Mwenyekiti wa CCJ, Richard Kiyabo avamiwa

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
302
MWENYEKITI wa Chama Cha Jamii (CCJ), Richard Kiyabo, amevamiwa na kuporwa mkoba uliokuwa na nyaraka za chama hicho kinachopigania usajili wa kudumu.
Kiyabo, anadaiwa kuwa alivamiwa na watu wanne wasiofahamika na kumpora mkoba wake uliokuwa na nyaraka mbalimbali za chama hicho kilichojizolea umaarufu katika kipindi kifupi.
Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa tatu asubuhi jijini Dar es Salaam katika maeneo ya Kariakoo, Mtaa wa Msimbazi, jirani na jengo la klabu ya soka ya Simba, ambapo Kiyabo alikuwa akitembea kwa miguu.
Baada ya tukio hilo, Kiyabo alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi na kupatiwa RB yenye namba MS/RB/3606/2010.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, mwenyekiti huyo alisema alishangazwa jinsi tukio hilo lilivyotokea, kwani lilifanywa kwa kushitukiza na watu hao waliokuwa katika gari dogo aina ya Toyota Cresta, ambalo hakuweza kutambua namba zake.
“Kwa kweli hadi sasa naona maisha yangu yamo hatarini… hii sasa ni mara ya pili kutokewa na tukio la aina hii, leo (juzi) asubuhi nikiwa Kariakoo nikifuatilia masuala ya chama, ghafla nilivamiwa na watu waliovalia makoti meusi na kupora briefcase yenye nyaraka mbalimbali za siri zinazohusu CCJ.
“Walionipora walisimamisha gari lao mbele yangu kidogo kisha wakatoka na kunishika mikono yangu, halafu wakairudisha nyuma, nilikuwa naongea na simu, mmoja wao akatoa kitambulisho chenye nembo ya serikali akanionyesha.
“Walipomaliza wakachukua begi langu wakaingia kwenye gari lao ambalo sikutambua namba zake, lakini niliona likiwa na vioo vya giza (tinted) wakaondoka zao… muda wote watu walikuwa wakipita wakiniangalia, lakini hawakunisaidia,” alisema Kiyabo.
Alibainisha kuwa kutokana na kushtukizwa na tukio hilo, hakuweza kuwatambua kwa sura watu walioshiriki uhalifu huo anaouhusisha na harakati za kisiasa, hasa kipindi hiki ambacho chama chake kimekuwa kikifuatilia usajili wa kudumu.
Alisema ingawa tukio hilo lilitokea mapema, lakini hakuna mpita njia aliyejitokeza kumsaidia zaidi ya kumuangalia huku wengine wakiendelea na shughuli zao.
Kwa mara ya kwanza, mwanzoni mwa Februari mwaka huu, Kiyabo alikumbana na vitisho vya kuuawa alivyopokea kwa njia ya simu kutoka kwa watu asiowafahamu, hali iliyomfanya kutoa taarifa polisi.
Muda mfupi baada ya kuvamiwa kwa mwenyekiti huyo wa muda, aliyekuwa Mbunge wa Kishapu kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Fred Mpendazoe, alikuwa kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) akieleza nia yake ya kukihama chama hicho kikongwe na kujiunga na CCJ. Tangu kuanzishwa kwake, CCJ imekuwa ikihusishwa na vigogo kadhaa wa CCM ambao baadhi yao wamekuwa wakikikana chama hicho ambacho katika kipindi kifupi kimeweza kuwa masikioni na machoni mwa wananchi, kutokana na habari zake kuandikwa na kutangazwa mara kwa mara na vyombo vya habari.
 
ni kipindi kigumu kwa wanasiasa kwani kadri uchaguzi unapoelekea ndio hatari itazidi , kama wamezuia fedha kwenye kampeni watu watazitumia kukodi majambazi kuteketeza wengine

poleni wanasiasa
 
Watu wazima wengine bwana! sasa hiyo picha hapo ni ya nini? Moderators kungekuwaga na kitufe cha opposite ya "thanks" kwa ajili ya vitu kama hivi
 
na wewe acha ujinga mweneykiti wa chama unatembea bila ulinzi na kwa nini utembee na documents za chama kwenye mkoba ??kwani huna ofisi?
 
na wewe acha ujinga mweneykiti wa chama unatembea bila ulinzi na kwa nini utembee na documents za chama kwenye mkoba ??kwani huna ofisi?

Mkuu Kigogo kama mtoto ndo kwanza anatambaa.
 
Watu wazima wengine bwana! sasa hiyo picha hapo ni ya nini? Moderators kungekuwaga na kitufe cha opposite ya "thanks" kwa ajili ya vitu kama hivi

- Unalilia Mods, Bwa! ha! ha! unaleta viroja kwa kutegemea Mods wakusaidie ha! ha! ha! eti Mods ha! ha! ha! ha! ninashkuru sana kwamba ujumbe umefika, saafi sana.

