyekiti UVCCM Geita, Manjale Magambo: Ukipigwa kwenye Kura za maoni usikimbie, baki ujenge Chama chetu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Geita, Manjale Magambo, amewataka wanachama wa chama hicho kutokata tamaa au kununa pale wanaposhindwa kwenye kura za maoni.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Manjale amesema kuwa, kushindwa kwenye kura za maoni hakumaanishi mwisho wa safari, bali ni fursa ya kujitathmini na kuendelea kukijenga chama cha Mapinduzi.

Ametoa kauli hiyo akiwa katika Jimbo la Bukombe katika mwendelezo wa ziara ya kamati ya utekelezaji (UVCCM) ambapo amesisitiza kuwa, kuna baadhi ya watu wana tabia ya kutafuta njia ya kutokea pindi wanaposhindwa, lakini kwa wale walio na nia ya dhati ya kushiriki katika maendeleo ya chama, wanapaswa kubaki imara na kuendelea kujenga chama pamoja.

‘’Ukipigwa kwenye kura za maoni hakuna haja ya kununa, kuna watu wanatabia wakishapigwa kwenye kura za maoni wanatafuta mlango wa kutokea, ukipigwa baki humuhumu tukijenge chama chetu…acha mambo ya kununanuna unataka uwe wewe tu.

 
Back
Top Bottom