Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kagera, Ndg. Faris Buruhani, amewataka wananchi wa Kata ya Kibingo, Wilaya ya Kyerwa, kuacha tabia ya kuwachagua viongozi wa vyama vya upinzani na badala yake waendelee kuiunga mkono CCM.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM katika Ofisi ya Kijiji cha Rwenkende, Faris alisema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta mageuzi makubwa katika zao la kahawa kwa kupandisha bei yake kutoka Shilingi 1,200 hadi Shilingi 5,000. Alisisitiza kuwa ni muhimu kwa wananchi kuwa na shukrani kwa kumuunga mkono Rais kwa kura nyingi ifikapo uchaguzi mkuu.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM katika Ofisi ya Kijiji cha Rwenkende, Faris alisema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta mageuzi makubwa katika zao la kahawa kwa kupandisha bei yake kutoka Shilingi 1,200 hadi Shilingi 5,000. Alisisitiza kuwa ni muhimu kwa wananchi kuwa na shukrani kwa kumuunga mkono Rais kwa kura nyingi ifikapo uchaguzi mkuu.