Es!
 
ni kipindi kigumu kwa wanasiasa kwani kadri uchaguzi unapoelekea ndio hatari itazidi , kama wamezuia fedha kwenye kampeni watu watazitumia kukodi majambazi kuteketeza wengine

poleni wanasiasa

- Pole pole wananchi wanaanza kuamka, kumpora Documents ni dalili za uoga nani anayeogopa sasa wananchi au viongozi mafisadi? Unaona pole pole the game starts to change!

Respect.


FMEs!
 
Kila kitu kina muda ama wakati wake. Na wakati ni ukuta. Watanzania wamechoshwa na machafu ya CCM, hivyo hakuna mbinu itakayoweza kuzuia mageuzi ya kweli.
CCM wameyataka wenyewe haya yanayotokea na yatakayotokea hapo mbeleni. Watanzania wa sasa si mabwege tena, wanaona na wanajua kinachoendelea na sasa wanataka haki na usawa wa kweli kwa kila mtanzania.
 
Hivi jamaa hana ofisi mpaka azunguke na mafile ya chama? Nitashangaa kama hawa jamaa watafika mbali. Naona wanalia lia sana ili kutaka kura za huruma.

CCM wanahitaji ngangari na wala sio kulia lia.
 
Hivi jamaa hana ofisi mpaka azunguke na mafile ya chama? Nitashangaa kama hawa jamaa watafika mbali. Naona wanalia lia sana ili kutaka kura za huruma.

CCM wanahitaji ngangari na wala sio kulia lia.

Acha pumba wewe! If you dont cry for a Nation you must then be a fisadi.
BTW inaonekana hii ni kazi ya usalama wa mafisadi....Si bure chama hiki kinawapeleka peleka.
 
Huyu mwenyekiti vp tena?
Anatembea na full doc k/koo! alitaka afoji nn maeneo ya gerezani?
Dah inasikitisha sana hana hata ulinzi! Watakuwa CCM hao bila shaka.
 
Hiyo ndio CCM maana hawa jamaa wanataka kuimaliza nchi,Wameshaona tayari hawa CCJ wanakuja kivingine kabisa ndio maana wanafanya hivyo...Na mengi sana yatatokea kwa hiki kipindi!!
 
Hivi jamaa hana ofisi mpaka azunguke na mafile ya chama? Nitashangaa kama hawa jamaa watafika mbali. Naona wanalia lia sana ili kutaka kura za huruma.

CCM wanahitaji ngangari na wala sio kulia lia.

Uhuru wa kusema chochote (U-MC) wakati mwingine ni sehemu ya tatizo, hivi una sababu ya kuwa na nyaraka ofisini ambazo haziruhusiwi kutoka nje ya ofisi? Nadhani hizi zitakuwa ni picha za ukutani kama ile ya muungwana vinginevyo nyaraka za ofisi hulazimika wakati fulani kuwa nje ya ofisi kwa sababu za ki utendaji. Unachonikumbusha: Umependa boga (CCM) hivyo umependa na ua lake pia ndio maana naona upo ku discourage wapenda nchi kwa kuwapenda walanchi.

Mwe!!
 
-Sasa je hatuna uhakika kama ni usalama wa taifa wanaolipwa kwa hela za watanzania ndo wanafanya haya?

Pia siri za chama mbona anaziweka ktk risk kiasi hicho?
 
-Sasa je hatuna uhakika kama ni usalama wa taifa wanaolipwa kwa hela za watanzania ndo wanafanya haya?

Pia siri za chama mbona anaziweka ktk risk kiasi hicho?

Inawezekana ni stage show ili ipatikane sympathy from watanzania kuwa wanadhulumiwa. Haingii akilini iweje atembee na siri za chama mkononi?? Jamani watanzania tumekuwa watoto kiasi hicho?
 
na wewe acha ujinga mweneykiti wa chama unatembea bila ulinzi na kwa nini utembee na documents za chama kwenye mkoba ??kwani huna ofisi?

Mkuu,

Hata akiamua kuziacha ofisini hizo documents TISS wakitaka watakuja kuzichukua tu. Ni watemi wale wewe!!!!!

Tiba
 
Huyu mwenyekiti vp tena?
Anatembea na full doc k/koo! alitaka afoji nn maeneo ya gerezani?
Dah inasikitisha sana hana hata ulinzi! Watakuwa CCM hao bila shaka.
Hii habari kanyaboya; leo ni April 1
 
Unamdanganya nani? Mbona mimi niko nae hapa hata dalili za kuporwa hana??? Thibitisha uwongo wako. 1 Aprili???????????????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…